Keen
JF-Expert Member
- Sep 27, 2007
- 617
- 172
Chama chetu cha Mapinduzi sasa hakipendwi kama mwanzo wake. Hakiaminiwi kirahisi hata pale kulikokuwa na ngome za chama chetu kama Lindi na Mtwara.Kinalalamikiwa;kinazidi kuchukiwa. Yawezekana kuna tatizo la ki-mfumo...mazoea. Lakini,wapo watu ndani ya chama chetu ambao ndio walezi wa mfumo huo unaosawajisha heshima ya chama chetu. Mkiwa kama watanzania wenye vyama na msio na vyama,ni nani hasa ni tatizo katika CCM yetu? Kwanini? Tusaidieni ili tujirekebishe na kuimarisha chama chetu. Karibuni waungwana! Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam.
Mada nzuri. Tatizo la chama chetu ni pale tuliporuhusu wenye fedha kutumia fedha zao ku-influence maamuzi ndani ya chama, na pia kuruhusu utumishi ndani ya siasa kuwa biashara. Leo CCM si chama cha wananchi wa hali ya chini bali kundi la watu wenye mali tena ma-billion. Cha ajabu hata wanaoingia kwenye madaraka kupitia CCM wakiwa maskini baada ya muda wanakuwa matajiri. Hii ndiyo CCM yetu ya leo. Kuwa waziri au naibu waziri ndani ya serikali ya CCM ni kama kuokota jiwe la dhahabu.