Mtindo wa Serikali kutoa majibu mepesi kwa maswali mazito Bungeni na kwingineko unakera sana, ni sawa na kuwatukana Watanzania

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Serikali, hasa hii ya awamu ya tano, imekuja na mtindo mpya wa kutoa majibu mepesi sana kwa maswali mazito sana yanapoulizwa na wabunge au Watanzania kwa ujumla. Hii inakera sana. Waingereza huwa wanaita huu mtindo "kuitukana akili yangu" au insulting my intelligence.

Huko nyuma mara nyingi wenye kufanya hivi walikuwa ni jeshi la Polisi. Utawauliza kwa nini mmemkamata mtuhumiwa bila ushahidi wa kutosha watakuambia analisaidia jeshi la polisi katika upelelezi. Utawauliza ilikuwaje mahabusu aliyekuwa mzima mlipomkamata afe ghafla watasema alishikwa na homa kali ya ghafla usiku - japo mwili ulikutwa na majeraha. Sasa wengi tuliwapuuza Polisi tukiwaona ni watu wasioelimika sana ndio maana wanatoa majibu yasiyo na kichwa wala miguu.

Lakini naona kama serikali iligundua mafanikio ya Jeshi la Polisi na sasa imeiga mtindo wao wa kutoa majibu mepesi kwa maswali mazito. Siku kadhaa zilizopita sawli liliulizwa katika Bunge, kwamba kwa nini ripoti ya CAG haijafikishwa Bungeni kwa mujibu wa katiba. Chenge akajibu kwamba mbunge aliyeuliza hakusoma sheria nyingine - akiashiria ipo sheria inayopingana na matakwa ya katiba, kitu ambacho ni uongo. Juzi hapa Ziitto aliuliza sababu za kuhamisha wakala wa ndege za serikali ofisi ya raisi, na jibu linakuja kwamba raisi ndiye anapanga idara za serikali - kama vile Zitto aliuliza bila kujua hilo. Hapewi sababu ya kuhamisha Wakala wa Ndege bali anaambiwa nani anaepanga idara.

Kuna mifano mingi sana naweza kutoa, lakini acha hii miwili itoshe kwa mtu yeyote asiye mwendawazimu au mlevi tu wa madaraka au ushabiki wa kisiasa. Sasa nimejiulza, hivi serikali imefikia mahali kwa makusudi kabisa imeamua kuwatukana Watanzania hadharani, kwa kuwaambia sisi tulio madarakani tuna akili kuliko nyie tunaowaongoza, na tuna uwezo wa kujibu maswali yenu mazito kwa namna ya kuzitukana akili zenu?

Ni kwa nini serikali mara zote ione kwamba kila swali linaloulizwa sio kwa maslahi ya nchi bali nia ni kutaka kuiumbua serikali? Kwa nini serikali inaamua kuchukua mwelekeo wa mpambano (confrontational and antagonistic) kila inapoulizwa swali? Ukweli ni kwamba hizo ni tabia za serikali ya kidikteta, labda kilichobaki ni tangazo la Msigwa kwamba sasa ni rasmi Tanzania ina serikali ya kidikteta, isiyotaka kuulizwa maswali.

Ningependa kutoa onyo kwa Bunge la Tanzania na serikali kwa ujumla, msiwachukulie Watanzania kama mabwege wa kuambiwa chochote wakakubali. Msitukane akili za Watanzania, kwa kuwa mkiendelea na hii tabia, ipo siku haya yatakuja kuwageuka.
 
Mtindo huo umeanzishwa na raia na mzalendo namba moja nchi hii. Hawa wengine wameiga kwenye kile kinachofahamika kama kwenda na kasi ya mkulu. Unakumbuka majibu aliyotoa siku alipokutana na waandishi wa habari? Sasa hivi hawana hofu wala hawana muda wa kujibu majibu sahihi kwani hawategemei kura kuendelea kuwepo madarakani. Vyombo vya dola chini ya CDF watasimamia uchaguzi na wagombea wa ccm watatangazwa washindi bila kujali box la kura linasema nini.
 
