Msaada wa mawazo na ushauri, please only serious people here

Msaada wa mawazo na ushauri, please only serious people here

kokuemage

Member
Joined
Jan 24, 2013
Posts
34
Reaction score
4
Mimi ni mwanamke nina miaka 37 sasa hivi,nimeolewa na nina watoto watatu miaka 17,13 & 6yrs.Nimeishi na mume wangu kwa miaka 18 sasa hivi,mume wangu ni maasai wa mjini sio wale wavaa lubega.

Tatizo ni huyu baba nimembeba sana mpaka naona nimechoka na vile umri umeenda sijui nifanyeje. Sio mwanaume muwajibikaji kabisa.

Hajui ada za wattoo zinatoka wapi, chakula, maendeleo ndani ya nyumba, hajui chochote yeye ni kama mtallii.Hata akiona pazia liko upande hatengenezi au chumba hakina bulb hajigusi, ni mimi ndio nifanye.

Ada za watoto ndio kabisa akijatahidi sana kama ada ni laki 4 basi atatoa laki 2 tena kwa shida na kwa awamu. Akikuta hela zako au pochi umeweka vibaya anaruka mpaka na hela zako.

Sio muwajibakaji hata tone yeye ni starehe na starehe na yeye.

Kweli nimevumilia sana tokea mwanzo ila mbona naona kama siwezi tena? mzigo umenilemea na hana msaada wewe ndio ukimbizane watoto watakula nini, watasomaje, watavaa nini, nyumba inaitaji nini etc.

Ndoa ni kwa shida na raha,nimejenga nyumba mwenywe na kila kitu nimefanya mwenywe tena yeye ulikuwa ukimpa hela ndio anaenda kulewa, mpaka leo ana miaka 43 sasa hivi ni wa kurudi usiku wa manane.

Nimechoka kuvumilia jamani namuambia aondoke aniache maana nyumba ni ya watoto na ni nguvu yangu, mwenywe hataki.

Ukipika chakula akikuta anakula hajui hata kinatoka wapi.

Juhudi zote za maendeleo na watoto ni mimi mwenywe.

Haya maisha yamenichosha sana jamani nifanyeje nimejikuta simpendi tena kabisa na sina hamu nae kabisa hata ya mapenzi.

Sina mpenzi wa nje basi tu nimeona huu ni mzigo ambao umefika mwisho,nataka nimuche nafanyaje na yeye ndio amekataa kutoka ndani ya nyumba kabisa? nimechoka kweli kwei.

Toka kanioa ni ile miezi ya awali ndio alishawahi nitoa out,sikumbuki hata mara ya lmwisho aliniambia mke wangu twende out ni lini, au tukakaa kupanga maisha/maendeleo ya watoto au chochote ni lini.

Mimi ndio wa kukimbizana na maendeleo ya shule ya watoto. Kila siku ni kuomba kulipa ada kwa instalment.

Nimekua ndio kama niko peke yangu yeye akija usiku na mtungi wake ni kelele na kulala.

Yuko kama vile anaishi guest,akija usiku saa zingine fujo na kelele. Sikumbuki hata mara ya mwisho ameshawahi nipa laki ya matumizi au hata elfu 50 ni lini? akitoa hela ya chakula ni elfu 20 kama mara ya mwisho kanipa miezi 2 iliyopita.

Hata nikiwa na msiba kwetu hakanyagi wala haudhurii.

Jamani hebu nishaurini nifanyeje?
 
Nenda tafuta wakili na umpe talaka. Ukishampa talaka na kila kitu kikiwa kimekaa kisheria unaweza kumtoa humo ndani kwa nguvu
 
pole sana.............................hapo suluhisho ni talaka tu kwani hakuna tiba nyingine hapo kama ingetakiwa tiba ni pale mwanzoni kabisa mwa mahusiano yenu ila kwa sasa its toooo late just divorce him.
 
Mmm pole shosti,kwa ufupi mzigo umeshaanza kukushinda,baada ya miaka 18 ya uvumilivu,hongera sana una moyo na zidisha uvumilivu, ivi tangu mwanzo kwa nini ulimzowesha hiyo tabia mpaka amebobea nayo?
 
