Msaada: Sielewi tofauti ya dunia na ulimwengu

Msaada: Sielewi tofauti ya dunia na ulimwengu

wa stendi

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2016
Posts
26,008
Reaction score
28,342
Wakuu poleni na majukumu,

Husika na kichwa cha habari hapo juu, hivi wakuu ni nini tofauti ya dunia na ulimwengu, hua nashindwa kuelewa, naomba kujuzwa.

Nawasilisha!
 
dunia ni sayari ya Tatu
ulimwengu maeneo yote yanayokaliwa na watu ndani ya dunia.... lakini subiri Bakita wanakuja
 
Dunia ni sayari, ulimwengu in vilivyomo kama mito maziwa milima watu n.k.
 
Dunia ni hii sayari ya tatu kutoka juani ambamo sisi tunaishi.
Dunia hii inapimika, namaanisha ina uzito wake unaojulikana, kipenyo chake nk.
Lakini ulimwengu haupimiki, hauna mwisho. Vyote unavyoviona huko juu vipo katika ulimwengu.
 
Dunia ni hapa mahala tunapoishi ambayo ni sayari ya tatu ktk mfumo wa jua/solar systen.

ulimwengu ni mahala pote means that nyota,galaksi,sayari na kila kitu ambacho kinapatikana kwenye anga vipo ktk ulimwengu kwa ujumla unaweza sema ulimwengu umekombaini kila kitu.
 
Dunia sayari ( ardhi )
Ulimwengu. ( watu waishio kwenye ardhi au eneo la ardhi)

Dunia=ardhi
Ulimwengu=ardhi +watu
 
Mkuu wa stendi ukishaeleweshwa inabidi uwe unatupa mrejesho wa nini ulichoambulia/elewa!
 
Dunia ni umbo la kijiografia.

Ulimwengu ni watu na viumbe hai ndani ya dunia..
 
Dunia ni eneo la sayari tayoishi na ulimwengu ndio sisi+vitu
Walimwengu specifics means watu wa humu ulimwenguni!
 
Ulimwengu ni Mfumo wa Jua (the whole solar system), wakati Dunia ni sayari ya tatu kati mpangilio wa sayari unaoopatikana katika Mfumo wa Jua.

Katika muktadha mwingine, Ulimwengu ni Fikra zinazoambatana na matendo yote ya binadamu.
Anaita sasa.
 
Back
Top Bottom