Msaada: Naumwa fangasi sehemu za siri kwa muda mrefu

galileo zach

Senior Member
Nov 6, 2015
116
72
Habari zenu, naombeni msaada nimekuwa na tatizo la fungasi sehemu za siri kwa muda.

Nilipima VDRL nikawa sina kitu ndio nikaambiwa kwamba ni fungus ila mpaka kujua hilo nilikuwa nimeanza kutoka vipele sehemu za siri haswa kwenye mkanda karibu na kichwa vinatoa maji na kuwashwa halaf baadae vinakuwa kama vidonda.

Nimepewa dawa nyingi sana za kupaka ila hazisaidi nikachuma na sindano 5 za powersafe ila bado naombeni msaada kwa sasa hadi nikikojoa karibu na kichwa nasikia maumivu makali.

Naombeni msaada wakuu.
 
picha tafadhali
picha hiyo wakuu
IMG_20230802_190516_142.JPG
 
Pumbu jero Stage 3 hiyo.
Hakikisha uko dry muda mwingi na mzigo upate hewa/Ubaridi kwa Sana Mana joto ndio lao.
Kuwasha kokote usikune kwa kukwangua ikibidi tumia kitambaa au pamba kugusagusa.

Oga na angushia powder
wakati wa kulala na usivae nguo zenye kuleta joto au kubana.
Hakuna kurudia na zingatia usafi wa nguo hasa za ndani na taulo.
Tumia Fungistat Cream....kwa kuwa inasababisha joto
paka dk15 kabla ya kuoga then oga mwagia poda.
 
Kama upo sehemu yenye joto kama dsm, pwani au moro na una uwezo wa kwenda sehemu yenye baridi sana kama njombe au mbeya basi nenda huko. Ndani ya mwezi mmoja Tu unapona.

Kama haiwezekani basi uwe unaweka maji ya kuosha hizo sehemu kwenye friji au freezer na uoshe maji yakiwa ya baridi sana. Kwa siku osha na hayo maji zaidi ya mara mbili na ukipata nafasi uwe kama unaziloweka kwa muda mrefu kidogo.

NB: Kumbuka kujikausha vizuri na kupaka mafuta ya mgando
 
Habari zenu ,naombeni msaada nimekuwa na tatizo la fungasi sehemu za siri kwa muda.

nNlipima VDRL nikawa sina kitu ndio nikaambiwa kwamba ni fungus ila mpaka kujua hilo nilikuwa nimeanza kutoka vipele sehemu za siri haswa kwenye mkanda karibu na kichwa vinatoa maji na kuwashwa halaf baadae vinakuwa kama vidonda.

Nimepewa dawa nyingi sana za kupaka ila hazisaidi nikachuma na sindano 5 za powersafe ila bado naombeni msaada kwa sasa hadi nikikojoa karibu na kichwa nasikia maumivu makali.

Naombeni msaada wakuu
Mkuu pole sana kwa maradhi yako nitafute mimi kwa wakati wako ili niweze kukutibia upate kupona maradhi yako.
 
Back
Top Bottom