... na hapo ndipo umuhimu wa Spika, NS, na Wenyeviti wanaosimamia vikao unapokuja. Ni jukumu la Spika kuitaka Serikali kutoa majibu sahihi, fasaha, na ya kueleweka (SMART) pale ubabaishaji unapojitokeza; hiyo ndio maana halisi ya KUISIMAMIA SERIKALI ambalo ni jukumu la msingi la Bunge. Bahati mbaya ndio hivyo tena, DHAIFU na hoja za kipumbavu ndio zimekuwa hoja za kujadili miaka nenda miaka rudi!
 
Serikali, hasa hii ya awamu ya tano, imekuja na mtindo mpya wa kutoa majibu mepesi sana kwa maswali mazito sana yanapoulizwa na wabunge au Watanzania kwa ujumla. Hii inakera sana. Waingereza huwa wanaita huu mtindo "kuitukana akili yangu" au insulting my intelligence.

Huko nyuma mara nyingi wenye kufanya hivi walikuwa ni jeshi la Polisi. Utawauliza kwa nini mmemkamata mtuhumiwa bila ushahidi wa kutosha watakuambia analisaidia jeshi la polisi katika upelelezi. Utawauliza ilikuwaje mahabusu aliyekuwa mzima mlipomkamata afe ghafla watasema alishikwa na homa kali ya ghafla usiku - japo mwili ulikutwa na majeraha. Sasa wengi tuliwapuuza Polisi tukiwaona ni watu wasioelimika sana ndio maana wanatoa majibu yasiyo na kichwa wala miguu.

Lakini naona kama serikali iligundua mafanikio ya Jeshi la Polisi na sasa imeiga mtindo wao wa kutoa majibu mepesi kwa maswali mazito. Siku kadhaa zilizopita sawli liliulizwa katika Bunge, kwamba kwa nini ripoti ya CAG haijafikishwa Bungeni kwa mujibu wa katiba. Chenge akajibu kwamba mbunge aliyeuliza hakusoma sheria nyingine - akiashiria ipo sheria inayopingana na matakwa ya katiba, kitu ambacho ni uongo. Juzi hapa Ziitto aliuliza sababu za kuhamisha wakala wa serikali ofisi ya raisi, na jibu linakuja kwamba raisi ndiye anapanga idara za serikali - kama vile Zitto aliuliza bila kujua hilo. Hapewi sababu ya kuhamisha Wakala wa Ndege bali anaambiwa nani anaepanga idara.

Kuna mifano mingi sana naweza kutoa, lakini acha hii miwili itoshe kwa mtu yeyote asiye mwendawazimu au mlevi tu wa madaraka au ushabiki wa kisiasa. Sasa nimejiulza, hivi serikali imefikia mahali kwa makusudi kabisa imeamua kuwatukana Watanzania hadharani, kwa kuwaambia sisi tulio madarakani tuna akili kuliko nyie tunaowaongoza, na tuna uwezo wa kujibu maswali yenu mazito kwa namna ya kuzitukana akili zenu?

Ni kwa nini serikali mara zote ione kwamba kila swali linaloulizwa sio kwa maslahi ya nchi bali nia ni kutaka kuiumbua serikali? Kwa nini serikali inaamua kuchukua mwelekeo wa mpambano (confrontational and antagonistic) kila inapoulizwa swali? Ukweli ni kwamba hizo ni tabia za serikali ya kidikteta, labda kilichobaki ni tangazo la Msigwa kwamba sasa Tanzania ina serikali ya kidikteta rasmi, isiyotaka kuulizwa maswali.

Ningependa kutoa onyo kwa Bunge la Tanzania na serikali kwa ujumla, msiwachukulie Watanzania kama mabwege wa kuambiwa chochote wakakubali. Msitukane akili za Watanzania, kwa kuwa mkiendelea na hii tabia, ipo siku haya yatakuja kuwageuka.
Sheria yoyote inayokwenda kinyume na Katiba ni Null and Void. Kilangila.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sheria yoyote inayokwenda kinyume na Katiba ni Null and Void. Kilangila.

Sent using Jamii Forums mobile app
Uliona eeh, jinsi Chenge na Jenista walivyofanya ubabaishaji kwenye swali kuhusu kwa nini ripoti ya CAG haikufika Bungeni? Yaani ubabaishaji wa hali ya juu kwa kuwa tu wanajua kuzungusha maneno sheria. Hata hivyo walijitafakari kesho yake ripoti ya CAG ikaletwa Bungeni!
 