Aisee, ndoa ndoano.
Unaonaje kwenye akili ukamuona naye kama mmoja wa watoto? Akiondoka ndio utapata msaada wa kusomesha watoto?

Jana niliona ushuhuda wa mmama mmoja ambaye yeye ndio alikuwa mlevi wa kutupa na sigara kwa sana alikuwa anaspend more than $10,000 kwa week lakini mumewe alimvumilia na mpaka alivyofanyiwa deliverance.
 
Pole sana, sitaki kukushauri uvunje ndoa yako
 
You don't like the things he does, but you have made it easy for him to do this for 18 years.

It seems wewe unachohitaji ni DIVORCE basi sema tu na huyo mwanaume kang'ang;ania tu humo ndani
 
Ushauri mzuri sana.
salama Kigoma lakini!
Aisee, ndoa ndoano.
Unaonaje kwenye akili ukamuona naye kama mmoja wa watoto? Akiondoka ndio utapata msaada wa kusomesha watoto?

Jana niliona ushuhuda wa mmama mmoja ambaye yeye ndio alikuwa mlevi wa kutupa na sigara kwa sana alikuwa anaspend more than $10,000 kwa week lakini mumewe alimvumilia na mpaka alivyofanyiwa deliverance.
 
Huyo ana pepo, mlete kwangu nikamwombee abadilike.
 
Spiritual wife, spirit f lust @ work
Bila kuwa delivered hapo nothing u can do!!!

Chagua kumpeleka akafanyiwe deliverence unless hizo roho zitahakikisha mnaachana maana ndo kazi yake.

Na ww unavumiliaje mda wote huo? !!
 
mimi ni mwanamke nina miaka 37 sasa hv. nimeolewa na nina watoto watatu. miaka 17,13 & 6yrs. nimeishi na mume wangu kwa miaka 18 sasa hivi. mume wangu ni maasai wa mjini sio wale wavaa lubega.
tatizo ni huyu baba nimembeba sana mpaka naona nimechoka na vile umri umeenda sijui nifanyeje. sio mwanaume muwajibikaji kabisa. hajui ada za waotto zinatoka wapi, chakula, maendeleo ndani ya nyumba, hajui chochote yeye ni kama mtallii. hata akiona pazia liko upande hatengenezi au chumba hakina bulb hajigusi. ni ww ndio ufanye. ada za waotto ndio kabisa akijatahidi sana kama ada ni laki 4 bac atatoa laki 2 tena kwa shida na kwa awamu. akikuta hela zako au pochi umeweka vibaya anaruka mpaka na hela zako. sio muwajibakaji hata tone yeye ni starehe na starehe na yeye. ni kwlei nimevumilia sana tokea mwanzo ila mbona naona kama siwezi tena? mzigo umenilemea na hana msaada wewe ndio ukimbizane waotto watakula nini, watasomaje, watavaa nini, nyumba inaitaji nini etc. ndoa ni kwa shida na raha. nimejenga nyumba mwenywe na kila kitu nimefanya mwenywe tena yeye ulikuwa ukimpa hela ndio anaenda kulewa, mpaka leo ana miaka 43 sasa hivi ni wa kurudi usiku wa manane. nimechoka kuvumilia jamani namuambia aondoke aniache maana nyumba ni ya watoto na ni nguvu yangu mwenywe hataki. ukipika chakula akikuta anakula hajui hata kinatoka wapi. juhudi zote za maendeleo na watoto ni mimi mwenywe. haya maisha yamenichosha sana jamani nifanyeje nimejikuta simpendi tena kabisa na sina hamu nae kabisa hata ya mapenzi. sina mpenzi wa nje bac tu nimeona huu ni mzigo ambao umefika mwisho. nataka nimuche nafanyaje na yeye ndio amekataa kutoka ndani ya nyumba kabisa? nimechoka kweli kwlei. toka kanioa ni ile miezi ya awali ndio alishawahi nitoa out. sikubmuki hata mara ya mwisho aliniambia mke wangu twende out ni lini, au tukaka kupanga maisha/maendeleo ya watoto au chochote ni lini. mimi ndio wakukimbizana na maendeleo ya shule ya watoto. kila siku nikuomba kulipa ada kwa instalment. nimekua ndio kama niko peke yangu yeye akija usiku na mtungi wake ni kelele na kulala. yuko kama vile anaishi guest. akija usiku saa zingine fujo na kelele. sikumbuki hata mara ya mwisho ameshawahi nipa laki ya matumizi au hata elfu 50 ni lini? akitoa hela ya chakula ni elfu 20 kama mara ya mwisho kanipa miezi 2 iliyopita. jamani hebu nishaurini nifanyeje?????? hata nikiwa na msiba kwetu hakanyagi wala haudhurii.

