Auz
JF-Expert Member
- Apr 6, 2016
- 13,190
- 10,918
Kama wewe ndio unayeongoza mada, nini kinakukatisha tamaa wakati hadhira itakuwa inakusikiliza? Ingekuwa mtu mwingine anaongea, hapo ungekuwa na wasiwasi wa uwezekano wa kutomsikia vizuri.Nina tatizo la usikivu kidogo yaani sauti inachelewa kufika ..
Japo darasani niliko resit mtihani watu huwa wananidharau na kuniona mjinga lakini kiukweli nafaulu kuliko wengi wao..
Inafikia hatua napachukia na nachukia kukaa na watu wengi naona nikae peke yangu hasa hii Open school inapokuwa muda umeisha ndo natulia najisomea kwa amani.
Leo kulikuwa na presentation lakini nilipochaguliwa kwenda ku present kabla hata sijaenda watu wananicheka, nilivunjika moyo sana..
Kiukweli nilikuwa nimeandaa presentation nzuri sana na niliumiza kichwa. Lakini matatizo yamekuwa sehemu ya watu kunifanyia mzaha.
Inavunja moyo kwa kweli naona niache tu na mtihani nisifanye..
Nisaidieni kabla sijachukua maamuzi haya.
Jiamini, na hakikisha unamaliza masomo yako.