Utapeli Uagizaji wa Bidhaa Kutoka Nje ya Nchi

Rais Wa Malofa

JF-Expert Member
Aug 27, 2015
681
773
Wana Jamii Forums Salaam. Natumai kila mtu ameshakifuta vumbi kichinjio chake tayari kwa ajili ya kesho.

Nimekuwa nikiona matangazo mbalimbali ya watu kuagiza Bidhaa mbalimbali toka nje ya nchi. Kiukweli yale matangazo yamekuwa yakivuta attention ya watu na wengine wamekuwa wakijitosa na kuagiza bidhaa nje ya nchi mimi nikiwa mmoja wapo.

Kuna waagizaji ambao ni maarufu na wengine ambao sio maarufu. Mimi niliwahi kufanya biashara na bwana mmoja maarufu saana humu ndani ambaye anaagiza bidhaa toka nje ya nchi na mara nyingi ukitaka kuagiza bidhaa kutoka Ebay au Amazon huwa ana recommend akuagizie kupitia Ali Express.

Mwaka jana nilikuwa na shida. Kutokana na reputation ya yule bwana nikaamua kufanya nae mawasiliano na kumuomba aniagizie samsung S9+ kwa kuamini kwamba yeye ni mzoefu na hawezi fanya utapeli wa aina yoyote.

Nilimpatia link ya simu niliyokuwa naitaka toka ebay ila akanishauri aniagizie toka Aliexpress. Nilimkubalia kwa sababu nilitokea kumwamin saana kupitia post zake humu ndani. Baada ya kumpa jina la simu na rangi niliyotaka

Sikujihangaisha tena na kila kitu nilimwachia amalize yeye. Gharama ya simu mpaka kunifikia mkononi ilikuwa milioni moja na laki mbili na elfu arobaini. Nililipa pesa zote bila baki kupitia Tigo pesa.

Baada ya miezi miwili ya kusubiri nilipokea mzigo wangu wa simu ukiwa umefungwa vizuri. Ilikuwa ni samsung s9 plus kwa nje. Kwa kuwa ilikuwa ni mpya nilitegemea high performance lakini cha ajabu ile simu ilianza kupata joto kubwa kwa nyuma na ilikuwa inaishiwa chaji baada ya masaa manne au matano regardless matumizi. Nilijaribu kuwasiliana na jamaa yangu mmoja ambae pia alikuwa anatumia simu kama ile kutaka kujua huenda ni tatizo la simu kwa ujumla lakini jamaa aliniambia simu yake ilikuwa haipati joto na akichaji asubuhi inadumu na chaji mpaka jioni.

Nilijaribu kugoogle maneno yaliyoko nyuma ya simu ambayo huwa yanaonyesha model pamoja na manufacturer wa simu. Nilikuja kugundua ile simu ilikuwa ni clone/fake na ilitakiwa kuuzwa angalau laki 4 au 3. Niliumia saana lakini sikuwa na cha kufanya.

Jamaa aliyenifanyia hivi ni maarufu saaaana humu ndani kwenye haya mambo ya uagizaji wa bidhaa toka nje ya nchi ila Kesho tukapige kura tu.
 
Watu sijui tunapata uzito gani kuagiza sisi wenyewe nje ya nchi
Ni simple ila tunaona kama ni vigumu sna
Aya ndio madhara yake

Usimuamini sna mtu asa aya Mambo ya pesa utapigwa tu

Taka usitake
 
Unaweza ukawa unamlaumu bure, kumbuka yeye anaagiza nje so walioituma ndo walifanya huo uhuni, hii ndo risk ya kuagiza kitumtandaoni tegemea kupata kitu ambacho hukutegemea.
 
Ukweli mchungu ni huu hapa.
Kununua simu aliexpress za topbrands kama LG, iphones, Sony, Samsung, Googlepxl, na nyinginezo ukiambiwa ni brand new ni umedanganywa hizo ni refurbs (zile simu ambazo zilikua na shida zikatengenezwa wanaziweka macover mapya zionekane mpya ila in reality sio mpya, na wanafanya repackaging kabisa na box lake ukiifungua unasema 0 mileage.

