Elius W Ndabila
JF-Expert Member
- Jul 17, 2019
- 339
- 677
Na Elius Ndabila
+255768239284
Wiki iliyopita niliandika kidogo juu Elimu ya Uhusiano wa Kimataifa/DEPLOMATIC RELATIONS .Nilikuwa nimejikita zaidi kwenye kuangazia mambo ya diplomasia ya Kiuchumi. Nilifafanua zaidi juu ya mtu anayeitwa Consular ambaye ndiye anahusika sana na Diplomasia ya kiuchumi kwenye mambo ya mahusiano ya Kimataifa.
Nimepata maombi mengi kutoka kwa wasomaji wangu yanayouliza kunatofauti gani kati ya Balozi(AMBASSADOR) na CONSULAR? Maswali haya yamenipa wasaa wa kutoa majibu ijapo kwa uchache. Leo nitazungumza kinagaubaga juu ya Balozi ni nani, anavyopatikana, kazi zake na anavyoweza kufukuzwa kazi. Fuatana nami kwenye makala hii.
Balozi ni mwakilishi rasmi wa serikali ya nchi yake katika nchi nyingine. Anatumwa huko na wizara ya mambo ya nje akitazamiwa kama mwakilishi wa mkuu wa nchi inayomtuma. Kwa lugha ya kidiplosia kunakuwa na Sending state and Receiving State.
Nchi inayomtuma Balozi kwenda nchi nyingine ni Sending State lakini nchi inayompokea huyo Balozi ni Receiving State, hii ni kwa mjibu wa mkataba wa Vienna wa mwaka 1961. Katika Nyanja ya uteuzi wa Mabalozi kuna mabalozi waaina mbili, mabalozi wanaoteuliwa kwa utashi wa kisiasa na pili wanaoteuliwa kutokana na weledi wao.
Kuna balozi za aina mbili, balozi za kudumu na balozi za nchi na nchi. Balozi za kudumu ni zile zinazofunguliwa na nchi kwenda shirika au taasisi ya kimataifa kwa mfano ubalozi wa Tanzania Geneva unahudumu mahusiano ya Tanzania na Ofisi za Umoja wa Mataifa sambamba na kuhudumu Vienna, Austria. Ubalozi wa Tanzania New York unahudumu katika mahusiano ya Tanzania na Umoja wa Mataifa, lakini pia unahudumu nchi za Jamaica, Trinidad and Tobago, Barbados na Guyana.
Mapendekezo ya kumteua mtu kuwa Balozi hufanywa kwa siri kubwa. Baada ya nchi kupendekeza jina la balozi hutuma jina hilo kwenye nchi wanayotaka huyo Balozi aende jina likishafika nchi receiving state inaweza kumkubali au kumkataa. Kwa lugha ya kidiplomasia balozi anapokuwa amekataliwa wanaita Persona non grata.
Balozi anapokuwa persona non grata nchi inaweza kuwajibu nchi waliopeleka ombi la jina la balozi kuwa hatumtaki au wakamua kukaa kimya kuonyesha kuwa hawamtaki. Mwaka 1997 Brad Pitt alikuwa persona non grata kwenda China, Libya walishawahi kumbwa na hili, George Kenedy wa USA mwaka 1952 alimkata Balozi wa Soviet nion kwa ujumla orodha ni ndefu. Ukisoma the Treaty of Lausane in 1923 inaweza kukusaidia pia.
Kuna balozi za nchi na nchi ambazo hufunguliwa kufuatia makubaliano baina ya pende mbili (mutual consent) kama iliyoainishwa kwenye ibara ya pili ya VCDR 1961. Ufunguaji huu wa balozi kwa mujibu wa ibara hii unahusu pia balozi za mashirika au taasisi za kimataifa kama vile UN, UNDP, FAO, WHO, ILO n.k Mabalozi wa mashirika na taasisi za kimataifa wanaotumwa na taasisi hizo ama mashirika hayo ndani ya nchi zinazowapokea huitwa Wawakilishi Wakazi.
