Msaada wa mawazo: Ndoto inayomtisha mke wangu kumbe inahusu familia yangu

Kiebuta

Member
Jun 12, 2019
36
188
Wakuu habari za majukumu ya kulijenga taifa letu.
Hivi karibuni nilipata kuhama sehemu niliyokuwa na kuhamia sehemu nyingine kikazi, na Mungu ni mwema nafasi (cheo) kilikuwa ni cha juu tofauti na awali na chenye masirahi zaidi.

Sasa nmelipoti huku na kwakweli niliwajulisha ndugu zangu wa karibu na walinipongeza, mke wangu pia alimjulisha mama yake (ndo mtu yuko nae karibu zaidi na hawafichani kitu)
Sasa nikapanga safari kwenda nyumbani hivi karibuni na nilimweleza mke wangu kuwa nitaenda hom kuwasalimia.

Leo katika maongezi wife amenieleza kuwa juzi aliota ndoto kuhusu mimi na haikuwa nzuri, na katika ndoto kuna mtu alimueleza vitu hivyo ananiomba nikifika niwe makini sana, nimshirikishe Mungu na nisile kitu bila kuomba.
Nikajalibu kumdadisi ili anisimulie lakini sikufanikiwa, alikataa kabsa na kusema hawezi kunisimulia.

Wazo likanijia na kuhisi hii ndoto ni lazima amemsimulia mama yake kwani ndiyo mshauri wake namba moja,
Mimi huwa NIMEITRACK SIMU YA WIFE.
Hivyo nikaingia kwenye call zake, kwel nikakuta call ya mama yake wameongea kwa muda sana, nikadownload hayo maongezi, bahati mbaya yalikuwa kilugha chao na mimi sikielewi...
Nikamtumia rafiki yangu mmoja ambaye ni kabila sawa na wife hivyo akaitafsiri yale maongezi, yalikuwa hivi kiufupi

" Mama juzi nilivyoenda kulala kuna bundi alikuwa akilia hapa kwangu, na nilikemea akaondoka, ila nikapitiwa na usingizi mzito ambapo kuna ndoto ilinijia niko napigiwa ramri, na kuna sauti inaniambia wanamuita mumeo kwao kuna mambo anaenda kufanyiwa, moja ya anaemuita ni mama yake mzazi, nyumbani siyo kuzuri awe makini" mama yake akamuuliza umemwambia, wife akasema hapana, bhasi wakakubaliana wasiniambie ila waniombee tu Mungu aniepushe...

Wanajamvi, ninaomba ushauri wenu...mke hajui kama tayari ninajua alichoota, na pili kwa upande wangu siamini sana katika ushirikina, anaeweza tafsiri hiyo ndoto msaada jamani...
Mpaka sasa nimeahilisha safar zote nilizokuwa nimepanga.
 
Piga kimya mkuu mwanamke wako anakupenda sana
Wakuu habari za majukumu ya kulijenga taifa letu.
Hivi karibuni nilipata kuhama sehemu niliyokuwa na kuhamia sehemu nyingine kikazi, na Mungu ni mwema nafasi (cheo) kilikuwa ni cha juu tofauti na awali na chenye masirahi zaidi.

Sasa nmelipoti huku na kwakweli niliwajulisha ndugu zangu wa karibu na walinipongeza, mke wangu pia alimjulisha mama yake (ndo mtu yuko nae karibu zaidi na hawafichani kitu)
Sasa nikapanga safari kwenda nyumbani hivi karibuni na nilimweleza mke wangu kuwa nitaenda hom kuwasalimia.

Leo katika maongezi wife amenieleza kuwa juzi aliota ndoto kuhusu mimi na haikuwa nzuri, na katika ndoto kuna mtu alimueleza vitu hivyo ananiomba nikifika niwe makini sana, nimshirikishe Mungu na nisile kitu bila kuomba.
Nikajalibu kumdadisi ili anisimulie lakini sikufanikiwa, alikataa kabsa na kusema hawezi kunisimulia.

Wazo likanijia na kuhisi hii ndoto ni lazima amemsimulia mama yake kwani ndiyo mshauri wake namba moja,
Mimi huwa NIMEITRACK SIMU YA WIFE.
Hivyo nikaingia kwenye call zake, kwel nikakuta call ya mama yake wameongea kwa muda sana, nikadownload hayo maongezi, bahati mbaya yalikuwa kilugha chao na mimi sikielewi...
Nikamtumia rafiki yangu mmoja ambaye ni kabila sawa na wife hivyo akaitafsiri yale maongezi, yalikuwa hivi kiufupi

" Mama juzi nilivyoenda kulala kuna bundi alikuwa akilia hapa kwangu, na nilikemea akaondoka, ila nikapitiwa na usingizi mzito ambapo kuna ndoto ilinijia niko napigiwa ramri, na kuna sauti inaniambia wanamuita mumeo kwao kuna mambo anaenda kufanyiwa, moja ya anaemuita ni mama yake mzazi, nyumbani siyo kuzuri awe makini" mama yake akamuuliza umemwambia, wife akasema hapana, bhasi wakakubaliana wasiniambie ila waniombee tu Mungu aniepushe...

