Msaada nyumba ya Jirani; CHADEMA haitajengwa na Lowassa

Juliana Shonza

JF-Expert Member
Dec 19, 2012
2,009
1,607
Miongoni mwa mambo ya msingi sana ambayo kila mwanasiasa ama taasisi ya siasa wanatakiwa kuwa nayo ni DIRA, Dira ndio inatoa mwelekeo kwenye mpango kazi kuwa mnaamua kuwa na taasisi ya aina gani, ifikie malengo yapi na kwa muda gani. Mkikosa DIRA taasisi yenu siku zote itaendeshwa kwa mitazamo na maono ya baadhi ya watu ama mtu na atawapeleka pale anapoona yeye ni sahihi na kwa wakati anaojisikia yeye kuwapeleka hapo.

Nifupishe maandishi, nimeona kwenye vyombo vya habari leo hii, wameandika LOWASSA: NITAIJENGA CHADEMA na wameendelea kwenye story hiyo kuelezea mpango wa ziara za kichama nchi nzima ambazo EDO amejiandaa kuzifanya. Sawa..ila naomba niwasaidie kufikiri.

1. TATHIMINI.
Naomba kuwauliza, mliwahi kukutana na kupeana tathimini za matokeo ya uuchaguzi mkuu, mkaulizana wapi mliteleza na wapi mlipatia..??? ili sasa katika mpango wa KUIJENGA CHADEMA muanze na pale mlipoteleza.

Lakini swali lingine la msingi sana, Mmefanya tathimini ndani ya miezi sita ya MAGUFULI '"the bulldozer'' madarakani "HALI YA SIASA"ya nchi imekaaje..? mmeusoma upepo..?

Naomba niwasaidie TAKWIMU fupi kabisa;
a) Wananchi "hata wanachama na viongozi wa Chadema" wanaendelea kuiunga mkono Serikali ya CCM chini ya MAGUFULI. Hatua zinazoendelea kuchukuliwa za kutumbua majipu "ambazo CHADEMA kwa influence ya EDO wanazipinga" wananchi wanazikubali. Taasisi ya CZI wametoa majibu ya utafiti wao wakionyesha kuwa MAGUFULI ni namba moja the most influencial figure kwa sasa, wakifuatiwa na akina MAJALIWA na wengineo,,,LOWASSA hata kwenye 20 bora hayupo...,how could he build your party.,kwa influence gani..?

b) LOWASSA anakimbiwa na aliowaita "MARAFIKI ZAKE" hata wale maswahiba na waimba zumari waliohama nae wakitoka CCM wanarudi makundi kwa makundi, Vijana wake wa 4U Movement and Lowassa for Change ni Vinara wa kumkana kwenye mitandao, leo Peter Mwininga na kundi lake, hatawaki kabisa kuhusishwa na Lowassa, Mwapachu amesharudi, Kingunge, Mgeja na Msindai wameandika barua kwa Mwenyekiti wa CCM ili waweze kurudishwa.

Wenyeviti wa UVCCM wa Mikoa na Wilaya waliohama kipindi cha uchaguzi wakiongozwa na Mwenyekiti wa Wilaya ya ROMBO Beatrice Condrad wamerudi CCM, makundi kwa makundi ya Vijana wanajiunga na CCM hasa wale Viongozi wa CHADEMA.

TAKWIMU Hazidanganyi, Wenyeviti wa BAVICHA wa Wilaya zaidi ya TANO wameshajiunga na CCM ndani ya Miezi sita ya utawala wa MAGUFULI tena kutoka katika Mikoa ambayo inatajwa kuwa NGOME ya CHADEMA kama yule wa MBEYA.

Wenyeviti wa CHADEMA waliojiunga na CCM nao hawana hesabu, hivi hamuangalii vyombo vya habari, Mwenyekiti wa Wilaya ya Lindi Mjini na hata huyu wa Juzi tu wa Wilaya ya Iringa mjini tena Wilaya ambayo mbunge wake ni wa CHADEMA, bado uongozi wa CHAMA unateteleka..? Hamjiulizi..??

Waliokuwa wagombea UBUNGE nao wanahama CHADEMA bila hesabu, jana pekee wamerudi wawili aliyekuwa Mgombea wa Ubunge Manispaa ya Morogoro na yule wa Mvomero..bado mnasema LOWASSA is right person kukijenga CHADEMA na kwamba he's influencial enough.???

Nasema hivi, Hata Influence ndani ya MONDULI nyumbani kwake imekwisha kabisa. Kijana ambaye alikuwa Mkoba wake, mtunza siri wa nyumbani na MUUMINI wa LOWASSA Ndugu Elisante KIMARO nae AMESHAMKANA mara tatu kwenye mikutano ya hadhara ndani ya Wilaya ya MONDULI.....i can't see how is this person anakuwa MJENZI wa chama..?