Serikali, hasa hii ya awamu ya tano, imekuja na mtindo mpya wa kutoa majibu mepesi sana kwa maswali mazito sana yanapoulizwa na wabunge au Watanzania kwa ujumla. Hii inakera sana. Waingereza huwa wanaita huu mtindo "kuitukana akili yangu" au insulting my intelligence.

Huko nyuma mara nyingi wenye kufanya hivi walikuwa ni jeshi la Polisi. Utawauliza kwa nini mmemkamata mtuhumiwa bila ushahidi wa kutosha watakuambia analisaidia jeshi la polisi katika upelelezi. Utawauliza ilikuwaje mahabusu aliyekuwa mzima mlipomkamata afe ghafla watasema alishikwa na homa kali ya ghafla usiku - japo mwili ulikutwa na majeraha. Sasa wengi tuliwapuuza Polisi tukiwaona ni watu wasioelimika sana ndio maana wanatoa majibu yasiyo na kichwa wala miguu.

Lakini naona kama serikali iligundua mafanikio ya Jeshi la Polisi na sasa imeiga mtindo wao wa kutoa majibu mepesi kwa maswali mazito. Siku kadhaa zilizopita sawli liliulizwa katika Bunge, kwamba kwa nini ripoti ya CAG haijafikishwa Bungeni kwa mujibu wa katiba. Chenge akajibu kwamba mbunge aliyeuliza hakusoma sheria nyingine - akiashiria ipo sheria inayopingana na matakwa ya katiba, kitu ambacho ni uongo. Juzi hapa Ziitto aliuliza sababu za kuhamisha wakala wa ndege za serikali ofisi ya raisi, na jibu linakuja kwamba raisi ndiye anapanga idara za serikali - kama vile Zitto aliuliza bila kujua hilo. Hapewi sababu ya kuhamisha Wakala wa Ndege bali anaambiwa nani anaepanga idara.

Kuna mifano mingi sana naweza kutoa, lakini acha hii miwili itoshe kwa mtu yeyote asiye mwendawazimu au mlevi tu wa madaraka au ushabiki wa kisiasa. Sasa nimejiulza, hivi serikali imefikia mahali kwa makusudi kabisa imeamua kuwatukana Watanzania hadharani, kwa kuwaambia sisi tulio madarakani tuna akili kuliko nyie tunaowaongoza, na tuna uwezo wa kujibu maswali yenu mazito kwa namna ya kuzitukana akili zenu?

Ni kwa nini serikali mara zote ione kwamba kila swali linaloulizwa sio kwa maslahi ya nchi bali nia ni kutaka kuiumbua serikali? Kwa nini serikali inaamua kuchukua mwelekeo wa mpambano (confrontational and antagonistic) kila inapoulizwa swali? Ukweli ni kwamba hizo ni tabia za serikali ya kidikteta, labda kilichobaki ni tangazo la Msigwa kwamba sasa ni rasmi sasa Tanzania ina serikali ya kidikteta, isiyotaka kuulizwa maswali.

Ningependa kutoa onyo kwa Bunge la Tanzania na serikali kwa ujumla, msiwachukulie Watanzania kama mabwege wa kuambiwa chochote wakakubali. Msitukane akili za Watanzania, kwa kuwa mkiendelea na hii tabia, ipo siku haya yatakuja kuwageuka.
Kumbuka tafiti ya TWAWEZA ccm inapendwa na wenye akili ndogo na upeo mdogo kina mama wa vijijini masikini wa kutupwa

LIKUD
Lizaboni
Salary Slip
Mshana Jr
 
Kumbuka tafiti ya TWAWEZA ccm inapendwa na wenye akili ndogo na upeo mdogo kina mama wa vijijini masikini wa kutupwa

LIKUD
Lizaboni
Salary Slip
Mshana Jr
Nakubalina nawe 100%. Mtu mwenye uwezo wa kufikiri na asiye mwendawazimu wala mlevi, hata kama sio mwanachama wa upinzani, hawezi kukubaliana na haya wanayofanya CCM kwa sasa, serikalini, ndani na nje ya Bunge.
 
Back
Top Bottom