Mfano wa vigezo hivyo huwa ni uzalendo, uelewa mzuri wa Balozi juu ya nchi anayoteuliwa, Utamaduni wa huko n.k
Balozi hufanya kazi kwa mujibu wa Mkataba wa Vienna wa Mwaka 1961 unaohusu Mahusiano ya Kidiplomasia. Mkataba huu umeainisha Upendeleo na Kinga anazopata Balozi (Privileges and Immunities) anapokuwa katika nchi aliyopangiwa kufanya kazi zilizoanishwa katika Ibara ya Tatu (Article 3) ya Mkataba huo.
Nikwambie kitu kimoja, Balozi anakinga /immunities kubwa sawa na Rais hii ni kwa kuwa Balozi awapo kwenye nchi Fulani basi basi inahesabiwa kama ni nchi nyingine. Yaani ofisi na makazi ya balozi inakuwa kama nchi yenye territory, Population, sovereighty etc hivyo inajitawala. Hata premises/makazi za mabalozi haziruhusiwi kusogelea. Hurusiwi hata kugusa begi la Balozi wala nguo zake. Ukisoma kuanzia Ibara ya 22 ya VCDR imeeleza vizuri.
Kwa ufupi Ibara ya 22 (Article 22): Ubalozi hauwezi kuingiliwa bila ya ridhaa yake. Kwa mujibu wa Vienna Convention on Diplomatic Relations of 1961 Ubalozi unachukuliwa kama nchi ndani ya nchi. Mfano Ubalozi wa China ni sawa na China ndani ya Tanzania. Hata wakati wa vita makazi ya balozi hayapaswi kuguswa na mtu yeyote.
Ibara ya 24 (Article 24): Kumbukumbu na nyaraka za Ubalozi haziwezi kukaguliwa. Ni siri ya nchi ya hiyo iliyomtuma Balozi. Hii inahusisha mawasiliano mengine pia kama Simu, e-mail n.k Ibara ya 27 (Article 27): Begi la Kidiplomasia/Balozi haliwezi kukaguliwa. Mfano briefcase na pochi. Ndiyo maana viwanja vya ndege vina milango imeandikwa "Diplomats Only".
Ibara ya 29 (Article 29): Mabalozi wana kinga dhidi ya kukamatwa na kuwekwa kizuizini katika nchi wanapofanyia kazi. Ibara ya 30 (Article 30): Makazi binafsi (Nyumba anayoishi akiwa katika nchi anayofanyia kazi) ya mwanadiplomasia/balozi hayawezi kuingiliwa.
Ibara ya 31 (Article 31): Wanadiplomasia/ mabalozi wana kinga dhidi ya mashitaka ya ndani ya nchi isipokuwa kwa mambo yasiyohusu Ubalozi (Mambo yake binafsi kama real estate na biashara).Ibara ya 32 (Article 32): Kinga ya Balozi inaweza kuondolewa na nchi iliyomtuma tu na si nchi ambayo balozi huyo anafanya kazi yake.
Kwa maana fupi ni kuwa Balozi anaweza kuwajibishwa na nchi iliyomtuma (Sending State), mfano Balozi wetu akiharibu huko nje Rais Magufuli ndiye atakayemtumbua. Ninanukuu ibara ya 41(1) Without prejudice to their privileges and immunities, it is the duty of all persons enjoying such privileges and immunities to respect the laws and regulations of the receiving state. They also have a duty not to interfere internal affairs of the state.
Kwa kawaida anaongoza ofisi ya ubalozi ambako anasaidiwa na maafisa wengine wanaotumwa katika utaratibu wa diplomasia. Ifahamike wazi kuwa uteuzi wa mabalozi hufanyika kwa siri mno kufuatia mawasiliano baina ya Marais wa nchi mbili au kadhaa. Wizara ya Mambo ya Nje huweza kupendekeza jina kwa Rais, lakini pia Rais anaweza kumteua yeyote kutokana na vigezo atavyoona vina faa kwa mtu anayetaka kumteua.
