Msaada wa haraka wakuu

exalioth

JF-Expert Member
Joined
Jun 22, 2016
Posts
2,391
Reaction score
4,145
Nsaidien mkewangu ananitesa kimawazo

Kifupi iko hivi kipindi namuoa sku yapili yupo nyumbani nliokota kwenye kimkoba mamba yacm skutaka kumuuliza niliikopi ile mamba nkawanayo tumekaa miaka mi4tunamtoto1

Kilichoniumiza nimekuja kugundua anamawasliano na ile namba maana nmekua mtulivu skunyngi nkaona baadh ya sms kbaya zaidi nliona sms ya muamala aliotuma hela wife kwa hiyo namba nmeipigia kwa namba ngeni nmwanaume anantesa kwakwel naumia nashindwa ata kusema

Mawazo yenu ndo msaada

Imeandikwa
Exalioth
App ya jamiiforms
 
Mkuu pole sana, huyo sio riziki kwako kajikinga mvua inawezekana hata mtoto sio wako, toka umemuoa alikuja na namba ya simu
 
DU POLE Mwanaume mwenzangu aisee. Hebu ngoja wajuzi waje ili tujue jinsi ya kufanya. LEO KWA MWENZIO KESHO KWAKO
 
Sasa si ukae nae chini umuulize hiyo namba ni ya nani
 
Umeshamuuliza wife wako kuhusu hilo?
Amekujibuje?

Mwambie; "uliapa kuwa nami kwenye shida na raha maisha yako yote, kifo ndicho kitutenganishe; sasa naona unashindwa kutekeleza kauli yako. Chunga tusitenganishwe na gunia 2 za mkaa au mapanga na visu."

Akiendelea , siku ukifumania evidences piga chini tu.

Ila tatizo la ndoa za sasa hawaachani kiroho safi kabisa, hilo halipo! Ni kuua, kuuana au mmoja kujinyonga. Sijui mdudu gani kaingia mapenzini!?
 
Mkuu pole sana, huyo sio riziki kwako kajikinga mvua inawezekana hata mtoto sio wako, toka umemuoa alikuja na namba ya simu
Hata mimi hilo limenisikitisha sana.

Afanye maamuzi mapema.
 
Unagongwa shtuka wewe shaur yako
Mpige chini ni shetani huyoo
 
Kwa nini ulioa mke wa mtu? Ndio shida ya kuoa mwanamke aliyeanzishwa mapenzi na wengine, kwako kaja kwa sababu tu yule anayempa akitakacho hakuwa tayari kumuoa. Kifupi huyo si wako, wewe ni mhifadhi tu
 
kwanini unateseka.. muulize ujue ukweli,,,,halafu wewe bwege kweli miaka minne unambebea wife namba......endelea kumfuatilia uumie zaidi..
 
Bado mkiambiwa muoe Bikra mnajitoa akili. Mnahaki ya kufanyiwa ujinga.

Sijui kwa nini sieleweki pamoja na upuuzi mnaofanyiwa.
 
Ongea na mke wako tafuta best way kuapproch hayo maongezi
 
Endeleeni na maisha, hilo katika ndoa haliepukiki. Hata wewe kuna namba ambazo anazitilia shaka lakini ametulia tu.

Kikubwa kaa nae na uongee nae, hiyo namba hata ungechana kikaratas ipo kichwani.

#mwanamke hachungwi
 
Mtumie muamala kama buku 20 hivi kwenye namba ngeni halafu mwamabie wewe ni mgeni dar umepewa namba kwamba yeye anaweza kukusaidia wewe unatafuta gari la kununua, mkutane sehemu muongee kama itawezekana usimlazimishe jifanye huna umuhimu nae sana, akiingia kingi mvute sehemu ukiwa na Rafiki yako wa karibu mumbane aseme ukweli tu na mumueleze wazi kwamba hamna nia ya kumdhuru sababu nyote ni wanaume. Kutokea hapo akiongea ukweli kama anakula vitu yako rudi nyumbani piga chini mke kwa haraka. Nasisitiza usipige wala kujeruhi yoyote, iwe ni kwa amani kabisa. Rudi nyuma fungua ukarasa mpya ukiwa na Amani tele rohoni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…