MSAADA: Ubora ya gari aina ya 'Suzuki Swift'

Concrete

JF-Expert Member
Mar 12, 2011
3,605
549
Nimepata kusikia kuwa gari aina ya Suzuki Swift ni gari nzuri sana kwa mtanzania wa ngazi ya kati(Middle Class) kwa matumizi binafsi katika mazingira ya mijini Kwa vigezo vya BEI NAFUU, MAFUTA KIDOGO, UIMARA, VIPURI VINAPATIKANA nk.

Wataalam wa mambo humu JF ninaomba maoni na ushauri wenu kabla ya kufanya maamuzi ya kununua, hususani ninataka kujui bei yake, utumiaji wake wa mafuta, ubora na udhaifu wake, aina ya gari mbadala wake nk.
 
nkuu nakushauri chukua Honda Fit. Ni gari dogo kama swift ila ina nafasi kubwa zaidi ndani na unaweza kupakia mzigo mkubwa sana kwa size ya gari. zile configurations za viti zinakupa uwezo mkubwa wa matumizi yake. kumbuka gari ina kazi sio kukutoa sehemu moja kwenda nyingine pekee. mafuta mimi Napata mpaka 16km kwa lita moja kwa safari za mjini na foleni. Niliwahi kwenda nacho morogoro na kurudi. nilitumia lita 18.5 kwa kutembea km 398 (kutokea bilicanas kwenda mitaa ya jamhuri stadium na kurudi tena mitaa ya bilicanas!) Honda Fit zimeanza kuenea mjini kwa hiyo spea sasa zinapatikana kwa urahisi zaidi. Jaribu halafu utakuja kunambia.
 
nkuu nakushauri chukua Honda Fit. Ni gari dogo kama swift ila ina nafasi kubwa zaidi ndani na unaweza kupakia mzigo mkubwa sana kwa size ya gari. zile configurations za viti zinakupa uwezo mkubwa wa matumizi yake. kumbuka gari ina kazi sio kukutoa sehemu moja kwenda nyingine pekee. mafuta mimi Napata mpaka 16km kwa lita moja kwa safari za mjini na foleni. Niliwahi kwenda nacho morogoro na kurudi. nilitumia lita 18.5 kwa kutembea km 398 (kutokea bilicanas kwenda mitaa ya jamhuri stadium na kurudi tena mitaa ya bilicanas!) Honda Fit zimeanza kuenea mjini kwa hiyo spea sasa zinapatikana kwa urahisi zaidi. Jaribu halafu utakuja kunambia.
Mkuu asante sana kwa ushauri wako mzuri.

Vipi kuhusu bei ya kununua, ubora katika kudumu kati ya Honda Fit Vs Suzuki Swift?
 
Mkuu asante sana kwa ushauri wako mzuri.

Vipi kuhusu bei ya kununua, ubora katika kudumu kati ya Honda Fit Vs Suzuki Swift?


Manunuzi of course ni subject to vitu vingi km mileage, mwaka wa gari nk. ila kitu kimoja ambacho binafsi nina uzoefu nacho hususan kuhusiana na gari za Honda ni kuwa ni gari ngumu sana. labda uwe rough driver unaingia kwenye mashimo kama uko mashindanoni. lkn kwa decent driving hutoenda gereji ndugu yangu mpaka utamiss gereji. wewe ni service tu. sina uzoefu sana na swift zaidi ya kuwa niliwahi kuendesha moja ya rafiki yangu. kwa kweli driving experience yake sio nzuri kama ya Honda fit. nadhani kwa kukusaidia, nenda kwenye google halafu andika compare Honda fit and Suzuki swift. unaweza ukaweka miaka unayoilinganisha yani 2004 au 2005 etc. kasha andika users' reviews. hapo utapata maoni ya watumiaji wa gari zote mbili kasha utajua mchele na pumba. nakutakia kila la heri ila karibu kwenye umiliki wa Honda uwe mmoja wa madereva/wamiliki wenye kufurahia magari yao!!!
 
Back
Top Bottom