Msaada wa mawazo na ushauri

Msaada wa mawazo na ushauri

Mwaka Wa Saba

Member
Joined
May 27, 2020
Posts
29
Reaction score
38
Niende moja kwa moja kwenye mada yangu, Mimi ni kijana umri miaka 33.

Nimefanya kazi kama Mwalimu wa Sekondari kuanzia 2012 mpaka mwaka 2019 baada ya kupata fursa ya kwenda kujiendeleza kielimu nchini Marekani kuanzia January 2020.

Katika kipindi cha miaka hiyo 7 nikiwa kama Mwalimu nimepitia mambo ambayo mwanzo sikuwahi kuamini kama ni kweli au ni mapito madogo tu. Hapa nilihisi labda cheo changu kwani hapa nilibahatika kiukweli kuaminiwa na kuwa makamu katika taasisi kubwa mno na pia kusimamamia miradi mingi ambayo ilinisaidia kusafiri nchi mbalimbali. Nilijiona mwenye bahati na sijawahi kuwa tatizo kwa niliowaongoza.

Kwanza nilipoteza uoni wa jicho langu moja, pia kupata maumivu ya mwili mara kwa mara bila kujua chanzo chake hata pale nilipoenda hospital.

Nikiwa kazini nilianza kuandamwa na ajali japo sikuona ni tatizo kubwa katika maisha. Mwisho nikapata ajali mbaya nikiwa njiani kuelekea mkoani kuichukua familia yangu, kwa mapenzi ya Mungu nilitoka salama bila jeraha ila abiria niliokuwa nimewapa msaada walipata majeraha makubwa na wakaja kuzinduka baada ya mwezi.

Hapa nilipata mstuko kwani nilipelekwa mahakamani na kwa mshangao kesi ilichukua mwaka na nusu bila kuisha kwa madai wale majeruhi wanadai fidia na hapa nafikri polisi walijawa na tamaa ya hela.

Baada ya matukio hayo nikaaza kupata mitihani mizito tena, watoto wangu nao wakaanza kupata ajali za moto, kiasi kwamba muda mwingi nikautumia kwenye kuhangaika kutibu watoto na mimi mwenyewe.

Kitu kilichonisukuma kuandika hili ni hali ninayopitia baada ya kurejea Tanzania katikati ya mwaka 2020, Kila nilipojaribu kutafuta kazi ya kufanya nilijikuta mgonjwa, nikikaa nyumbani siiumwi kitu.

Nilijaribu kuacha kuhangaika kutafuta kazi hizi zinazohitaji taaluma yangu kwa hofu ya labda husda nijikite kwenye kazi ndogo ndogo kama kilimo, ufugaji au hata uvuvi, ila baada ya watu kuniona huko yanatokea mauzauza tena na lazima nipoteze kila kitu mpaka hata hela ya kula inaisha yote na hapo utapata taarifa watoto wanaumwa.

Kibaya zaidi nimetengwa na familia yote baada ya Mimi kugoma kujiingiza kwenye mambo ya kuamini kuwa nimerogwa, naweza amini hivyo ila sijaona kuwa suluhisho ni mimi kwenda kwa waganga.

Pia wengi wanaamini nimechanganyikiwa kutaka kufanya kazi kama kilimo au biashara ndogo wakifikiria nimetoka Marekani na nimesafiri sana iweje nisifanye kazi za ofisini kama akili ipo sawa? Binafsi hilo halinisumbui na sitaki kuamini kuwa lazima niwe ofisini kabisa.

Pia katika kipindi nikiwa vizuri nilikuwa na kundi kubwa mno la marafiki ambao nilijitoa kwao mno ila hapa ninaposema hata simu hazipokelewi labda wanahisi nataka kuwaomba hela. Hali hii imeniweka katika hali ngumu mno nisijue nianze na lipi nimalize na lipi.