Pamoja na kuwa Mabalozi wanayomajukumu makubwa huko wanakokuwa wanaziwakilisha nchi zao, lakini kwa mjibu wa sheria za kimataifa ambazo ndiyo msingi wa mipaka ya Balozi, zimeainisha majukumu matano tu ya Balozi.
Kwa mujibu wa ibara ya tatu ya Vienna Convention on Diplomatic Relations (VCDR 01961 kazi za balozi zimeainishwa kama ifuatavyo:
(a) Kuiwakilisha nchi iliyomtuma (Sending State) ndani ya nchi husika itakayompokea (Receiving State).Kipengele hiki pia kinahusisha uwakilishi wa taasisi au mashirika ya kimataifa ndani ya nchi husika.
(b) Kulinda maslahi ya nchi (dola) iliyomtuma ndani ya nchi iliyompokea pamoja na ya raia wake, bila ya kuathiri mipaka aliyowekewa kwa mujibu wa sheria za kimataifa. Hivyo Balozi anawajibu mkubwa katika kulinda maslahi lakini bila kuvunja miongozo mbalimbali ya kisheria. Kifungu hiki pia kinahusisha uwakilishi wa taasisi na mashirika ya kimataifa kama EU.
(c) Kujadiliana (negotiating) na serikali ya nchi iliyompokea (katika mambo mbalimbali yenye maslahi baina yao). Kunapotokea jambo lolote basi Balozi ana wajibu mkubwa kuka meza moja na taifa hilo kuangalia namna ya kuondoa changamoto hizo.Kifungu hiki ndicho kinawapa uwezo mabalozi kuingia na kusaini mikataba mbalimbali kwa niaba ya Marais wa nchi husika ama taasisi za nchi husika lakini bada ya mashauriano na nchi yake..
(d) Kuenenda na taratibu zote za kisheria katika kufuatilia yanayojitokeza ndani ya nchi iliyompokea na kutolea taarifa yale yanayojiri kwa nchi iliyomtuma. Balozi awajibu wa kutoa tarifa kwa nchi yake kama kuna jambo aliona kuwa ni lazima lifahamike. Na si kila jambo atalisema hasa ambalo si wajibu wake kulisemea.
Kifungu hiki pia kinahusisha hadi mashirika na taasisi za kimataifa kama EU.Kifungu hiki kinamaanisha kuwa mabalozi au wawakilishi hawa ndiyo macho na masikio ya marais, wakuu wa serikali, taasisi na mashirika ya kimataifa yaliyowateua kwenda katika nchi husika.
(e) Kuendeleza mahusiano ya kirafiki kati ya nchi iliyomtuma (Sending State) na nchi iliyompokea (Receiving State) sambamba na kuendeleza mahusiano ya kiuchumi, kiutamaduni na kisayansi
Balozi anaweza kuachana na kazi yake ya Ubalozi kwa muda wake a utumishi kuisha, kwa kutenguliwa au receiving state kumumfukuza. Na kwa mjibu wa sheria ukikoma kuwa Balozi hapo hapo immunity zako zinakuwa waved/ondolewa kinga.
Nihitimishe kwa kusema Balozi ni mkubwa kuliko Consular, ili Consular aweze kufanya majukumu yake vizuri anahitaji Balozi anayemsimamia vizuri. Uchumi wa dunia ya leo unategemea zaidi diplomasia ya kiuchumi na si vinginevyo. Balozi zinapaswa zisilale wao ndio nguzo ya uchumi hasa kwa fedha za kigeni. Mabalozi wakitimiza vizuri kazi zao Tanzania utalii halitakuwa tatizo na pia nchi itapata wawekezaji wengi ka kuwa kila kitu kipo.