Hivi mnafahamu maana ya KUJENGA chama..? neno Kujenga ama MJENZI mnafahamu ni mtu wa aina gani..???

Bado nashindwa kuelewa kuwa kimewakuta kipi ninyi ndugu zangu..? yale maarifa ya zamani yamekwenda wapi..? MJENZI wa Chama ataanza kuzunguka kwenye mikutano ya hadhara, wananchi watamuhoji juu ya kesi ya Mwanae SIOI ya WIZI wa Trilioni moja..mnataka ajibu nini..? mnajenga CHAMA gani..??? HOVYO KABISA..
 
Hapa ulikusudia kuandika nini dada? Ama mie ndo sijaelewa. Hata hivyo uchambuzi wako umeshiba kweli

"Wenyeviti wa UVCCM wa Mikoa na Wilaya wakiongozwa na Mwenyekiti wa Wilaya ya ROMBO Beatrice Condrad wamerudi CCM, makundi kwa makundi ya Vijana wanajiunga na CCM hasa wale Viongozi wa CHADEMA".
 
What-is-Wrong-with-this-CCM-Photo.png
UVCCM_wakipigana.jpg


Hawa ndio watajenga nyumba ya CCM.


swissme
 
Hapa ulikusudia kuandika nini dada? Ama mie ndo sijaelewa. Hata hivyo uchambuzi wako umeshiba kweli

"Wenyeviti wa UVCCM wa Mikoa na Wilaya wakiongozwa na Mwenyekiti wa Wilaya ya ROMBO Beatrice Condrad wamerudi CCM, makundi kwa makundi ya Vijana wanajiunga na CCM hasa wale Viongozi wa CHADEMA".
Nilimaanisha wale ambao walihama kipindi cha uchaguzi, wakasombwa na MAFURIKO, nao wameanza kurudi CCM kwa kasi ile ile ya MAFURIKO.
 
Nilimaanisha wale ambao walihama kipindi cha uchaguzi, wakasombwa na MAFURIKO, nao wameanza kurudi CCM kwa kasi ile ile ya MAFURIKO.
Ahsante sana Mheshimiwa kwa ufafanuzi huu mujarab. Othewise nikupongeze tu kwa kuwatetea akina mama wa Songwe ambao wanateseka kwa kukosekana huduma bora ya maji safi na salama
 
Kavurugwa huyo. Kwa akili za MACHADEMA, hakuna mwenye uwezo wa kujibu kwa hoja kama alivyoandika Mheshimiwa Juliana Shonza
Kama huyo sijui Swiss huwa hana uelewa wa chochote, yeye akiona neno CHADEMA tu anakurupuka kutetea bila maarifa.
 
Mh muda mfupi ulopita nimekuona ukichangia hoja mjengoni, inamaana umetoka nje Mara hii? Au unaandika upo mjengoni?
 
Nilimaanisha wale ambao walihama kipindi cha uchaguzi, wakasombwa na MAFURIKO, nao wameanza kurudi CCM kwa kasi ile ile ya MAFURIKO.
Nikusaidie tu dada yangu ni kweli baadhi ya wananchi wanaukubali utendaji wa Magufuli so far,Lakini usijidanganye wanaikubali CCM kama unavyodhani hasa nyie wabunge na UvCCM ambao mnaonekana ni bendera fuata upepo.Kuhusu tathmini ya uchaguzi walishafanya Moshi kama sijakosea na huo utafiti wa CZI nadhani Watanzania wengi hata bado hawajajua hicho ni kitu gani(CZI) na nini dhumuni lake la kuibuka siku za karibuni.
 
Miongoni mwa mambo ya msingi sana ambayo kila mwanasiasa ama taasisi ya siasa wanatakiwa kuwa nayo ni DIRA, Dira ndio inatoa mwelekeo kwenye mpango kazi kuwa mnaamua kuwa na taasisi ya aina gani, ifikie malengo yapi na kwa muda gani. Mkikosa DIRA taasisi yenu siku zote itaendeshwa kwa mitazamo na maono ya baadhi ya watu ama mtu na atawapeleka pale anapoona yeye ni sahihi na kwa wakati anaojisikia yeye kuwapeleka hapo.

Nifupishe maandishi, nimeona kwenye vyombo vya habari leo hii, wameandika LOWASSA: NITAIJENGA CHADEMA na wameendelea kwenye story hiyo kuelezea mpango wa ziara za kichama nchi nzima ambazo EDO amejiandaa kuzifanya. Sawa..ila naomba niwasaidie kufikiri.

1. TATHIMINI.
Naomba kuwauliza, mliwahi kukutana na kupeana tathimini za matokeo ya uuchaguzi mkuu, mkaulizana wapi mliteleza na wapi mlipatia..??? ili sasa katika mpango wa KUIJENGA CHADEMA muanze na pale mlipoteleza.

