Msaada: Mwanangu anaumwa hivi

Msaada: Mwanangu anaumwa hivi

Windhoek

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2016
Posts
478
Reaction score
838
Habari za jioni wakuu

Ninaandika hapa nikiwa sina amani kabisa. Mwanangu wa kike miaka 7 anaumwa ugonjwa unaotutisha. Usiku akiwa amelala kuna muda anakoroma sana tena kwa muda mrefu.

Yaani anakuwa ni kama kuna kitu zaidi ya kusinzia kwa kawaida. Akiwa katika hali hiyo hata ukimuamsha vipi haamki. Hata ukimtingisha vipi haamki yaani hata ufanye nini. Baada ya muda kama lisaa au masaa mawili ile hali inaisha anakuwa anatokwa na jasho sana. Ilianza kidogo kidogo ila sasa hali inazidi kuongezeka.

Amekuwa akisumbuliwa zaidi na ule ugonjwa wa kubanwa kifua sijui ndio Limonia. Amekuwa akipewa matibabu anapata nafuu (anapona). Na ana muda yuko vizuri.

Kama kuna mtu anayejua unaweza kuwa ugonjwa gani au tatizo gani naombeni ushauri ndugu zangu, nipo kwenye wakato mgumu.

Natanguliza shukrani
 
Kwanza umeenda hospitali...

Mwisho kabla ya kulala kumbuka kusali na pindi akiwa kwenye hiyo hali mwombe au kama unashindwa tafuta mtumishi amwombee.
 
Usichelewa bro huyo mpeleke hospital uwo ugonjwa naujua ila sitaki kusema apa mbele ya kanamdasi ila huwa inahusiana na ubongo kuna kitu huwa kitokea kwenye ubongo so kuna dawa utapewa
 
Acha kumsikilizia mtoto aisee
Kama financially hauko vizuri omba ila sio kumuangalia tu mkuu

Hata ikugharimu vyote tafadhali mpeleke kwa specialists wamuangalie
 
mpeleke hospital haraka licha ya kuwa hospital za government siziamini ila harakisha
 
Wahi hospital mkuu wangu napenda sana watoto naomba Nenda hospital kaone specialist wa watoto mkuu wangu ...nitashukuru kama binti atapata matibabu ..Kila la kheri mkuu
Wewe ni Mimi Mkuu....
Sipendi kuona Mtoto akiumwa jamani..
Huwa naumia....
 
Mpeleke Hospitali Mkuu.

Mtoto akiumwa huwa ni Complications sana.

Unaweza kudhania hiyo shida inatokana na ulivyosema ila Ikawa vingine..

Na hiyo kulala akiwa anakoroma, anamwamsha haamki siyo hali nzuri...

Pole Mkuu....Mpeleke Mtoto Hospitali haraka..
 
Habari za jioni wakuu

Ninaandika hapa nikiwa sina amani kabisa. Mwanangu wa kike miaka 7 anaumwa ugonjwa unaotutisha. Usiku akiwa amelala kuna muda anakoroma sana tena kwa muda mrefu...
Pole sana ndugu yangu, huko si kusinzia bali huyo ana kifafa mtu mwenye kifafa akidhirai huwa anapumua kwa nguvu sana ndugu yangu, vipi lakin hiyo hali haijawah kumkuta wakati wa mchana?

Mwepushe sana asiwe analala kifudifudi ili ikitokea asije lalia pua

Hii hali huwa ni mawasiliano ya umeme kwenye ubongo yanakata. Kuna wengine huwa wanatumia vidonge ili kupunguza hiyo ghasia inakuwa dozi ya maisha

Pole sana ndugu mpambanie mtoto kwa kumtafutia tiba iwe hospital au kokote we tafuta tiba ya mtoto daa pole sana ndugu mungu akupambanie uweze kupata tiba ya mtoto
 
Pole sana ndugu yangu, huko si kusinzia bali huyo ana kifafa mtu mwenye kifafa akidhirai huwa anapumua kwa nguvu sana ndugu yangu, vipi lakin hiyo hali haijawah kumkuta wakati wa mchana?

Mwepushe sana asiwe analala kifudifudi ili ikitokea asije lalia pua

Hii hali huwa ni mawasiliano ya umeme kwenye ubongo yanakata. Kuna wengine huwa wanatumia vidonge ili kupunguza hiyo ghasia inakuwa dozi ya maisha

Pole sana ndugu mpambanie mtoto kwa kumtafutia tiba iwe hospital au kokote we tafuta tiba ya mtoto daa pole sana ndugu mungu akupambanie uweze kupata tiba ya mtoto
Asante sana mkuu. Haijawahi kumtokea mchana au hata usiku akiwa hajalala. Mchana yuko kawaida tu na afya yake. Anaenda shule na anacheza na wenzake kama kawaidia
 
Back
Top Bottom