Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 11,882
- 20,538
Nikitafakari juu ya muungano wa Seifu na Zitto, sikosi kufikiria ni jinsi gani wataendesha chama cha ACT-Wazalendo kwa kuwa na lugha moja. Najiuliza kama ni Zitto au Seifu ambaye atakubali sera za mwenzake, au wataamua kuzichanganya ili kukipa chama mwelekeo mpya. Angalau wana mambo kadhaa ambayo wanafanana - dini moja hivyo kukua katika malezi yanayofanana. Na wote wana historia ya kufukuzwa toka vyama vyao vya awali, CCM na Chadema, na huenda hii ikawaunganisha sana. Wameanza vizuri kwa Seifu kupewa kadi namna moja - japo haieleweki hii kadi namba moja ilikuwa inamngojea nani na Zitto amekuwa na kadi namba ngapi siku zote hizi!
Ila sasa, kwa upande wa pili, wengi watasema Zitto na Seifu wote ni wabishi sana, na kila mmoja ana hulka ya kuona bila yeye chama hakiwezi kwenda popote! Hilo itabidi waliangalie kwa makini.
Zaidi ya hapo, hatusahau kwamba siku zote Seif amekuwa na msimamo wa kutaka kuvunja muungano wa bara na visiwani, na mtazamo wa jino kwa jino pale anapohisi kuonewa na serikali. Je, tutarajie mabadiliko ya itikadi ya ACT-Wazalendo kuelekea kuvunja muungano na sera za jino kwa jino?
Ila sasa, kwa upande wa pili, wengi watasema Zitto na Seifu wote ni wabishi sana, na kila mmoja ana hulka ya kuona bila yeye chama hakiwezi kwenda popote! Hilo itabidi waliangalie kwa makini.
Zaidi ya hapo, hatusahau kwamba siku zote Seif amekuwa na msimamo wa kutaka kuvunja muungano wa bara na visiwani, na mtazamo wa jino kwa jino pale anapohisi kuonewa na serikali. Je, tutarajie mabadiliko ya itikadi ya ACT-Wazalendo kuelekea kuvunja muungano na sera za jino kwa jino?