Msaada tiba ya jino

Msaada tiba ya jino

Habari ya muda huu wana jf, nasumbuliwa sana na jino, limeshambuliwa na wadudu....kuna yeyote mwenye kufahamu tiba yake bila kung'oa
Ntakuwa Dar baada ya siku nne. Kama utakuwa hujapata dawa utanitafuta nikupe dawa, tena bure.
 
sawa utachukua matunda yaliyoiva ya mti wa tura tura au wengine huita ndulele kama mawili matatu kulingana na ukubwa wa tunda, kisha utayakata kata halafu unaweka kwenye chombo utayakamua ile juisi yake halafu utachovya mswaki wako mpaka uenee kama dawa ya meno inavyokaa..
utaswaki kama dakika 3 mfululizo hapo utaona mapovu mengi mdomoni ila USIMEZE KABISA! na dawa ni chungu sana ila inavumilika utaendelea mpaka dakika 3 zikamilike, baada ya hapo utatema yale mapovu na utakaa kwa dakika 5 bila kusukutua kwa maji ya kawaida kisha zikipita utachukua maji ya vuguvugu utasukutua jino litapoa kabisa kabisa..
utaamua sasa wewe ukalizibe kama ni la kuziba au kama limeshakatika katika basi litakatika taratibu bila maumivu na unaweza kaa hata miaka mitatu halijauma, ikishindikana hiyo nitafute nikupatie dawa nyingine, shukran..

Papaa Gx Lissu jr94 davejillaonecka

View attachment 2131485

View attachment 2131486
Asante,hii ni ya kutunza kwa baadae
 
Habari ya muda huu wana jf, nasumbuliwa sana na jino, limeshambuliwa na wadudu....kuna yeyote mwenye kufahamu tiba yake bila kung'oa
Pata maganda ya mti wa Mlonge. Pondaponda na yachemshe (kama kikombe kimoja hivi). Sukutua kama unavyofanya wakati wa kubrashi meno. Unaweza kufanya asubuhi, mchana na jioni kwa siku tatu. Halafu nipe mrejesho.
 
Kwa ninavojua issue ya jino dawa huwa ni kung'oa tu, nyingine labda useme dawa ya kutuliza maumivu tu kwa muda.
 
Wadau nimerudi kwenye huu uzi kuwapa mrejesho, mlinipa msaada mkubwa sana, kila mmoja kwa kile alichoona kingenisaidia niwashukuru sana wote...binafsi niliamua kutumia ile njia niliyoona ina wepesi, basi niliamua kutumia dawa ya sensodyne kama ambavyo mmoja wa wana jf alivyoshauri hapa na mmoja wa wana jf.kwa kweli dawa ile iko vizuri sana...meno yametulia kabisa...kuanzia sasa sitoacha hiyo dawa...na ningependa niwashauri na wengine watumie dawa hii kama utaratibu wao wa kawaida kila siku kwa kuswakia asubuhi na usiku/jioni.
 
Wadau nimerudi kwenye huu uzi kuwapa mrejesho, mlinipa msaada mkubwa sana, kila mmoja kwa kile alichoona kingenisaidia niwashukuru sana wote...binafsi niliamua kutumia ile njia niliyoona ina wepesi, basi niliamua kutumia dawa ya sensodyne kama ambavyo mmoja wa wana jf alivyoshauri hapa na mmoja wa wana jf.kwa kweli dawa ile iko vizuri sana...meno yametulia kabisa...kuanzia sasa sitoacha hiyo dawa...na ningependa niwashauri na wengine watumie dawa hii kama utaratibu wao wa kawaida kila siku kwa kuswakia asubuhi na usiku/jioni.
Ya ndulele umeiacha mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom