A.alaykum wadau wenzangu wa forum hii,
Binafsi roho inaniuma saana pale navyoona wadau wakitapeliwa na wangine bila kufahamu kuwa wanatapeliwa
Nilikua muhanga wa kutokua na ajira kwa mwaka 1 tangu nilipo graduate ila nilipata wakati mgumu sana wakati
nasaka ajira ila shukran kwa hapo!!
Lengo la kuanzisha uzi huu ili uwe msaada kwa vijana wenzangu sababu mimi pia nilikua mhanga ila kwa wale walio
maliza vyuo hii July au August wengi bado ni wageni katika harakati za kusaka ajira na kupata reliable source hivyo
wengi wao huishia kutapeliwa katika hiki kipindi cha mpito napenda kuweka baadhi ya maangalizo wakati unaomba
ajira sehemu au unapoliona tangazo la kazi pia hata kutumiwa na best ako!!
Angalizo
kuwemakini wadau fanya research ya tangazo la kazi kwanza kabla ya ku apply zingatia haya;
1. Address zake zinapatikana? ingia mtandaoni/google na search hio web au address yao hapo ndio utaona kweli ipo au la sababu hio taasisi inataka kukulipa 1.7 milion itashindwa vipi kuwa na web ya shilingi laki 3??!! uta search huipati
2. Angalia jinsi tangazo lilivyo andikwa wote wajanja hapa ila tunapishana uweledi tu sasa fix huwa zinajulikana na tu be smart and reasonable usiwe novice thinker
3. Ogopa sana hizi
recruit@hotmail.com au
hr@yahoo.com najua yapo mashirika yanatumia address hizo ila kuwa makini
4. Short deadlines since advert imetoka hii inataka kukutoa attention ili ujione soon utapata kazi
5. Attachments matapeli wangine hawataki kabisa vyeti au Cv wanataka barua tu
6. Certification charges wangine wanataka vyeti viwe certified hili sio tatizo ila shida inakuja pale upeleke viwe certified na mtajwa au mhusika wao tu hapo ujue manyoya
Nadhan itakuwa njema saana hii post ikawa sticky ili wanufaike na wangine wataokuja
Na watakia kila la kheri wasaka ajira mtatoboa tu soon kikubwa jipangeni vizuri wakati wa usahili pia ujue jinsi ya kujiuza na kuwa confident
Wa salaam!!
--------------------------------------------
Almighty god I ask you to help me find a Woman who will guide to marriage!!!