Msaada: Ugonjwa wa Mdudu wa kidole

Msaada: Ugonjwa wa Mdudu wa kidole

Dupe

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2013
Posts
1,668
Reaction score
813
Habari zenu wanajamvi,

Naomba msaada wa kuujua ugonjwa wa mdudu wa kidole kiundani zaidi, Napenda nijue chanzo chake, matibabu yake na njia za kuepuka ugonjwa huu……!

Shukrani.
 
Loweka kidole kwenye mafuta ya taa kila siku mpaka kitakapokusanya usaa then ukamue endelea kutumia mafuta ya taa mpaka kitapona.

Thanks
 
Chukua kiwembe alaf chanja lile eneo lenye uvimbe kidogo dam itatoka then chovya kidole kwenye maji ya betri ya gar mara moja tu alafu toa hapo umepona.

Kitakauka chenyewe hamna hata kukamua usaha, huwez amini lakin nilishauriwa hivyo nikafuata ilichukua siku mbil tu kidole kimepona.
 
Usichovye kwenye lile eneo ulilochanja tu yan kucha yote na sehem ya juu kidogo ya kucha ipate maj hayo ya betri utahis maumiv pale ulipojichanja ila patatulia na usikioshe mpaka kikauke chenyewe kabsa haichukui masaa matano we acha tu dam igandie pale cha muhim n maj ya betri kumchoma mdudu
 
Kuna matunda fulani yana rangi ya njano.. waga yanota sehem yoyote.. mimi nayafaham kwa jina la.matulatula.. waga yaananza kuwa rangi ya kijan halaf yanaiva na kuwa rangi ya njano ndani kuna vimbegu vingi vidogo vidogo.

Chukua hilo tunda likiwa la njano litoboe kidindu halafu livishe kwenye kidole kilicho na mdudu kwa mda wa siku mbili au tatu... dawa nyingine chukua majani ya nna yaponde then yazungushie kwenye kidole chenye mdudu.

usikitoboe, kama unekitoboa usiweke vitunguu swaumu. Pole sana najua kidole hapo kinauma mpaka unachanganyikiwa, nilishawah kuumwa I know the pain.
 
@majorfaddy,
Haya matunda uliomuelekeza yanaitwa ndulele yanafanana na ngogwe.
 
Wasukuma huwa wanatumia ndula kubwa zilizo komaa kutibu tatizo hilo kwa kuitoboa na kuivisha kwenye kidole chenye tatizo!
 
Nawashukuru wote nitafanyia kazi
 
hii huwa ni abscess ambayo hujitokeza sehemu yoyote ile.

hili tatizo huweza pia kutokea kwenye unyayo etc hivyo huhitaji kufanyiwa incision and drainage kama majipu mengine.

kule kwetu huwa wanaita khevola idawa anamaelezo mazuri ila ni jipu tu kama majipu mengine.
 
Last edited by a moderator:
Nyie mnaosema utumie ant biotic yyte utapona mmewahi kuugua huo ugonjwa au mnaiskia tu,huu igonjwa ni hatari sana zaidi ya mnavodhani, watu wanalemaa na kupoteza uhai sababu ya ugonjqa huu,ni sumbufu kweli ugonjwa huu na wengi wapona kwa dawa za jadi napo unatakiwa uuwahi sana.

kuna rafiki yangu nusura alemae ulimchimba mkono balaa katibiwa miezi mitatu hospitali,dawa zote mlotaja hapo juu hutumika ila lazimabuuwahi sana,na pia wengine hufunga kifuko cha chumvi kwa muda mrefu,ukichelewa ni balaa kubwa sana unaoza mkuu.
 
Huu ugonjwa uliwahi nipata majoriffydady uko sahihi hayo matunda kijijini kwetu yanaitwa ndulele yako kama nyanya chungu huwa yanaota porini unachukua liiloiva vizuri.

Unalikata juu na chini muundo wa pete kisha unavaa kidoleni mwisho kabisa mm niliva saa nne asubuhi nikalala nalo hadi kesho yake asubuhi uvimbe kwisha na maumivu kwisha. Kijini yalikuwepo ila mjini sijauona huo mti.
 
Ukipata hilo tunda ni dawa rahic sana na unapona bila matatizo. Huo ugonjwa unaum mnoo hasa wakati unaanza unahic kama mapigo ya yamehamia kwenye kidole
 
pole sana lakini njia nyingne ukiona dalili za mdudu kidoleni tafuta majani ya mchongoma( hina ya majani) yatafunee harafu kamua kudiwe na majimaji bandika kwenye mdudu japo utapa maumiv ila mdudu atatok mwenyew bila kusubir usaha
 
Back
Top Bottom