Najaribu mno kutoka nilipo ila naanguka tena. Kwasasa ninaomba kama kuna mtu amepitia hali hii na alitokaje katika hili ajaribu kushauri, pia msaada mkubwa ninaoomba kwenu ni kama yupo mtu atahitaji tufanye kazi nitakuwa tayari huenda itasaidia mno, binafsi mwenyewe nahisi siwezi tena kwani hata mtaji wote umeteketea kwa kuilisha familia na matibabu wakati siingizi kitu.

Pia nitakuwa tayari hata kuishi porini kufanya kazi ili tu niokoe familia yangu.

Natanguliza shukrani zangu.
 
Tiba ya kwanza ni ww kujitambua.

Tiba ya pili naamini kabisa una issues za kisaikolojia zaidi ..amini hilo .nenda kaa Dk atakusaidia. Iambie akili yako wewe sio mgonjwa..wewe sio mzembe na wewe unaweza kila unachotaka hapa dunian..yaan uwe unaoga unalala jiambie mambo positive tu
La mwisho kama unataka kutoka hapo delete namba za marafiki wako wote au block.

Badili marafiki, toka kwenye hiyo zone uliyopo utakaa hata mwaka hujaumwa!

All the best
 
Mkuu nafikiri unahitaji tiba kwanza ya kiroho. Ni wewe kuchagua upande upi unataka uhusike kwenye tiba yako. Futa yote ya nyuma then anza upya. Kama unaamini Mungu basi muamini na umkaribie sana.
 
Tiba ya kwanza ni ww kujitambua...
tiba ya pili naamini kabisa una issues za kisaikolojia zaidi ..amini hilo .nenda kaa Dk atakusaidia....iambie akili yako wewe sio mgonjwa..wewe sio mzembe..na ww unaweza kila unachotaka hapa dunian..yaan uwe unaoga unalala jiambie mambo positive tu
La mwisho kama unataka kutoka hapo delete namba za marafiki wako wote au block..
Badili marafiki ....toka kwenye hiyo zone uliyopo utakaa hata mwaka hujaumwa!.

All the best
Shukran mkuu kwa ushauri wako, haya nayapokea yote na hili la marafiki nalichukua kwa uzito mkubwa
 
Tiba ya kwanza ni ww kujitambua.

Tiba ya pili naamini kabisa una issues za kisaikolojia zaidi ..amini hilo .nenda kaa Dk atakusaidia. Iambie akili yako wewe sio mgonjwa..wewe sio mzembe na wewe unaweza kila unachotaka hapa dunian..yaan uwe unaoga unalala jiambie mambo positive tu
La mwisho kama unataka kutoka hapo delete namba za marafiki wako wote au block.

Badili marafiki, toka kwenye hiyo zone uliyopo utakaa hata mwaka hujaumwa!

All the best
Maamuzi magumu na sahihi bila shaka atazingatia
 
Kuna magap ya informations umeyaacha:
1. Ulikuwa unafundisha government ama private?
2. Kazi uliacha ama uliachishwa?
3. Marekani ulienda kwa ufadhili ama ulijipeleka kwa pesa yako.
4. Marekani ulienda kwa kozi ya muda gani?

Unforgetable
 
Kuna magap ya informations umeyaacha:
1. Ulikuwa unafundisha government ama private?
2. Kazi uliacha ama uliachishwa?
3. Marekani ulienda kwa ufadhili ama ulijipeleka kwa pesa yako.
4. Marekani ulienda kwa kozi ya muda gani?

Unforgetable
Kuna mengine nimeyaacha kweli, ila nilikuwa Private na nilipewa ruhusa ya kusafiria, pia nilienda kwa udhamini na ilikuwa ni miezi 3.
 
Hali inayokupata sio ya kawaida, japo wewe unaiona ya kawaida sababu alokutengeneza amekufunga usiwe na uelewa kwamba hiyo hali yako is abnormal.

Nachokushauri ni haya mawili:

1. Kama una imani thabiti kwenye dini yako basi nenda kawaone viongozi wako wa dini waweze kukuondolea hayo uliyobebeshwa.

