Msimu mpya wa Ligi Kuu ya NBC kuanzia Septemba 16, 2025

Msimu mpya wa Ligi Kuu ya NBC kuanzia Septemba 16, 2025

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Ligi Kuu ya NBC kwa msimu wa 2025/2026 inatarajiwa kuanza rasmi Septemba 16, 2025, ambapo mashabiki wa soka nchini watashuhudia tena ushindani mkali miongoni mwa vilabu vikubwa na vidogo, huku kila timu ikisaka pointi muhimu kuanzia hatua za mwanzo za ligi hiyo maarufu nchini Tanzania.

Sasa hivi, timu ziko katika harakati za kusajili wachezaji mbalimbali ili kuboresha vikosi vyao na kuhakikisha kuwa zinaingia kwenye msimu mpya zikiwa na nguvu na ushindani wa kutosha.

Unatamani timu yako ianze na nani?
 
Bodi ihakikishe marefa walio onesha mapungufu msimu uliopita basi wanaondolewa pia ihakikishe ratiba inayobalance kwa timu zote, pia ihakikishe inatunga sheria kwa waamuzi watakaoonekana kutenda makosa wakati wa kutafsiri sheria 17 ikiwezekana washushwe daraja.

Kabla ya ligi kuanza basi tunaomba Serikali isimamie sheria za TFF ili karia asigombee tena kugombea na kushnda kwa karia kutatupa taswira mbaya kama nchi kwamba mtu yeyote tu anaweza kujiongezea muda wa kuhudumu ktk shirikisho ingawa muda wake ushaisha.

BODI ihakikishe inasimamia kanuni zote kwa usahihi bila kupendelea vilabu viwili vya simba au yanga kufanya hivyo kutaipa hadhi dabi yetu ya kariakoo na ligi kwa ujumla.

kwenda kinyume na haya kunauwezekano wa nchi yetu kufungiwa kushiriki mashndano ya kimataifa
 
Siku atakayo ondoka Karia pale Tff basi Katibu wake Kidau ndani ya masaa 24 atakua amesha fungashiwa vilago.
 
Ligi Kuu Ya Bongo Bado Ipo?
Nikajua Ilishafungiwaga Na FIFA?
Wanaofuatilia Ligi Ya Bongo Wanamioyo Migumu,kama Wanachama Wa Ccm,kuwa Mfuasi Wa Hivyo Vitu Inakubidi Akili Uweke Pembeni Maana Haitakiwi.
 
Kila nikikumbuka kuwa Karia ataendelea kuwa boss mkuu wa TFF kwa miaka mingine minne, nakosa hata shauku ya kufuatilia mpira wa kibongo naona ni kuikosea heshima akili na ufahamu wangu kuhusu mpira.
Ni kwamba huyo Karia atakaza fuvu lake na hivyo kuipuuza sera ya michezo iliyoweka utaratibu wa mihula miwili pekee kwa viongozi wa michezo kuhudumu kwenye nafasi zao?

Ni kwamba Mwana FA atamkingia kifua ili auvuruge utaratibu wa miaka yote, na ambao upo chini ya BMT; kwa sababu tu ya uswahiba na usimba wao? Ikitokea hivyo basi itakuwa ni dharau kubwa sana kuwahi kutokea kwenye mpira wetu.

Binafsi namshauri Wallace Kariabaachane na uroho wake wa madaraka. Pia afahamu TFF ni shirikisho la mpira wa miguu nchini! Na siyo NGO yake ya kupiga hela.
 
Bodi ihakikishe marefa walio onesha mapungufu msimu uliopita basi wanaondolewa pia ihakikishe ratiba inayobalance kwa timu zote, pia ihakikishe inatunga sheria kwa waamuzi watakaoonekana kutenda makosa wakati wa kutafsiri sheria 17 ikiwezekana washushwe daraja.

Kabla ya ligi kuanza basi tunaomba Serikali isimamie sheria za TFF ili karia asigombee tena kugombea na kushnda kwa karia kutatupa taswira mbaya kama nchi kwamba mtu yeyote tu anaweza kujiongezea muda wa kuhudumu ktk shirikisho ingawa muda wake ushaisha.

BODI ihakikishe inasimamia kanuni zote kwa usahihi bila kupendelea vilabu viwili vya simba au yanga kufanya hivyo kutaipa hadhi dabi yetu ya kariakoo na ligi kwa ujumla.

kwenda kinyume na haya kunauwezekano wa nchi yetu kufungiwa kushiriki mashndano ya kimataifa
Simba na ya ga nao wacheze saa 8 mchana.
Mambo yaigi kusimama wiki5 hatutaki kuyao a tena.
Tatu malogo asichezeshe mechi tena nbc ligi kuu
 
Ni kwamba huyo Karia atakaza fuvu lake na hivyo kuipuuza sera ya michezo iliyoweka utaratibu wa mihula miwili pekee kwa viongozi wa michezo kuhudumu kwenye nafasi zao?

Ni kwamba Mwana FA atamkingia kifua ili auvuruge utaratibu wa miaka yote, na ambao upo chini ya BMT; kwa sababu tu ya uswahiba na usimba wao? Ikitokea hivyo basi itakuwa ni dharau kubwa sana kuwahi kutokea kwenye mpira wetu.

Binafsi namshauri Wallace Kariabaachane na uroho wake wa madaraka. Pia afahamu TFF ni shirikisho la mpira wa miguu nchini! Na siyo NGO yake ya kupiga hela.
Kwa mazingira jinsi yalivyosetiwa sasa hivi wewe unaona hilo la yeye kuiongoza tff kwa muhula mwingine wa haramu linashindikana?

Ndugu nafikiri wewe unatambua vilivyo jinsi gani hii nchi imeoza kila mahali na ni kawaida sana kwa jambo la ajabu au maamuzi ya ajabu kufanyika hili tu kundi fulani la watu wachache waendelee kunufaika.
 
Back
Top Bottom