Wanajamvi, ninaomba ushauri wenu...mke hajui kama tayari ninajua alichoota, na pili kwa upande wangu siamini sana katika ushirikina, anaeweza tafsiri hiyo ndoto msaada jamani...
Mpaka sasa nimeahilisha safar zote nilizokuwa nimepanga.
 
Pole sana na hongera kwa kufahamu Hilo pls be extra careful and watch out ur in danger very danger ur nearly to be terminated. Funga na kuomba Ili MUNGU akuepushe na Hilo linalokuja sio kila mtu unayemwambia kuwa umepandishwa cheo anafurahi hata Kama ni ndugu yako wa damu anaweza kuwa adui yako namba moja. Be care my brother
 
kuna msemo unasema "miti iliyonyooka ndio hukatwa mapema porini"...acha kuwa transparent sana kwa binadamu yeyote yule,huwezi jua adui yako ni nani au anapata habari zako kutoka kwa nani..!!kuna kitu kinaitwa husda na hiki binadam hasa waafrika wengi tunacho,tunapenda ufanikiwe lakini usifanikiwe kutuzidi!!
Ukweli hili limenifundisha sana, iwe kuna ukwel au hakuna ukweli, ila haitakiwi kusema kila kitu kwa wanaokuzunguka iwe ni mafanikio au vinginevyo maana huwezi kujua mapokeo.
 
mkuu sali sana kuna husda inakunyemelea pia jitaidi sana kua msiri wa maendeleo yako coz waafrika tunaupendo wakinafiki sana wakutakiana mazur kwa maneno nakutakiana mabaya kwa vitendo...
 
Apo fasta akili lazima ufikirie mbali sawa usipokuwa makini unaenda kumpoteza mkeo anafamilia itakosa amani na hamutoelewana na mkeo
 
Tena iwe mwanzo na mwisho kutangaza maendeleo yako mzee baba utakufa na utavuruga familia yako IPO hivi

Kwa uelewawangu mama yako mzazi au jamaa zako ilipowambia kama umepandishwa sheo wanataka uendee wakakufanyie kitu ili mkeo umsahau mkeo badala yake uwakumbuke jamaa zako uwasaidie hivyo pesa utakayoipata upeleke kwenu umsahau mkeo
 
Kosa kubwa kutangaza mambo yako siku hizi hata familia ya tumbo moja hatupendani mambo yako yaishie kwako na mkewe kama wengine wanajua unafanya kazi basii inatosha kujua hivyo hivyo,hata kama unanunua vitu vya maendeleo acha kabisa kuwaambia watu iwe siri yako na mkeo
 
Mkuu pole sana kwa majanga, hapo kosa lako ni kutangaza mafanikio yako hakuna mtu anapenda kumwona mwenzie amefanikiwa usipende kudisclose mambo yako olela olela binadamu sio watu wazuri sana
 
kuna msemo unasema "miti iliyonyooka ndio hukatwa mapema porini"...acha kuwa transparent sana kwa binadamu yeyote yule,huwezi jua adui yako ni nani au anapata habari zako kutoka kwa nani..!!kuna kitu kinaitwa husda na hiki binadam hasa waafrika wengi tunacho,tunapenda ufanikiwe lakini usifanikiwe kutuzidi!!
Ni kwel kabsa,
 
Tena iwe mwanzo na mwisho kutangaza maendeleo yako mzee baba utakufa na utavuruga familia yako IPO hivi

Kwa uelewawangu mama yako mzazi au jamaa zako ilipowambia kama umepandishwa sheo wanataka uendee wakakufanyie kitu ili mkeo umsahau mkeo badala yake uwakumbuke jamaa zako uwasaidie hivyo pesa utakayoipata upeleke kwenu umsahau mkeo
Mi nilikuwa nachukulia kawaida sana, sikuwa nawaza mambo tofauti...but nimejifunza sana
 
Kosa kubwa kutangaza mambo yako siku hizi hata familia ya tumbo moja hatupendani mambo yako yaishie kwako na mkewe kama wengine wanajua unafanya kazi basii inatosha kujua hivyo hivyo,hata kama unanunua vitu vya maendeleo acha kabisa kuwaambia watu iwe siri yako na mkeo
Sure, umakini unahitajika sana,
 
Back
Top Bottom