Wewe ni kabila gani mumiiii .................... nahisi nakufahamu vile!
 
Mmmmmmmmmmmh! Ngoja nitulie kwanza! UMUHIMU WA MTU UNAONEKANA AKIWA HAYUPO!

Mimi navoona ni kuwa huyo baba anakupenda bado ila kuna communication break down ambayo hamkuishughulikia mda mrefu sasa imefikia explosion stage. Na mwenzio inawezekana hafurahii hio hali ilivo ila wewe ushafunga mageti yoteee maelewana and since moyoni umeshaamua yule hatma yake ni disposal tu, basi haumpi mwenzio mwanya wa kujirudi.

Trust me unaweza kuwa hujajigundua but kama mtu kakutoka rohoni itakuwa una mtreat very harsh! Maybe na wewe Mungu kakubariki kakipato kadogo basi ndo kumkalia mwenzio kichwani moja kwa zote! Unamuona mzigo. Sasa nae kachoka kaona hata akijitutumua you dont appreciate at all, ndo maana kasusa hafanyi kitu.

And the only reason anakaa myabe he keeps HOPING things might change, na anajua akiondoka ITS REALLY OVER!!!!!! Ndo maana yote unamfanyia he still wants to spend the rest of his life with you and the kids. Give your marriage another chance. Usitumie force kumbadilisha. Tumia motivation na negotiations kujua why he turned that way! Lazima kuna kitu.

Trust me SINGLE LIFE kwa mtu alieenda age kama wewe dada yangu sio rahisi. Plus ni mfano gani unawapa wanao esp kama wa kike unao. You kicked their father out!!!!!!!!!!!!! Pleaseeeeeeeee! Kuna watu wajane they wish watu wao wangekuepo japo hata kama zigo kama mumeo! Usitafute kuzeeka mwenyewe! Kuna wamama single wanaenda kununua vijana. Au hata ukimtimua ukadandia mume wa mtu anaeibaiba do you think you will be happier!

I dont know, ut for me since uchumi unaweza kuumudu THINK BEYOND ECONOMICS! Kama usipokuwepo watoto itakuaje? Ukiugua ghafla, na mambo kama hayo! Hata wenzio hali mbaya. Ukiona kwako kwaungua, kwetu kwateketea atiiii!!!!!!!!!!! Sema tu tunaangalia mbali!
 
Kabla ya kuleta malalamiko hapa JF. Umeshawahi peleka malalamiko kwa walezi wenu wa ndoa au hata kanisani? Anzia kwny ngazi ya familia na washenga. Ikishindikana tafuta msaada wa kisheria. Pole sana kwa changamoto
 
Kimsingi; this husband is completely discouraging! ila najiuliza je yupo hivyo kwa kupenda ama ni product ya malezi au mazingira aliyokulia au anayoishi!? Any answer may create a good solution to this problem!

Maneno yangu:
Mvumilie mumeo wakati wa shida na raha, magonjwa na afya ndivyo kiapo cha kanisani kinavyosema; and i guess Mungu alijua safari ya ndoa in ups and downs, ndo maana kaweka hichi kiapo! Mheshimu Mungu!

USITENGANE NA MUMEO NO MATTER WHAT, kila jaribu is under your abilities! Keep praying day and night!

Pole sana!
 
Missing you Dada.

Mujini ya Kapuya ndio yameshika kasi baada ya yale ya mwenyeji wako Zitto vs Waraka wa siri. Naamini unajua pia Division Five imerudi Zero. Bado mradi wetu wa mabasi unaendelea vzr. Hayo machache tu.

Kigoma shwari bwana, habari za mujini?
 
Back
Top Bottom