2. Option ya pili ni wewe kwenda kwa wazee ulikozaliwa ili waweze kukufanyia mchakato wa kufunguliwa. Hao ndugu zako wanaokuambia umefungwa wako sahihi, wasikilize na ukubali kusaidiwa. Hapa naomba nikupe tahadhari: Waamini ndugu zako wa damu tuu.

Unforgetable
 
Ogea chumvi ya mawe kwa mwezi mmoja utakuwa poa, ama mkoa na usiage mtu anza mapambano upya kuna ndugu zako wanakuchezea
Hili usidharau mkuu, binafsi nmeprove hii ni 100%,kuna kipindi magumu yaliniandama kila aliyenijua tukikutana alikua ananielekeza kwa mganga wake japo mimi sikuwah kwenda na sitoenda mpka mauti,niliona bandiko sehemu nikaanza hiyo kuoga na chumvi ya mawe,huku naswali sana kweli Mungu alinijibu japo subra ni muhimu sana maana unaweza usione hapohapo majibu ila yapo
 
Shukran sana, Mimi ni Muslim
Ndugu yangu ufahamu kuwa suala la sisi kufikwa na Mitihani ya M'Mungu hapa Duniani ni jambo la KAWAIDA tu na la LAZIMA kwani hii ni KANUNI na UTARATIBU aliojiwekea Mwenyewe M'Mungu.
Na hili linathibitishwa na aya nyingi tu ndani ya Quran mfano, katika Quran 2:155-54 M'Mungu anasema,"Na tutakutieni katika msukosuko (MTIHANI) wa khofu na njaa na upungufu wa mali na wa watu na wa matunda. Na wapashe habari njema wale wanaosubiri.Ambao uwapatapo msiba (MTIHANI) husema,"Hakika sisi ni wa M'Mungu, na Kwake Yeye tutarejea."
Kadhalika katika suratul Mulk (67:1-2) M'Mungu anasema, "Ametukuka Yule Ambaye mkononi Mwake kuna ufalme; Naye ni Mwenye uwezo juu ya kila kitu.Ambaye ameumba MAUTI na UHAI ili kukujaribu (yaani, kukufanyieni MTIHANI) ili aone ni nani kati yenu mwenye vitendo vizuri zaidi? Naye ni Mwenye nguvu (na) Mwenye msamaha."
Lakini pia Quran 29:2-3 M'Mungu anasema, "Je,watu wanadhani wataachwa (tu hivi hivi wasitiwe misukosuko au mitihani) kwa kuwa tu wanasema tumeamini? Ndio basi wasijaribiwe? Hapana; bila shaka Tuliwatia katika taabu wale waliokuwa kabla yao,----

Mkuu!Kama ulikuwa mbali na njia za Mwenyezi Mungu,basi jisogeze na uepuke njia zisizo mpendeza na uyafanye yenye kumpendeza Mwenyezi Mungu kwa wingi.
Kama kipato chako kimeshuka sana,basi jilinganishe na walio chini yako zaidi kwa kipato na kisha mshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwa bado wewe utakuwa umewazidi wengine kwa kipato
Fanya ibada kwa dhati na usijitenge na Ayat,Surat na dua za ulinzi kila uwapo na uendako.

Endelea kufanya juhudi katika utafutaju wa ridhiki huku ukimuweka Mwenyezi Mungu mbele.

Asante.
 
Kwa hiyo baada ya kurudi ukakuta kibarua chako kimeota nyasi ama ilikuwakuwaje mpaka ukapoteza ajira yako?
Unforgetable
Nimerudi ni kipindi cha Corona na nilienda kazini kabisa baada ya hapo, ila kama umesoma vizur utaona nimesema kuwa tatizo halikuwa kwenda kazini ila kushindwa kwenda kazini kwa sababu za kuumwa na kuuguliwa pia.
Mfano nipo kazini ila performance inakuwa ndogo kwakuwa week nzima unakuwa na sababu za kuumwa kila mara kwahiyo busara inaweza kuwa kwako kuancha au kulazimisha kwenda japo unamkwaza muajiri.
 
