Msaada: Mke wangu Maziwa hayatoki

Msaada: Mke wangu Maziwa hayatoki

hp4510

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2012
Posts
8,230
Reaction score
8,522
Wakuu habari za majukumu mke wangu amejifungua ila tatizo ni kuwa maziwa hayatoki kabisa je ni dawa gani anaweza kutumia?
 
Mama ajitahidi zaidi kula. Lishe ya uhakika kwa mama ni muhimu.
Aendelee kumpa mtoto ziwa hata kama maziwa hayatoki. Mtoto akivyonza, husaidia ku-stimulate maziwa kutoka.

Mama wa mtoto anapewa chakula gani?
 
Je, miguu nayo inavimba?! Anza na uji wa pilipili manga kama wadau hapo juu walivyopendekeza. Pia Wapare wana uji unaitwa "Idundi" yaani uji unga wa mhogo mixed na mtindi. Uwe mwepesi kimtindo na unywewe ukiwa wa moto. Ni dawa nayo. Yasipotoka hapo leta feedback twende extra mile mpaka yatoke. Hatuna mzaha na afya za wenetu!
 
Ajitahidi kunywa uji wa pilipili manga kwa wingi,apate lishe nzur,ayamwagie maji yamoto kiasi wakat wa kuoga. Hayo nilikua nayafanya mimi maziwa yalikua yanamwagika yenyewe.
 
Suluhisho ni mbegu za maboga (tetele)zinapatikana sana Mbeya na Iringa
 
Je, miguu nayo inavimba?! Anza na uji wa pilipili manga kama wadau hapo juu walivyopendekeza. Pia Wapare wana uji unaitwa "Idundi" yaani uji unga wa mhogo mixed na mtindi. Uwe mwepesi kimtindo na unywewe ukiwa wa moto. Ni dawa nayo. Yasipotoka hapo leta feedback twende extra mile mpaka yatoke. Hatuna mzaha na afya za wenetu!
bade hayatoki mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom