Msaada wa kuagiza simu ebay/amazon,

ligolyser

Senior Member
Joined
May 9, 2013
Posts
155
Reaction score
15
habar ndugu zangu,nataka kuagiza simu ktk web tajwa apo juu,mimi nipo bukoba na nilijarbu kupitia ktk sehemu izo nikakuta simuu bei nafuu sana mfano samsung galaxy note2 usd$210 sasa sijui hadi kunifikia inaweza gharimu kias gani,.pia sina uelewa wowote wa kuagiza simu kutoka nchi za nje sijui naanzia wapi na naishia wapi na bank natakiwa kutumia ipi?? Mimi acount yangu ni crdb master card je inafaa?? Na vp proces za kuwasiliana na hao wauzaji mpaka kutuma pesa na wao kunitumia simu? Je nikituma pesa wasipo nijibu/ kunitumia simu natakiwa kufuata taratibu zipi ili kurudishiwa pesa zangu?? Nawakilisha kwenu na kwa anaeelewa anijuze apa ili iwe faida na kwa wengine ambao hawajui
 
Mkuu kama una mastercard ni vyema inawezekana. Create a paypal account kisha hiyo paypal account ndo itakuwezesha kufanya transaction kwa ebay. Uzuri wa ebay ni kwamba iko safe. Hauibiwi na ukilipia wanahakikisha mzigo unakufikia hadi address uliyowapa, in case isipofika watawasiliana na wewe na wakijiridhisha seller hakukutumia mzigo wanakutumia mwingine (ule ule ulioagiza).
Usihofu. Kingine ni kuwa, unaweza kuona product price iko chini ukashangaa bei inakuwa kubwa depending na shipping uliyochagua. The faster the more money, the delayed means the lesser the amount charged.
Wadau wengine watakuja kukuelekeza hapa mda si mrefu. iyokopokomayoko, njunwa wamavoko, munjy1, mangoro njooni mtoe msaada hapa kwa mdau
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…