NALO LITAPITA
JF-Expert Member
- Aug 25, 2011
- 333
- 90
Wakuu mimi ni graduate, wakati fulani nilileta hapa uzi nikiomba ushauri juu ya kuanzisha huduma za mpesa, tigopesa na airtel money. Ki ukweli nilinufaika sana na michango yenu. Naomba mnisaidie kuhusu mashine au huduma ya max malipo, kuna mdau aliniambia ukiwa nayo hii huna haja ya kutafuta zile line za uwakala ambzo baadhi yake mfano tigo hawatoi. Je ni kweli kuwa ukiwa na hii mashine ya Max malipo unaweza kutoa huduma a mpesa, tigopesa na airtel money bila kuhitaji line za uwakala? Na pia ukiacha malipo kwa ajili ya LUKU na DSTV ni malipo gani mengine mtu aweza fanya kupitia Max Malipo? Mwisho naomba aliyewahi kufanya biashara kupitia mashine hizi au ambae yuko kariibu na mtu anayefanya biashara hii anisaidie kunifafanulia jinsi mtu unavyoweza kunufaika na kuwa agent wa Max Malipo. Nisaidien wakuu walau nipate kitu cha kujishughulisha nacho.