+255768239284
Wiki iliyopita niliandika kidogo juu Elimu ya Uhusiano wa Kimataifa/DEPLOMATIC RELATIONS .Nilikuwa nimejikita zaidi kwenye kuangazia mambo ya diplomasia ya Kiuchumi. Nilifafanua zaidi juu ya mtu anayeitwa Consular ambaye ndiye anahusika sana na Diplomasia ya kiuchumi kwenye mambo ya mahusiano ya Kimataifa.
Nimepata maombi mengi kutoka kwa wasomaji wangu yanayouliza kunatofauti gani kati ya Balozi(AMBASSADOR) na CONSULAR? Maswali haya yamenipa wasaa wa kutoa majibu ijapo kwa uchache. Leo nitazungumza kinagaubaga juu ya Balozi ni nani, anavyopatikana, kazi zake na anavyoweza kufukuzwa kazi. Fuatana nami kwenye makala hii.
Balozi ni mwakilishi rasmi wa serikali ya nchi yake katika nchi nyingine. Anatumwa huko na wizara ya mambo ya nje akitazamiwa kama mwakilishi wa mkuu wa nchi inayomtuma. Kwa lugha ya kidiplosia kunakuwa na Sending state and Receiving State.
Nchi inayomtuma Balozi kwenda nchi nyingine ni Sending State lakini nchi inayompokea huyo Balozi ni Receiving State, hii ni kwa mjibu wa mkataba wa Vienna wa mwaka 1961. Katika Nyanja ya uteuzi wa Mabalozi kuna mabalozi waaina mbili, mabalozi wanaoteuliwa kwa utashi wa kisiasa na pili wanaoteuliwa kutokana na weledi wao.
Kuna balozi za aina mbili, balozi za kudumu na balozi za nchi na nchi. Balozi za kudumu ni zile zinazofunguliwa na nchi kwenda shirika au taasisi ya kimataifa kwa mfano ubalozi wa Tanzania Geneva unahudumu mahusiano ya Tanzania na Ofisi za Umoja wa Mataifa sambamba na kuhudumu Vienna, Austria. Ubalozi wa Tanzania New York unahudumu katika mahusiano ya Tanzania na Umoja wa Mataifa, lakini pia unahudumu nchi za Jamaica, Trinidad and Tobago, Barbados na Guyana.
Mapendekezo ya kumteua mtu kuwa Balozi hufanywa kwa siri kubwa. Baada ya nchi kupendekeza jina la balozi hutuma jina hilo kwenye nchi wanayotaka huyo Balozi aende jina likishafika nchi receiving state inaweza kumkubali au kumkataa. Kwa lugha ya kidiplomasia balozi anapokuwa amekataliwa wanaita Persona non grata.
Balozi anapokuwa persona non grata nchi inaweza kuwajibu nchi waliopeleka ombi la jina la balozi kuwa hatumtaki au wakamua kukaa kimya kuonyesha kuwa hawamtaki. Mwaka 1997 Brad Pitt alikuwa persona non grata kwenda China, Libya walishawahi kumbwa na hili, George Kenedy wa USA mwaka 1952 alimkata Balozi wa Soviet nion kwa ujumla orodha ni ndefu. Ukisoma the Treaty of Lausane in 1923 inaweza kukusaidia pia.
Kuna balozi za nchi na nchi ambazo hufunguliwa kufuatia makubaliano baina ya pende mbili (mutual consent) kama iliyoainishwa kwenye ibara ya pili ya VCDR 1961. Ufunguaji huu wa balozi kwa mujibu wa ibara hii unahusu pia balozi za mashirika au taasisi za kimataifa kama vile UN, UNDP, FAO, WHO, ILO n.k Mabalozi wa mashirika na taasisi za kimataifa wanaotumwa na taasisi hizo ama mashirika hayo ndani ya nchi zinazowapokea huitwa Wawakilishi Wakazi.
