Msaada: Natafuta kazi yoyote ya halali

Msaada: Natafuta kazi yoyote ya halali

beautybrain

Member
Joined
Mar 8, 2016
Posts
38
Reaction score
35
Natumai humu ndani wote ni wazima wa Afya.
Kwa mara nyingine Tena nakuja kwenye jukwaa hili kuomba nafasi yoyote ya kazi ambayo itakuwa halali.
Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 24, Elimu yangu nina Bachelor of Arts in Sociology,ambayo nimehitimu mwaka Jana.
Uzoefu wa kazi.
nilipohitimu masomo yangu nilibahatika kupata kazi katikati hoteli moja hapa Dar es salaam ambayo ilikuwa chini ya usimamizi wa wachina, ambayo nilikuwa nafanya nafasi ya Receptionist, kazi ambazo niliokuwa nafanya kama zifuatazo;
-kumuandikisha mteja anapofika mfano kumpa fomu ya kujaza na kuskanii passport yake.
-kuandaa na kuchukua malipo kwa mteja.
-kushughulikia malalamiko ya mteja.
-kukamilisha taratibu za kuja na kuondoka kwa mteja.
*sababu ya kutoendelea na hii kazi ni kwamba hotel ilishindwa kuendelea.

Ukiachana na kazi ya receptionist vilevile Nina uzoefu wa kazi ya Insurance Benefit ambazo nilikuwa nafanya kazi kama Insurance Benefit officer, nilikuwa na majukumu yafuatayo;

-Kufuatilia Masai,malipo pamoja na kanuni za matibabu ya bima ya Afya kwa Wateja.
_Kuhifadhi na kudumisha rekodi za mgonjwa katika vituo mbalimbali vya Afya.
_Kuandaa report na rekodi za mgonjwa.
Vilevile katika masomo ya darasa nimejifunza Fani mbalimbali kama guidance and counseling,Social psychology,vilevile nimejifunza principle of human resource Management and administration.
Vilevile Nina uwezo wa kutumia computer application kama vile Ms.words,Excel,PowerPoint and Internet.
NB:nahitaji kazi yoyote Ile hata ya kujitolea ambayo itaweza kunisaidia nauli na kula..ili niongeze ujuzi kuliko kukaa nyumbani.
Ahsante Sana na Mungu awabariki.
 
Umeongea ukweli mtupu endelea kumuomba Mungu utapata ila ni vizur ungeanza kwa kujiajir njoo Dm nitakupatia mtaji uanze hata kuuza juice hy itakusaidia na kukupa sababu ya kukutana na watu watakaokusaidia
 
Umeongea ukweli mtupu endelea kumuomba Mungu utapata ila ni vizur ungeanza kwa kujiajir njoo Dm nitakupatia mtaji uanze hata kuuza juice hy itakusaidia na kukupa sababu ya kukutana na watu watakaokusaidia
Ahsante mkuu
 
Umeongea ukweli mtupu endelea kumuomba Mungu utapata ila ni vizur ungeanza kwa kujiajir njoo Dm nitakupatia mtaji uanze hata kuuza juice hy itakusaidia na kukupa sababu ya kukutana na watu watakaokusaidia
Mbona wanaume wanaokuja kuomba msaada humu hamuwasaidii comment kama hizi sizioni kabisa thread za jinsia ya kiume wakiomba msaada ...hili jambo linashangaza kweli duh
 
Na tena hawa wadada wawe makini sana, maana wanaume wakitafuta kazi humu hakuna comment za hata kuwapa moyo. shauri yenu wadada
Mkuu kwan wew hujagundua kitu bado ..me nishagundua..positive na positive Sikh zote zinakwepana...positive na negative zinavutana...sijui kwanin wanaume tupo ivoo
 
Mkuu kwan wew hujagundua kitu bado ..me nishagundua..positive na positive Sikh zote zinakwepana...positive na negative zinavutana...sijui kwanin wanaume tupo ivoo
Hapana mkuu, wale wote wanaojifanya kutaka kuwasaidia wadada sio kama kweli wanataka wawasaidie. Kuna kuwa kuna agenda pale
 
Kuna wasiwasi wa kupata kazi haramu, naona kila dalili
 
Natumai humu ndani wote ni wazima wa Afya.
Kwa mara nyingine Tena nakuja kwenye jukwaa hili kuomba nafasi yoyote ya kazi ambayo itakuwa halali.
Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 24, Elimu yangu nina Bachelor of Arts in Sociology,ambayo nimehitimu mwaka Jana.
Uzoefu wa kazi.
nilipohitimu masomo yangu nilibahatika kupata kazi katikati hoteli moja hapa Dar es salaam ambayo ilikuwa chini ya usimamizi wa wachina, ambayo nilikuwa nafanya nafasi ya Receptionist, kazi ambazo niliokuwa nafanya kama zifuatazo;
-kumuandikisha mteja anapofika mfano kumpa fomu ya kujaza na kuskanii passport yake.
-kuandaa na kuchukua malipo kwa mteja.
-kushughulikia malalamiko ya mteja.
-kukamilisha taratibu za kuja na kuondoka kwa mteja.
*sababu ya kutoendelea na hii kazi ni kwamba hotel ilishindwa kuendelea.

Ukiachana na kazi ya receptionist vilevile Nina uzoefu wa kazi ya Insurance Benefit ambazo nilikuwa nafanya kazi kama Insurance Benefit officer, nilikuwa na majukumu yafuatayo;

-Kufuatilia Masai,malipo pamoja na kanuni za matibabu ya bima ya Afya kwa Wateja.
_Kuhifadhi na kudumisha rekodi za mgonjwa katika vituo mbalimbali vya Afya.
_Kuandaa report na rekodi za mgonjwa.
Vilevile katika masomo ya darasa nimejifunza Fani mbalimbali kama guidance and counseling,Social psychology,vilevile nimejifunza principle of human resource Management and administration.
Vilevile Nina uwezo wa kutumia computer application kama vile Ms.words,Excel,PowerPoint and Internet.
NB:nahitaji kazi yoyote Ile hata ya kujitolea ambayo itaweza kunisaidia nauli na kula..ili niongeze ujuzi kuliko kukaa nyumbani.
Ahsante Sana na Mungu awabariki.
utaweza kuwa nany!
 
Back
Top Bottom