Anigrain
JF-Expert Member
- Nov 15, 2020
- 1,698
- 4,284
Habari zenu wakuu...! Niende kwenye mada moja kwa moja
Sehemu nayoishi kuna tatizo la umeme kuwa hauna nguvu/umeme mdogo kiasi kwamba kuna baadhi ya vifaa vya umeme ukiwasha haviwaki au vinawaka kwa kusua sua sana
Kutokana na tatizo hilo ikawa ni ngumu kutumia fridge Kwani muda wote umeme unapanda na kushuka, nikashauliwa nitafute stabilizer ili inisaidie kwenye issue ya fridge
Nikatafuta na kuanza kutumia, siku ya Kwanza kuanza kutumia ilipiga kazi vizuri na Fridge liakawa linawaka muda wote tofauti na mwanzo
Ila shida imeakuja jana usiku baada ya kushtukia tu Stabilizer imezima ghafra, nikajaribu kuangalia dalili za shoti ila sikuona, ikabidi nifungue sehumu iliyoandikwa Fuse, na kukuta imeungua
Ikabidi leo niwe na kazi ya kutafuta replacement, ile Fuse niliyoikuta ilikuwa ina 10A, hivo ikanilazimu kutafuta hiyo hiyo ila sikufanikiwa kupata, nikapata ya 6A
Nimekuja kujaribu kuweka ila hii ndio imeungua mapema sana ata kabla ya fridge kuwaka, nikaweka tena ingine na habari ikawa ni ile ile
Sasa nimekuja kwa wenye uelewa na hivi vitu, je natakiwa kupata exactly Fuse yenye 10A? na nimejaribu kutafuta kwa maeneo yangu nimefeli kupata, je naweza kuweka iliyo juu ya 10A? Mfano nikipata 12/13A?
Athari zake zinaweza kuwa zipi endapo nikiweka Fuse yenye Ampire kubwa kuliko ile iliyokuwepo mwanzo? Na hiyo ya 10A naweza kupata wapi kwa urahisi
NB: Kwa sasa nipo Vikindu-Mkuranga
Sehemu nayoishi kuna tatizo la umeme kuwa hauna nguvu/umeme mdogo kiasi kwamba kuna baadhi ya vifaa vya umeme ukiwasha haviwaki au vinawaka kwa kusua sua sana
Kutokana na tatizo hilo ikawa ni ngumu kutumia fridge Kwani muda wote umeme unapanda na kushuka, nikashauliwa nitafute stabilizer ili inisaidie kwenye issue ya fridge
Nikatafuta na kuanza kutumia, siku ya Kwanza kuanza kutumia ilipiga kazi vizuri na Fridge liakawa linawaka muda wote tofauti na mwanzo
Ila shida imeakuja jana usiku baada ya kushtukia tu Stabilizer imezima ghafra, nikajaribu kuangalia dalili za shoti ila sikuona, ikabidi nifungue sehumu iliyoandikwa Fuse, na kukuta imeungua
Ikabidi leo niwe na kazi ya kutafuta replacement, ile Fuse niliyoikuta ilikuwa ina 10A, hivo ikanilazimu kutafuta hiyo hiyo ila sikufanikiwa kupata, nikapata ya 6A
Nimekuja kujaribu kuweka ila hii ndio imeungua mapema sana ata kabla ya fridge kuwaka, nikaweka tena ingine na habari ikawa ni ile ile
Sasa nimekuja kwa wenye uelewa na hivi vitu, je natakiwa kupata exactly Fuse yenye 10A? na nimejaribu kutafuta kwa maeneo yangu nimefeli kupata, je naweza kuweka iliyo juu ya 10A? Mfano nikipata 12/13A?
Athari zake zinaweza kuwa zipi endapo nikiweka Fuse yenye Ampire kubwa kuliko ile iliyokuwepo mwanzo? Na hiyo ya 10A naweza kupata wapi kwa urahisi
NB: Kwa sasa nipo Vikindu-Mkuranga