Simu ambazo unaweza kuzipata. Mpya yaani brand new kutoka mitandao ya kichina kama aliexpress, alibaba, na mingineto ni hizi hapa

1. XIAOMI
2. HUAWEI
3. LENOVO
4. ZTE
5. NOKIA
Na nyenginezo brand kubwa kubwa za kichina.

Kwa hiyo ndugu zangu mnaonunua hizo s9 sijui s10 na iphones kariakoo na makumbusho na maduka mengi nchini kwa kuambiwa ni mpya ni mnadanganyika na kurubuniwa, ila si mnapenda bei rahisi huko ndio penyewe.

Mfano Ukitaka Samsung mpya hizi flagship kwa hapa TZ utapata kwenye maduka ya mitandao ya simu, dealership stores na baadhi ya maduka makubwa ila bei zake lazima ushtuke kidogo ukija kulinganisha na zile za wachinku.
 
Pole Kwa yaliyokukuta Ila AliExpress ule mtandao unaongoza Kwa kuuza vitu vya hovyo sana na kama unapenda cheap ndiyo utabinunua Hadi basi Ila huyo mfanya biashara kwanini akutajie mtandao unaouza vitu vibaya bora Amazon ingawaje kule napo unatakiwa uwe Makini mana wapigaji wengi
 
Pole Kwa yaliyokukuta Ila AliExpress ule mtandao unaongoza Kwa kuuza vitu vya hovyo sana na kama unapenda cheap ndiyo utabinunua Hadi basi Ila huyo mfanya biashara kwanini akutajie mtandao unaouza vitu vibaya bora Amazon ingawaje kule napo unatakiwa uwe Makini mana wapigaji wengi
Ila wengine tunaagiza vitu na tunapata vya og kabsa wala hamna utapeli.

Kwa ishu mfano za simu, unaeza ingia website ya hiyo simu hlf ukaagiza. Hapo ni kama kule Aliexpress umepaogopa.

Ila simu watu tunaagiza Aliexpress na tunaletewa vilevile bila uhuni, zipo reviews pale unaeza soma zote na simu ukikuta inashida kuna utaratibu wake kabla muuzaji hajapewa chake.
 
Wana Jamii Forums Salaam. Natumai kila mtu ameshakifuta vumbi kichinjio chake tayari kwa ajili ya kesho.

Nimekuwa nikiona matangazo mbalimbali ya watu kuagiza Bidhaa mbalimbali toka nje ya nchi. Kiukweli yale matangazo yamekuwa yakivuta attention ya watu na wengine wamekuwa wakijitosa na kuagiza bidhaa nje ya nchi mimi nikiwa mmoja wapo.

Kuna waagizaji ambao ni maarufu na wengine ambao sio maarufu. Mimi niliwahi kufanya biashara na bwana mmoja maarufu saana humu ndani ambaye anaagiza bidhaa toka nje ya nchi na mara nyingi ukitaka kuagiza bidhaa kutoka Ebay au Amazon huwa ana recommend akuagizie kupitia Ali Express.

Mwaka jana nilikuwa na shida. Kutokana na reputation ya yule bwana nikaamua kufanya nae mawasiliano na kumuomba aniagizie samsung S9+ kwa kuamini kwamba yeye ni mzoefu na hawezi fanya utapeli wa aina yoyote.

Nilimpatia link ya simu niliyokuwa naitaka toka ebay ila akanishauri aniagizie toka Aliexpress. Nilimkubalia kwa sababu nilitokea kumwamin saana kupitia post zake humu ndani. Baada ya kumpa jina la simu na rangi niliyotaka
Sikujihangaisha tena na kila kitu nilimwachia amalize yeye. Gharama ya simu mpaka kunifikia mkononi ilikuwa milioni moja na laki mbili na elfu arobaini. Nililipa pesa zote bila baki kupitia Tigo pesa.

Baada ya miezi mwiwili ya kusubiri nilipokea mzigo wangu wa simu ukiwa umefungwa vizuri. Ilikuwa ni samsung s9 plus kwa nje. Kwa kuwa ilikuwa ni mpya nilitegemea high performance lakini cha ajabu ile simu ilianza kupata joto kubwa kwa nyuma na ilikuwa inaishiwa chaji baada ya masaa manne au matano regardless matumizi. Nilijaribu kuwasiliana na jamaa yangu mmoja ambae pia alikuwa anatumia simu kama ile kutaka kujua huenda ni tatizo la simu kwa ujumla lakini jamaa aliniambia simu yake ilikuwa haipati joto na akichaji asubuhi inadumu na chaji mpaka jioni.

Nilijaribu kugoogle maneno yaliyoko nyuma ya simu ambayo huwa yanaonyesha model pamoja na manufacturer wa simu. Nilikuja kugundua ile simu ilikuwa ni clone/fake na ilitakiwa kuuzwa angalau laki 4 au 3. Niliumia saana lakini sikuwa na cha kufanya.

Jamaa aliyenifanyia hivi ni maarufu saaaana humu ndani kwenye haya mambo ya uagizaji wa bidhaa toka nje ya nchi ila Kesho tukapige kura tu.
majina tunayojipa yanasadifu matendo yetu.....pole sana Rais wa malofa.
uzi auoneMwl.RCT
 
Ukweli mchungu ni huu hapa.
Kununua simu aliexpress za topbrands kama LG, iphones, Sony, Samsung, Googlepxl, na nyinginezo ukiambiwa ni brand new ni umedanganywa hizo ni refurbs (zile simu ambazo zilikua na shida zikatengenezwa wanaziweka macover mapya zionekane mpya ila in reality sio mpya, na wanafanya repackaging kabisa na box lake ukiifungua unasema 0 mileage.

Simu ambazo unaweza kuzipata. Mpya yaani brand new kutoka mitandao ya kichina kama aliexpress, alibaba, na mingineto ni hizi hapa

1. XIAOMI
2. HUAWEI
3. LENOVO
4. ZTE
5. NOKIA
Na nyenginezo brand kubwa kubwa za kichina.

Kwa hiyo ndugu zangu mnaonunua hizo s9 sijui s10 na iphones kariakoo na makumbusho na maduka mengi nchini kwa kuambiwa ni mpya ni mnadanganyika na kurubuniwa, ila si mnapenda bei rahisi huko ndio penyewe.

Mfano Ukitaka Samsung mpya hizi flagship kwa hapa TZ utapata kwenye maduka ya mitandao ya simu, dealership stores na baadhi ya maduka makubwa ila bei zake lazima ushtuke kidogo ukija kulinganisha na zile za wachinku.
Ndio maana mm nikitaka simu naenda Sore Agent bei inachangamka ila kitu OG ,unakuta Headset ya Samsung ni 35k dukani kwao, mtaani 3.5I hy tofauti ndio kielelezo cha quality
 
Kuna bidhaa zingn hukuti huku...mfano viatu, mi naagiza nje na nakua niko unique, bongo kiatu wanauza ghali na hakina kiwango.

Na pia ni umakini hauko, mbn tunaagiza tunaletewa vilevile
Kwa wewe sawa sasa mtu anaagiza kitu nje akati bongo vipo mfano huyu ndugu yetu anaagiza s9 plus nje ya nini sasa wakati zipo kibao kkoo?
 
Kwa wewe sawa sasa mtu anaagiza kitu nje akati bongo vipo mfano huyu ndugu yetu anaagiza s9 plus nje ya nini sasa wakati zipo kibao kkoo?
Dhana ya upigaji tena kariakoo hlf pia ile kujua kwenye duka lao ni ghali sana.

Simu za Apple na samsung kuzipata Og tena mtandaoni ni kitu kigumu. Labda mtu aagize kupitia official website ya hiyo simu.

Simu zingine unapata vizuri tu kama oppo, oneplus, huawei, motorola, nk
 
Back
Top Bottom