Lakini swali lingine la msingi sana, Mmefanya tathimini ndani ya miezi sita ya MAGUFULI '"the bulldozer'' madarakani "HALI YA SIASA"ya nchi imekaaje..? mmeusoma upepo..?

Naomba niwasaidie TAKWIMU fupi kabisa;
a) Wananchi "hata wanachama na viongozi wa Chadema" wanaendelea kuiunga mkono Serikali ya CCM chini ya MAGUFULI. Hatua zinazoendelea kuchukuliwa za kutumbua majipu "ambazo CHADEMA kwa influence ya EDO wanazipinga" wananchi wanazikubali. Taasisi ya CZI wametoa majibu ya utafiti wao wakionyesha kuwa MAGUFULI ni namba moja the most influencial figure kwa sasa, wakifuatiwa na akina MAJALIWA na wengineo,,,LOWASSA hata kwenye 20 bora hayupo...,how could he build your party.,kwa influence gani..?

b) LOWASSA anakimbiwa na aliowaita "MARAFIKI ZAKE" hata wale maswahiba na waimba zumari waliohama nae wakitoka CCM wanarudi makundi kwa makundi, Vijana wake wa 4U Movement and Lowassa for Change ni Vinara wa kumkana kwenye mitandao, leo Peter Mwininga na kundi lake, hatawaki kabisa kuhusishwa na Lowassa, Mwapachu amesharudi, Kingunge, Mgeja na Msindai wameandika barua kwa Mwenyekiti wa CCM ili waweze kurudishwa.

Wenyeviti wa UVCCM wa Mikoa na Wilaya waliohama kipindi cha uchaguzi wakiongozwa na Mwenyekiti wa Wilaya ya ROMBO Beatrice Condrad wamerudi CCM, makundi kwa makundi ya Vijana wanajiunga na CCM hasa wale Viongozi wa CHADEMA.

TAKWIMU Hazidanganyi, Wenyeviti wa BAVICHA wa Wilaya zaidi ya TANO wameshajiunga na CCM ndani ya Miezi sita ya utawala wa MAGUFULI tena kutoka katika Mikoa ambayo inatajwa kuwa NGOME ya CHADEMA kama yule wa MBEYA.

Wenyeviti wa CHADEMA waliojiunga na CCM nao hawana hesabu, hivi hamuangalii vyombo vya habari, Mwenyekiti wa Wilaya ya Lindi Mjini na hata huyu wa Juzi tu wa Wilaya ya Iringa mjini tena Wilaya ambayo mbunge wake ni wa CHADEMA, bado uongozi wa CHAMA unateteleka..? Hamjiulizi..??

Waliokuwa wagombea UBUNGE nao wanahama CHADEMA bila hesabu, jana pekee wamerudi wawili aliyekuwa Mgombea wa Ubunge Manispaa ya Morogoro na yule wa Mvomero..bado mnasema LOWASSA is right person kukijenga CHADEMA na kwamba he's influencial enough.???

Nasema hivi, Hata Influence ndani ya MONDULI nyumbani kwake imekwisha kabisa. Kijana ambaye alikuwa Mkoba wake, mtunza siri wa nyumbani na MUUMINI wa LOWASSA Ndugu Elisante KIMARO nae AMESHAMKANA mara tatu kwenye mikutano ya hadhara ndani ya Wilaya ya MONDULI.....i can't see how is this person anakuwa MJENZI wa chama..?

Hivi mnafahamu maana ya KUJENGA chama..? neno Kujenga ama MJENZI mnafahamu ni mtu wa aina gani..???

Bado nashindwa kuelewa kuwa kimewakuta kipi ninyi ndugu zangu..? yale maarifa ya zamani yamekwenda wapi..? MJENZI wa Chama ataanza kuzunguka kwenye mikutano ya hadhara, wananchi watamuhoji juu ya kesi ya Mwanae SIOI ya WIZI wa Trilioni moja..mnataka ajibu nini..? mnajenga CHAMA gani..??? HOVYO KABISA..
Upo sahihi,Mbowe aione hii
 
Ukiona wanakusema Sana jua mioyoni mwao wanakukubali, muda bado maghu aliahidi ahadi za 123 trillions kipindi cha kampeni tunamsubiri amalize kutekeleza ila mpaka sasa sukari imeishamshinda tunaangalia jambo gani jingine litakalo mshinda
 
Tamaa ilimponza fisi.

Wewe mbona ulishindwa kuijenga CHADEMA, na badala yake mkaanza KUIBOMOA chini kwa chini na wenzako?!

Tuache tuijenge sisi.

Wewe endelea na UMAALUMU wako.
 
Back
Top Bottom