Msaada, nitapata wapi maziwa ya infacare?

Msaada, nitapata wapi maziwa ya infacare?

moudoudo og

Member
Joined
Jan 30, 2015
Posts
24
Reaction score
0
Habari za asubuhi wakuu,

Poleni na mihangaiko na majukumu. Kwa yeyote anayejua yanapopatikana maziwa ya Watoto wachanga infacare namba 1 naomba anisaidie kunielekeza, Mimi nipo Dar nimetafuta maduka mengi nimekosa na mwanangu ndio anatumia hayo. Kwa yeyote anayejua Tafadhali!
 
Nenda supermarket ya TSN pale karibu na Muhimbili barabara ya umoja wa mataifa au TSN ya Bamaga.
 
Namba ngapi kama ni no3 haipo sokoni hata nyingine ndiyo zinaishia
 
utayapata dukani na yatakuwa kwenye kopo....
 
Hayo maziwa ni shida kidogo kwa sasa, nenda Namanga pale madukani kwa wapemba utapata, ukikosa niambie nikuelekeze sehemu nyengine
 
Asante,ngoja kwanza niyatafute Leo kote mlikonielekeza nikikosa nitampa hayo s26
 
Hayo maziwa ni shida kidogo kwa sasa, nenda Namanga pale madukani kwa wapemba utapata, ukikosa niambie nikuelekeze sehemu nyengine

Mkuu utafiti nimekosa halo namanga naomba unielekeze wapi pengine naweza kuyapata
 
Back
Top Bottom