Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,912
- 30,253
MSIKITI WA MFALME MOHAMED WA SITA
Naangalia picha ya msikiti uliojengwa ndani ya viwanja vya Kinondoni Muslim School akili yangu inarudi nyuma hadi miezi ya mwisho ya mwaka wa 1968.
Mwaka wa 1968 miezi mitatu ya mwisho wa mwaka ndani ya darasa moja katika shule hiyo iliyojengwa na East African Muslim Welfare Society (EAMWS) marehemu Tewa Said Tewa alikuwa anaongoza mkutano wa EAMWS yeye akiwa Mwenyekiti katika nafasi yake kama Rais wa jumuia hiyo kwa upande wa Tanganyika agenda iliyokuwa mezani ikiwa nini kifanyike kuepusha EAMWS isivunjike kwa kuwa mikoa mingi ilikuwa imejitoa baada ya kuzuka mgogoro ulioanzia tawi la EAMWS Bukoba.
Kisa hiki ni maarufu sana kwa Waislam.
Baadhi ya wajumbe katika mkutano ule walichangia mjadala katika mkutano ule wakibubujikwa na machozi kwani ilikuwa wazi EAMWS imefikia mwisho wake na inavunjika.
Kilichokuwa kinawaliza ni kuwa ule upande uliokuwa umejitenga ulikuwa umekataa sulhu wao wakishikilia kuwa EAMWS lazima ivunjwe hawana hajanayo.
Wakati ule EAMWS ilikuwa inajenga Chuo Kikuu katika uwanja wake wa Chang'ombe na kuvunjika kwake maana yake ni kuwa mradi ule na miradi mingine ya kujenga shule nchi nzima ndiyo itakuwa mwisho na Waislam watarudi palepale walipokuwa wakati wa ukoloni kwa kukosa elimu waliyotegemea sasa wataipata kwa juhudi zao wenyewe kupitia EAMWS na miradi ya elimu iliyokuwa inatekelezwa kinara wa juhudi hizi akiwa Mufti Sheikh Hassan bin Ameir.
Katika viongozi wa EAMWS waliokuwapo katika mgogoro ule walio hai ni wawili - Bilal Rehani Waikela na Advocate Mussa Kwikima wote kutoka Tabora na huu ndiyo mkoa ambao haukujitoa katika EAMWS.
EAMWS ikavunjika na Chuo Kikuu hakikujengwa na shule zilizokuwa zinajengwa zikasimama.
Leo ndani ya ardhi ile ya EAMWS pale Kinondoni Muslim School umesimama msikiti mkubwa wa fahari na wa kujivunia.
Naangalia picha ya msikiti uliojengwa ndani ya viwanja vya Kinondoni Muslim School akili yangu inarudi nyuma hadi miezi ya mwisho ya mwaka wa 1968.
Mwaka wa 1968 miezi mitatu ya mwisho wa mwaka ndani ya darasa moja katika shule hiyo iliyojengwa na East African Muslim Welfare Society (EAMWS) marehemu Tewa Said Tewa alikuwa anaongoza mkutano wa EAMWS yeye akiwa Mwenyekiti katika nafasi yake kama Rais wa jumuia hiyo kwa upande wa Tanganyika agenda iliyokuwa mezani ikiwa nini kifanyike kuepusha EAMWS isivunjike kwa kuwa mikoa mingi ilikuwa imejitoa baada ya kuzuka mgogoro ulioanzia tawi la EAMWS Bukoba.
Kisa hiki ni maarufu sana kwa Waislam.
Baadhi ya wajumbe katika mkutano ule walichangia mjadala katika mkutano ule wakibubujikwa na machozi kwani ilikuwa wazi EAMWS imefikia mwisho wake na inavunjika.
Kilichokuwa kinawaliza ni kuwa ule upande uliokuwa umejitenga ulikuwa umekataa sulhu wao wakishikilia kuwa EAMWS lazima ivunjwe hawana hajanayo.
Wakati ule EAMWS ilikuwa inajenga Chuo Kikuu katika uwanja wake wa Chang'ombe na kuvunjika kwake maana yake ni kuwa mradi ule na miradi mingine ya kujenga shule nchi nzima ndiyo itakuwa mwisho na Waislam watarudi palepale walipokuwa wakati wa ukoloni kwa kukosa elimu waliyotegemea sasa wataipata kwa juhudi zao wenyewe kupitia EAMWS na miradi ya elimu iliyokuwa inatekelezwa kinara wa juhudi hizi akiwa Mufti Sheikh Hassan bin Ameir.
Katika viongozi wa EAMWS waliokuwapo katika mgogoro ule walio hai ni wawili - Bilal Rehani Waikela na Advocate Mussa Kwikima wote kutoka Tabora na huu ndiyo mkoa ambao haukujitoa katika EAMWS.
EAMWS ikavunjika na Chuo Kikuu hakikujengwa na shule zilizokuwa zinajengwa zikasimama.
Leo ndani ya ardhi ile ya EAMWS pale Kinondoni Muslim School umesimama msikiti mkubwa wa fahari na wa kujivunia.