Mtihani wa kidato cha pili

Mtihani wa kidato cha pili

lusitu

Member
Joined
Jul 29, 2015
Posts
43
Reaction score
10
Jumla ya wanafunzi 490,016 leo hii 16.11.2015 wanatarajia kuanza mitihani yao ya kitaifa Nchini kote,ikumbukwe kuwa wanafunzi hawa ndio waliomaliza Darasa la saba mnamo mwaka,2013 ambapo kwa mujibu wa kumbukumbu zilizopo "NECTA" zinaonyeha waliofanya mtihani darasa la saba walikuwa 844,934.Mwaka 2012 waliofanya mtihani wa darasa la saba walikuwa 865,534 na mwaka 2014 waliofanya mtihana kidato ha pili walikuwa 405,204. Hivyo basi kwa kuangalia miaka miwili ya 2012 na 2013 utaona Jumla ya wanafunzi 1,710,472 walifanya mitihani ya Darasa la saba na kwa Mwaka 2014 na 2015 Jumla ya wanafunzi 895,220 walifanya Mtihani wa Kidato cha pili.Kwa kuangalia miaka hiyo utaona zaidi ya wanafunzi 400,000 kila mwaka wanaishia Njiani .Kwa mtazamo wangu hii si dalili njema kwa ustawi wa Taifa letu.Swali la kujiuliza je,ina maana wazazi wa wanafunzi hao hawana uwezo kuwaendeleza watoto wao au nini kimetokea. Kwakuwa JF ni sehemu ambayo baadhi yetu ni kama Darasa naomba wadau tujadili suala hli.
 
Sio lazima wote wapitie mkondo rasmi wa elimu wengine wanapitia mpango wa elimu ya sekondari kwa miaka miwili (QT) wakifaulu wanafanya mitihani ya Form Four (CSEE) wanaendelea na kitabu mbele kwa mbele. Mambo yamebadilika hata fundi makenika VETA akiamua anafika Chuo Kikuu
 
Sio lazima wote wapitie mkondo rasmi wa elimu wengine wanapitia mpango wa elimu ya sekondari kwa miaka miwili (QT) wakifaulu wanafanya mitihani ya Form Four (CSEE) wanaendelea na kitabu mbele kwa mbele. Mambo yamebadilika hata fundi makenika VETA akiamua anafika Chuo Kikuu

Mkuu hizi takwimu tulizopewa leo wanaofanya mtihani zinajumuisha na wanafunzi wa QT? kama siyo takwimu zao zikoje?
 
Mkuu hizi takwimu tulizopewa leo wanaofanya mtihani zinajumuisha na wanafunzi wa QT? kama siyo takwimu zao zikoje?

Mkuu takwimu za mleta uzi zinajumuisha waliopo kwenye mfumo rasmi tu, hao wa MEMKWA hawakujumuishwa.
Infact, kitaalamu mtihani huu kwa lugha nyingine ni upimaji tu sawa na ule wa darasa la nne (SFNE), kijana anapimwa ili kubaini ubora au udhaifu uliopo kabla ya kuendelea na hatua inayofuata.
QT wao wanafanya Mitihani yao sambamba na watahiniwa na kidato cha nne hivi sasa na matokeo yao yatatangazwa siku moja na ya Form four isipokuwa wao hawapewi cheti ila wakifaulu watapata tiketi ya kujisajili mwaka 2016 kama watahiniwa wa CSEE.
 
Back
Top Bottom