Msaada wa vitanda na magodoro 30 watolewa Muhimbili

Msaada wa vitanda na magodoro 30 watolewa Muhimbili

MsamiKowalski

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2015
Posts
285
Reaction score
56
attachment.php
attachment.php

Kampuni ya Golden Fleet LTD na Golden Coach LTD Wakabidi magodoro 30 na vitanda 30 Muhimbili Leo.

Mkurugenzi mtendaji wa kampunu hizo Bw.Mohammed Raza Dewj (kulia) akimkabidhi Afisa uuguzi wa idara ya uuguzi na Ubora wa Taifa muhimbili Bi.Mariana Makanda(kushoto).
 

Attachments

  • mo.jpg
    mo.jpg
    55.1 KB · Views: 2,974
  • moo.jpg
    moo.jpg
    53.5 KB · Views: 2,954
Safi sana. Nadhani wale wagonjwa waliokuwa wanalala chini inabidi walazwe kwenye hivyo vitanda na wapige picha watuoneshe maana hawachelewi kuvihamishia kwenye hospitali zao binafisi
 
Najua ukihoji 'juhudi' kama hizi utaonekana mbaya lakini ukweli ni kwamba mfumo uliopo ndio unawezesha mbunge asiye na msaada wowote kilipwa milioni 250 kama kiinua mgongo wa miaka mitano huku television na magazeti yote yakitanda picha za 'mtoa msaada' wa shilingi milioni tano!
Sasa hapo ni Muhimbili kwa vile rais alienda, na Nkasi je mbona hata syring na panadol hawana!? Ni vizuri kuuangali mfumo mzima badala ya kutarget pages za mbele za media.
 
Posho za vkao vya bunge vfutwe coz n sehm ya kaz yao kwan wana kaz nyngn??
 
Posho za wabunge zifutwe,, wao siwanajiita watetezi wa wananchi ??? basi tuanzie kwao kupunguza matumizi ili kuwasaidia wananchi wasilale chini na hospitali zetu zipate panadol na aspirin...
 
Safi sana. Nadhani wale wagonjwa waliokuwa wanalala chini inabidi walazwe kwenye hivyo vitanda na wapige picha watuoneshe maana hawachelewi kuvihamishia kwenye hospitali zao binafisi
Siyo awamu hii.
 
Asanteni sana golden fleet, sasa tatizo la kulala chini limepata utatuzi Mungu awajalie.
 
Ni jambo la kuleta matumaini.

Mfano Wabunge na Madiwani wote wangefanya harambee ya kuchangia vifaa, nafikiri Hospitali zote zingekuwa na vifaa vya kutosha.
 
Nkasi mbali lote huko????
Temeke tu hapo..... wagonjwa wanalala chini na wala sio jambo la ajabu kuambiwa xray machine haifanyi kazi


Najua ukihoji 'juhudi' kama hizi utaonekana mbaya lakini ukweli ni kwamba mfumo uliopo ndio unawezesha mbunge asiye na msaada wowote kilipwa milioni 250 kama kiinua mgongo wa miaka mitano huku television na magazeti yote yakitanda picha za 'mtoa msaada' wa shilingi milioni tano!
Sasa hapo ni Muhimbili kwa vile rais alienda, na Nkasi je mbona hata syring na panadol hawana!? Ni vizuri kuuangali mfumo mzima badala ya kutarget pages za mbele za media.
 
Posho za wabunge zifutwe,, wao siwanajiita watetezi wa wananchi ??? basi tuanzie kwao kupunguza matumizi ili kuwasaidia wananchi wasilale chini na hospitali zetu zipate panadol na aspirin...


Naafikiana nawe 100% nao walipwe kama watumishi wenngine wa umma, kiuhalisia ni kuwa wabunge wanaliibia sana taifa hili kutokana na kulipwa posho nyingi zisizo na tija kwa taifa, halafu pia baada ya vikao vya bunge wanakuwa kwenye shughuli zao binafsi zaidi kuliko kuwahudumia wapiga kura wao, ushahidi wa haya ni pale unaona wabunge wengi hawapo majimboni ila wanaishi Dar 90%++ ya maisha yao
 
attachment.php
attachment.php

Kampuni ya Golden Fleet LTD na Golden Coach LTD Wakabidi magodoro 30 na vitanda 30 Muhimbili Leo.

Mkurugenzi mtendaji wa kampunu hizo Bw.Mohammed Raza Dewj (kulia) akimkabidhi Afisa uuguzi wa idara ya uuguzi na Ubora wa Taifa muhimbili Bi.Mariana Makanda(kushoto).

Wagonjwa wanalala chini kwa maana ya kwenye magodoro yaliyowekwa chini na sio sakafuni. Na inawezekana hili linatokana na kukosa nafasi ya kuweka vitanda na sio kuwa vitanda hakuna. Piga picha vitanda vijazane wodini au kwenye corridor upitaji utakuwaje. Sual ni aidha kuongeza majengo au kuwapatia watanzania maisha bora na elimu ya kutosha ya afya ili wasiwe wengi huko hospitalini.

 
Last edited by a moderator:
Ukiongeza vitanda lazima uongeze na majengo ya wodi za kuweka hivyo vitanda.

kwani waliokuwa wamelala chini ..walikuwa wamelala nje ya wodi au ndani ya wodi
ila chini ya sakafu...? we wapi bana.
 
Hao waangalie sana raisi wetu magufuli wanakujaga na gia hiyohiyo
 
Safi sana. Nadhani wale wagonjwa waliokuwa wanalala chini inabidi walazwe kwenye hivyo vitanda na wapige picha watuoneshe maana hawachelewi kuvihamishia kwenye hospitali zao binafisi

Na hata vitanda mnahujumiwa tu?? Wagongwa wanalala chini kwenye Hospitali ya Taifa!! Inasikitisha kweli
 
Wabunge wetu ni vilaza sana aisee,, yaana sijawahi kuona mbunge anaenda hata hapo kutoa msaada
 
Back
Top Bottom