msaada tafadhali - polisi bana

noella

Senior Member
Joined
Mar 21, 2011
Posts
101
Reaction score
50
Najua hapa si mahala pake ila ndo penye wengi wapendwa nahitaji msaada wenu.

Nilireport mtu kunitishia maisha kituo kimoja cha polisi hapa dar,nikapewa RB.baada ya siku mbili nikapigiwa simu
na polisi ambaye alijitambulisha kama mpelelezi wa kesi yangu, akaniambia niende anisikilize,kesho yake nikaenda. nikamsimulia kisa chote. sasa polisi kutaka hela eti amenifanyia counselling halafu akamuita na yule mshtakiwa nae akamtoa hela na akamfanya wawe marafiki wakaenda bar kunywa.

kesho yake yule polisi akaniita tena kunipa feedback ya alichokisikia kutoka kwa mshtakiwa.badala ya kunipa feedback sasa akaanza kunitongoza alivyoona sielekei akanambia kwa kuwa sitaki mshtakiwa aende mahakamani basi inabidi tufunge kesi na itanibidi nilipie dolar mia nne, nikashangaa sana.nikamwambia mimi sina hela.akasema hata laki mbili mana wako wengi pale mkuu wa kituo kufunga kesi anaona kama ni usumbufu na maelezo meengi.mi nikachoka sasa nimeamua simpokei simu yake tena.lakini anatuma msg kuuliza nitaenda lini kufunga kesi.

nahitaji kujua, je nikifungua jalada nikapewa RB je ni lazima kufunga kesi?kama ndio je inalipiwa kufunga hiyo kesi? what if nahitaji bado kuitumia hiyo RB just incase mshtakiwa akikurupuka kunitishia tena? nahitaji mwongozo wenu please.
 

Sina haja ya kusoma post yako kwa sababu umesema si mahala pake jua kitu chochote kikikaa sehemu ambayo si mahala pake ni uchafu.
 
Nenda kwa firm za wanasheria kwani hawa polisi ni michosho tu.
 
Sina haja ya kusoma post yako kwa sababu umesema si mahala pake jua kitu chochote kikikaa sehemu ambayo si mahala pake ni uchafu.

nilihitaji msaada wa haraka na hapa najua wengi wanapapenda na hakuna linaloshindikana ndo mana nimeanza kwa kusema hivyo.

hata hivyo umesoma,usingesoma usingeweza kucomment.

watu wengine bwana ovyo
 
Sina haja ya kusoma post yako kwa sababu umesema si mahala pake jua kitu chochote kikikaa sehemu ambayo si mahala pake ni uchafu.

hapa wewe ndo umehara, fanya itusafishie hali ya hewa
 
Hupaswi kulipa chochote katika kufunga au kufungua file. Kama anakughasi mpr za takukuru ili acheke naxo
 
Yan nilivyokwambia nisisikie umeolewa au unaboy friend, nikisikia nakuua imekua, ishu!!
 
kisheria hutakiwi kulipia gharama yoyote ile kesi inafutwa then unatia sign mchezo umekwisha..hamna gharama za kufungua wala kufunga jalada...over..tena nahisi kesha jua hujui haki zako kama vipi muulize swali hili anatumia kifungu kipi cha sheria kuhalalisha ulipaji wa ufungaji wa hilo jalada..amini..hatakusumbua au mwambie ngoja niwasiliane na mwanasheria wangu..uone lazima atakaaa.....
 

Mbona haijakaa vizuri. Unapofungua jalada si unaandika statement na kuweka sahihi. Huyu mpelelezi alikuita ofisini au wapi? Je, Una uhusiano gani na aliyekutishia? Usiogope mahakama wewe utaitwa tu kama shahidi.
 
duh hii mambo imefikaje huku
nahitaji kujua, je nikifungua jalada nikapewa RB je ni lazima kufunga kesi?kama ndio je inalipiwa kufunga hiyo kesi? what if nahitaji bado kuitumia hiyo RB just incase mshtakiwa akikurupuka kunitishia tena? nahitaji mwongozo wenu please.



kisheria (kama zinafatwa) kufungua kesi ni bure na kufunga pia ilimradi haija fika mahakamani ni bure.

ukitoa taarifa inayoingizwa kwenye report book (RB), unapewa kikaratasi fulani chenye reference number ya hiyo taarifa yako iliyoingizwa kwenye report book.

maana yake umetoa taarifa na umwonapo mtuhumiwa unaweza kutoa taarifa kwa polisi yoyote aliye karibu nawe ili amkamate na kumfikisha kwenye kituo ulicho fungulia kesi

rb ina expire kwa kesi ambayo wewe na unaye mtuhumu mme amua kuya maliza mbele ya polisi au mmefikishana mpaka mahakamani na hakimu akatoa uamuzi. pia sheria huwa inazuia makosa kufufuliwa baada ya muda fulani uliowekwa kupita (angalia law of limitation act) otherwise unaweza kuitumia
 


Asante nash.sasa namsubiria apige tena simu nimuulize maswali ya kipolisi na yeye atajuta..kesi nifungue mimi afu anisumbue yeye hawa mapolisi njaa sijui vipi..ubarikiwe.
 
Asante nash.sasa namsubiria
apige tena simu nimuulize maswali ya kipolisi na yeye atajuta..kesi
nifungue mimi afu anisumbue yeye hawa mapolisi njaa sijui
vipi..ubarikiwe.

Ww nae una njaa,ss ulifungua kesi ya nn kama hutaki kwenda mahakamani?
 
Ww nae una njaa,ss ulifungua kesi ya nn kama hutaki kwenda mahakamani?
Kuna tofauti kati ya kutoa taarifa ya kutishiwa na kufungua jalada la mashtaka. Polisi wanajua jinsi ya kula hela ya wasiojua sheria.

tatizo hapa atakuwa ameulizwa ana uhusiano gani na aliyemtisha na akaambiwa leta namba ya simu. katika kuchukua taarifa, polisi atakuwa alimuona kama ni easy target.

kumbuka ukienda polisi ni sawa na umekwenda kwenye genge la majambazi, unatakiwa kuwa makini sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…