Kwenye kuendesha kuna kitu wanaita Optimal Speed. Hii inategemea na AERODYNAMIC ya gari.
Gari kama LaFerrari, Buggati Veyron, Zonda, Porsche, Mclaren na mengine mengi yaitwayo SPORTS CAR, yametengenezwa ili yaweze kuwa na Wind Resistance ndogo sana wakati yanasafiri. Masters katika hilo ni Formular 1 Car.
Ndege ili kupunguza Wind Resistance na hivyo kuchoma mafuta kidogo, husafiri juu sana angani kama km 8-10 juu ya usawa wa bahari. Huko upinzani wa upepo ni kidogo sana.
Hivyo hata kwenye magari, kila gari linategemea limetengenezwa vipi. Gari kama Range Rover ilivyokaa kama Box, unaona kabisa kuwa Wind Resistance itakuwa kubwa na hivyo likisafiri 180 km/hr litachoma mafuta mengi mno ili kufikia hiyo speed na hapo ndiyo mambo ya kW au Horsepower yanaanza kuonekana umuhimu wake.
Gari kama LaFerrari, unaweza kukuta linaanza kuchoma mafuta mengi kuzidi wastani kwenye speed kubwa zaidi ya ile iliyofikiwa na Range Rover au Bus au Roli.
Ukizidi hiyo Optimal Speed (Fuel Efficiency), mafuta yanaanza kutumika kwa wingi zaidi ya wastani. Ndiyo maana gari ya Veyron, linaonekana mara nyingi likiwa Fuel Station likipewa chakula yake.
Ndege za Wafaransa na UK ziitwazo Concord, kwa kitendo cha kuongeza speed mara mbili ya speed ya ndege za kawaida kubwa za abiria 1000km/hr, utumiaji mafuta wake ulikuwa mkubwa hadi ikafika wakati hizi ndege ikaonekana hazifai kabisa kwani kuzitunza ilikuwa gharama sana. Speed ya 2140 km/hr ilikuwa inakula mafuta si kawaida.
Sasa hivi wote wameishia kwenye Opitmal Speed ya 1000km/hr.
LaFerrari, Bugatti Veyron and Porsche 918 spyder.... Angalia Porsche anavyoachwa.....Laferrari anawaacha wote. Hizo HP zake sasa.....
nilichoelewa mpaka sasa ni kuwa km/h ni ileile kwa vyomboi vyote vinavyohusu mwendo. pia magari ya japan yanaweza kukimbia zaid ya 180km/h ila tu hiyo ndo standard waliyoamua kuandika kwenye dashboard. swali ni je ukiachilia mbali suala la cc ya engine nawezaje kujua horsepower ya gari ninalotumia? na je ni sahihi mwenye gari ya japan akiendesha mshale ukasoma 120km/h na mwenye la ulaya likasoma kwenye dashboard 240 km/h manake wa mwisho anamzid wa kwanza mara mbili kwa speed wanayokuwemo?