Msaada: Namtafuta Jane

muongozaji

JF-Expert Member
Joined
Oct 9, 2009
Posts
1,386
Reaction score
1,002
WanaJF, heshima kwenu. Naamini weekend inaenda vizuri.

Nimekuja kwenu na ombi moja. Namtafuta dada anayeitwa Jane. Jina lake la pili nadhani ni Ossoro (Jane Ossoro!).

Mara ya mwisho kupotezana na huyu dada ilikuwa mwaka 2001. Tulionana pale maeneo ya Chuo cha Afya na Tiba Muhimbili, Dar es salaam, aliponitembelea kama shemeji yake kwa mpenzi wake ambaye wakati huo alikuwa amehamia/amesafiri kwenda Marekani na kumuacha Jane Tanzania.

Baada ya hapo hatukuweza kuonana au kuwasiliana tena kutokana na changamoto za kimawasiliano zilizokuwepo kipindi hicho. Point muhimu ni kwamba kati ya mwaka 2000 na 2001 huyu Jane alikuwa akisoma Korogwe Girls, yeye akiwa form 5 au 6. I think alikuwa akisoma mchepuo wa arts.

Bila shaka hapa jukwaani kutakuwa na cohort ya wadada waliopita Korogwe Girls (iliyopo Korogwe, Tanga) between mwaka 1999 na 2002.

Nimejaribu kumtafuta kwa njia nyingine kwa muda mrefu but imeshindikana. Nafikiri njia hii inaweza kunisaidia kuwasiliana na kumjulia hali Jane.

Najua she was kinda heartbroken kutokana na yaliyotokea kati yake na rafiki yangu (boy friend wake), and kwasasa I just really wanna know how she is doing. Alikuwa a great shemeji na rafiki pia. Maisha yana mambo mengi na inabidi yaendelee.

Naomba kama Jane mwenyewe yuko hapa JF au mtu yeyote yule mwenye details zake regarding her whereabouts tafadhali aje PM.

Nitafurahi sana kupata taarifa zozote kuhusu yeye. Natanguliza shukurani kwenu. Blessings!
 
Daah, comments za wadau ni very interesting! Tusisahau hili sio jukwaa la mapenzi wakuu. Halafu tangu 2001 mpaka leo mtu unawezaje kuwa na wazo la mapenzi? Tena kwa mtu ambaye hamjawahi kuwa na uhusiano wenye muelekeo huo?? Watu wana mawazo aisee. Hata hivyo nayaheshimu! Well, ndio diversity yenyewe hiyo iliyoko JF.
 
Imagine Kama ameolewa na mume wake akapita hapa huoni Kama utamsababishia maswali? Kama ni mume wangu lazima atanitoa macho
 
Imagine Kama ameolewa na mume wake akapita hapa huoni Kama utamsababishia maswali? Kama ni mume wangu lazima atanitoa macho
Aaah Meeyah. Then hiyo itamaanisha kuwa huyo mumeo atakuwa na shida nyingine na wewe. Alikuwa hakuamini au alishakuchoka in the first place. Sio kwasababu ya kuuliziwa na mtu mwingine tena bila nia yoyote ovu! Hii meseji yangu iko very clear. Namtafuta kama ndugu na rafiki tu. Ana maisha yake, ni vizuri tuyaheshimu. Kwa taarifa yako ni dada tulikuwa tunaheshimiana sana. Pia ni dada alikuwa anajiheshimu mno. Vitu vingi sikuviandika kwenye hii thread kwasababu nilihofia kuwa kuna watu watafanya spinning badala ya kuwa positive!
 
Naona unataka kuchangamkia fursa baada ya kuchana na rafiki yako
Aisee!!! Hapana. Hayo ni mawazo yako binafsi mkuu. Siwezi kuku-judge though. Kimsingi ni kwamba hilo sio lengo langu na haiwezekani kabisa. Haingewezekana hata kama ingekuwa kwa kipindi kile. Naamini utakuwa umenielewa mkuu!
 
Aisee!!! Hapana. Hayo ni mawazo yako binafsi mkuu. Siwezi kuku-judge though. Kimsingi ni kwamba hilo sio lengo langu na haiwezekani kabisa. Haingewezekana hata kama ingekuwa kwa kipindi kile. Naamini utakuwa umenielewa mkuu!
Mke wa mtu unamtafuta wazi wazi hivyo? Mumewe yupo humu
 
Umemtaja Jane Ossoro,si na wewe ungeandika jina lako?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…