Ndugu yangu ufahamu kuwa suala la sisi kufikwa na Mitihani ya M'Mungu hapa Duniani ni jambo la KAWAIDA tu na la LAZIMA kwani hii ni KANUNI na UTARATIBU aliojiwekea Mwenyewe M'Mungu.
Na hili linathibitishwa na aya nyingi tu ndani ya Quran mfano, katika Quran 2:155-54 M'Mungu anasema,"Na tutakutieni katika msukosuko (MTIHANI) wa khofu na njaa na upungufu wa mali na wa watu na wa matunda. Na wapashe habari njema wale wanaosubiri.Ambao uwapatapo msiba (MTIHANI) husema,"Hakika sisi ni wa M'Mungu, na Kwake Yeye tutarejea."
Kadhalika katika suratul Mulk (67:1-2) M'Mungu anasema, "Ametukuka Yule Ambaye mkononi Mwake kuna ufalme; Naye ni Mwenye uwezo juu ya kila kitu.Ambaye ameumba MAUTI na UHAI ili kukujaribu (yaani, kukufanyieni MTIHANI) ili aone ni nani kati yenu mwenye vitendo vizuri zaidi? Naye ni Mwenye nguvu (na) Mwenye msamaha."
Lakini pia Quran 29:2-3 M'Mungu anasema, "Je,watu wanadhani wataachwa (tu hivi hivi wasitiwe misukosuko au mitihani) kwa kuwa tu wanasema tumeamini? Ndio basi wasijaribiwe? Hapana; bila shaka Tuliwatia katika taabu wale waliokuwa kabla yao,----

Mkuu!Kama ulikuwa mbali na njia za Mwenyezi Mungu,basi jisogeze na uepuke njia zisizo mpendeza na uyafanye yenye kumpendeza Mwenyezi Mungu kwa wingi.
Kama kipato chako kimeshuka sana,basi jilinganishe na walio chini yako zaidi kwa kipato na kisha mshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwa bado wewe utakuwa umewazidi wengine kwa kipato
Fanya ibada kwa dhati na usijitenge na Ayat,Surat na dua za ulinzi kila uwapo na uendako.

Endelea kufanya juhudi katika utafutaju wa ridhiki huku ukimuweka Mwenyezi Mungu mbele.

Asante.
Shukran kwa ukumbusho wako, kiukweli natambua mitihani ni sehemu ya maisha yetu, kikubwa ni je nitashukuru au kukufuru? Nitasubiri au kufanya kinyume chake?
Binafsi nimejitahidi pamoja na magumu bado naamini Mungu hajanitupa kwani hata haya mengine niliyokuwa nayo kabla ya hapo wala sikumuomba ila alinipa na nilipokuwa vizur wapo watu walikuwa na mitihani mikubwa zaid yangu. Hata sehemu niliyopiga mzinga na gari ndani ya week hiyo wakiteketea madaktar wetu na naamini wengi waliacha watoto na wake zao.
Namuomba Mungu nisikufuru ila msaada wa mawazo kama haya huleta faraja na nguvu.
Shukran sana.
 
Binadamu tukubali kukutana na changamoto jaman..bila changamoto hujaishi...utachanjwa michale mwili mzima na utazidi kudorora...barabara yenyewe ina kona ...lol
 
Shukran kwa ukumbusho wako, kiukweli natambua mitihani ni sehemu ya maisha yetu, kikubwa ni je nitashukuru au kukufuru? Nitasubiri au kufanya kinyume chake?
Binafsi nimejitahidi pamoja na magumu bado naamini Mungu hajanitupa kwani hata haya mengine niliyokuwa nayo kabla ya hapo wala sikumuomba ila alinipa na nilipokuwa vizur wapo watu walikuwa na mitihani mikubwa zaid yangu. Hata sehemu niliyopiga mzinga na gari ndani ya week hiyo wakiteketea madaktar wetu na naamini wengi waliacha watoto na wake zao.
Namuomba Mungu nisikufuru ila msaada wa mawazo kama haya huleta faraja na nguvu.
Shukran sana.
Allah akusimamie ndugu, Inn Shaa Allah.
 
Back
Top Bottom