Himidini
JF-Expert Member
- May 8, 2013
- 5,534
- 4,190
Najua hapa nazungumza na mzazi mwenye akili timamu,uzoefu wa maisha na anaeijua ndoa vizuri.
..
Ukumbuke kuwa kuna wanaume ambao ni watelekezaji hata kama wanaonekana wapo ktk familia.Sifa zao kubwa ni kubebesha mimba,kulaumu,Kukagua vyungu na kuishi kwa kutuhumu.Hawapendi kuambiwa ukweli hata ungekuwa mwepesi kiasi gani wakiambiwa hasira zao huzihamishia kwa mama,rafiki zake na watoto.Nina imani huyo ndiye mume uliyenae.Nini ufanye
...
SHIRIKISHA UPANDE WA MUME
Natambua wapo ndugu wa mume ambao wanakupenda na kukujali.Washirikishe suala lako,ukikwama nenda kwa wazee.Ambao pamoja na mambo mengine wanaweza kumuwekea utaratibu wa kutoa pesa toka pato lake au atafute kazi ili achangie matunzo ya watoto.
....
UTOFAUTI WA MILA
Uzoefu unaniambia kuwa bila shaka huyo mume mnatoka kabila tofauti hivyo kosa kubwa ulilofanya ni kumjengea utegemezi kwako tu pasipo kumpa nafasi ya u-baba uliokamilika (unless yuko frustrated na jambo fulani kwa muda mrefu) Sasa kutafuta talaka hakuna msaada kama utafikiria hivyo
....
NDOA YENU INA NGUZO MOJA
Wewe ndiye nguzo,,utakapojaribu kujitenga basi watoto,mali ulizojichumia zitazua mengine usiyotegemea.La muhimu ni wewe kama nguzo kusimama imara tena ikibidi kuweka sababu za kisheria kurudisha uwajibikaji ila kutengana hata kama huna hisia nae kimapenzi (result of unspoken dissatisfaction) hakutajenga.
...
MWISHO UMOJA KATIKA FAMILIA UNA GHARAMA.
Urudishe kwa busara,upendo,utaratibu na uangalifu wa hali ya juu.
Mungu asimame upande wako Mama.
^^
..
Ukumbuke kuwa kuna wanaume ambao ni watelekezaji hata kama wanaonekana wapo ktk familia.Sifa zao kubwa ni kubebesha mimba,kulaumu,Kukagua vyungu na kuishi kwa kutuhumu.Hawapendi kuambiwa ukweli hata ungekuwa mwepesi kiasi gani wakiambiwa hasira zao huzihamishia kwa mama,rafiki zake na watoto.Nina imani huyo ndiye mume uliyenae.Nini ufanye
...
SHIRIKISHA UPANDE WA MUME
Natambua wapo ndugu wa mume ambao wanakupenda na kukujali.Washirikishe suala lako,ukikwama nenda kwa wazee.Ambao pamoja na mambo mengine wanaweza kumuwekea utaratibu wa kutoa pesa toka pato lake au atafute kazi ili achangie matunzo ya watoto.
....
UTOFAUTI WA MILA
Uzoefu unaniambia kuwa bila shaka huyo mume mnatoka kabila tofauti hivyo kosa kubwa ulilofanya ni kumjengea utegemezi kwako tu pasipo kumpa nafasi ya u-baba uliokamilika (unless yuko frustrated na jambo fulani kwa muda mrefu) Sasa kutafuta talaka hakuna msaada kama utafikiria hivyo
....
NDOA YENU INA NGUZO MOJA
Wewe ndiye nguzo,,utakapojaribu kujitenga basi watoto,mali ulizojichumia zitazua mengine usiyotegemea.La muhimu ni wewe kama nguzo kusimama imara tena ikibidi kuweka sababu za kisheria kurudisha uwajibikaji ila kutengana hata kama huna hisia nae kimapenzi (result of unspoken dissatisfaction) hakutajenga.
...
MWISHO UMOJA KATIKA FAMILIA UNA GHARAMA.
Urudishe kwa busara,upendo,utaratibu na uangalifu wa hali ya juu.
Mungu asimame upande wako Mama.
^^