Mfano wa vigezo hivyo huwa ni uzalendo, uelewa mzuri wa Balozi juu ya nchi anayoteuliwa, Utamaduni wa huko n.k
Balozi hufanya kazi kwa mujibu wa Mkataba wa Vienna wa Mwaka 1961 unaohusu Mahusiano ya Kidiplomasia. Mkataba huu umeainisha Upendeleo na Kinga anazopata Balozi (Privileges and Immunities) anapokuwa katika nchi aliyopangiwa kufanya kazi zilizoanishwa katika Ibara ya Tatu (Article 3) ya Mkataba huo.
Nikwambie kitu kimoja, Balozi anakinga /immunities kubwa sawa na Rais hii ni kwa kuwa Balozi awapo kwenye nchi Fulani basi basi inahesabiwa kama ni nchi nyingine. Yaani ofisi na makazi ya balozi inakuwa kama nchi yenye territory, Population, sovereighty etc hivyo inajitawala. Hata premises/makazi za mabalozi haziruhusiwi kusogelea. Hurusiwi hata kugusa begi la Balozi wala nguo zake. Ukisoma kuanzia Ibara ya 22 ya VCDR imeeleza vizuri.
Kwa ufupi Ibara ya 22 (Article 22): Ubalozi hauwezi kuingiliwa bila ya ridhaa yake. Kwa mujibu wa Vienna Convention on Diplomatic Relations of 1961 Ubalozi unachukuliwa kama nchi ndani ya nchi. Mfano Ubalozi wa China ni sawa na China ndani ya Tanzania. Hata wakati wa vita makazi ya balozi hayapaswi kuguswa na mtu yeyote.
Ibara ya 24 (Article 24): Kumbukumbu na nyaraka za Ubalozi haziwezi kukaguliwa. Ni siri ya nchi ya hiyo iliyomtuma Balozi. Hii inahusisha mawasiliano mengine pia kama Simu, e-mail n.k Ibara ya 27 (Article 27): Begi la Kidiplomasia/Balozi haliwezi kukaguliwa. Mfano briefcase na pochi. Ndiyo maana viwanja vya ndege vina milango imeandikwa "Diplomats Only".
Ibara ya 29 (Article 29): Mabalozi wana kinga dhidi ya kukamatwa na kuwekwa kizuizini katika nchi wanapofanyia kazi. Ibara ya 30 (Article 30): Makazi binafsi (Nyumba anayoishi akiwa katika nchi anayofanyia kazi) ya mwanadiplomasia/balozi hayawezi kuingiliwa.
Ibara ya 31 (Article 31): Wanadiplomasia/ mabalozi wana kinga dhidi ya mashitaka ya ndani ya nchi isipokuwa kwa mambo yasiyohusu Ubalozi (Mambo yake binafsi kama real estate na biashara).Ibara ya 32 (Article 32): Kinga ya Balozi inaweza kuondolewa na nchi iliyomtuma tu na si nchi ambayo balozi huyo anafanya kazi yake.
Kwa maana fupi ni kuwa Balozi anaweza kuwajibishwa na nchi iliyomtuma (Sending State), mfano Balozi wetu akiharibu huko nje Rais Magufuli ndiye atakayemtumbua. Ninanukuu ibara ya 41(1) Without prejudice to their privileges and immunities, it is the duty of all persons enjoying such privileges and immunities to respect the laws and regulations of the receiving state. They also have a duty not to interfere internal affairs of the state.
Kwa kawaida anaongoza ofisi ya ubalozi ambako anasaidiwa na maafisa wengine wanaotumwa katika utaratibu wa diplomasia. Ifahamike wazi kuwa uteuzi wa mabalozi hufanyika kwa siri mno kufuatia mawasiliano baina ya Marais wa nchi mbili au kadhaa. Wizara ya Mambo ya Nje huweza kupendekeza jina kwa Rais, lakini pia Rais anaweza kumteua yeyote kutokana na vigezo atavyoona vina faa kwa mtu anayetaka kumteua.
Pamoja na kuwa Mabalozi wanayomajukumu makubwa huko wanakokuwa wanaziwakilisha nchi zao, lakini kwa mjibu wa sheria za kimataifa ambazo ndiyo msingi wa mipaka ya Balozi, zimeainisha majukumu matano tu ya Balozi.
Kwa mujibu wa ibara ya tatu ya Vienna Convention on Diplomatic Relations (VCDR 01961 kazi za balozi zimeainishwa kama ifuatavyo:
(a) Kuiwakilisha nchi iliyomtuma (Sending State) ndani ya nchi husika itakayompokea (Receiving State).Kipengele hiki pia kinahusisha uwakilishi wa taasisi au mashirika ya kimataifa ndani ya nchi husika.
(b) Kulinda maslahi ya nchi (dola) iliyomtuma ndani ya nchi iliyompokea pamoja na ya raia wake, bila ya kuathiri mipaka aliyowekewa kwa mujibu wa sheria za kimataifa. Hivyo Balozi anawajibu mkubwa katika kulinda maslahi lakini bila kuvunja miongozo mbalimbali ya kisheria. Kifungu hiki pia kinahusisha uwakilishi wa taasisi na mashirika ya kimataifa kama EU.
(c) Kujadiliana (negotiating) na serikali ya nchi iliyompokea (katika mambo mbalimbali yenye maslahi baina yao). Kunapotokea jambo lolote basi Balozi ana wajibu mkubwa kuka meza moja na taifa hilo kuangalia namna ya kuondoa changamoto hizo.Kifungu hiki ndicho kinawapa uwezo mabalozi kuingia na kusaini mikataba mbalimbali kwa niaba ya Marais wa nchi husika ama taasisi za nchi husika lakini bada ya mashauriano na nchi yake..
(d) Kuenenda na taratibu zote za kisheria katika kufuatilia yanayojitokeza ndani ya nchi iliyompokea na kutolea taarifa yale yanayojiri kwa nchi iliyomtuma. Balozi awajibu wa kutoa tarifa kwa nchi yake kama kuna jambo aliona kuwa ni lazima lifahamike. Na si kila jambo atalisema hasa ambalo si wajibu wake kulisemea.
Kifungu hiki pia kinahusisha hadi mashirika na taasisi za kimataifa kama EU.Kifungu hiki kinamaanisha kuwa mabalozi au wawakilishi hawa ndiyo macho na masikio ya marais, wakuu wa serikali, taasisi na mashirika ya kimataifa yaliyowateua kwenda katika nchi husika.
(e) Kuendeleza mahusiano ya kirafiki kati ya nchi iliyomtuma (Sending State) na nchi iliyompokea (Receiving State) sambamba na kuendeleza mahusiano ya kiuchumi, kiutamaduni na kisayansi
Balozi anaweza kuachana na kazi yake ya Ubalozi kwa muda wake a utumishi kuisha, kwa kutenguliwa au receiving state kumumfukuza. Na kwa mjibu wa sheria ukikoma kuwa Balozi hapo hapo immunity zako zinakuwa waved/ondolewa kinga.
Nihitimishe kwa kusema Balozi ni mkubwa kuliko Consular, ili Consular aweze kufanya majukumu yake vizuri anahitaji Balozi anayemsimamia vizuri. Uchumi wa dunia ya leo unategemea zaidi diplomasia ya kiuchumi na si vinginevyo. Balozi zinapaswa zisilale wao ndio nguzo ya uchumi hasa kwa fedha za kigeni. Mabalozi wakitimiza vizuri kazi zao Tanzania utalii halitakuwa tatizo na pia nchi itapata wawekezaji wengi ka kuwa kila kitu kipo.