Msaada kuhusu dawa za Wakorea

Msaada kuhusu dawa za Wakorea

Kacharimbe

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2011
Posts
216
Reaction score
35
Heshima wakuu,

naomba kupata uzoefu kuhusu matibabu ya wakorea hapa nchini. Nilikwenda kutibiwa nikaambiwa nina tezi dume (of course dalili wanazozisema zote ninazo). Wakasema nianze matibabu ya mwezi 1 kwa shs 150,000. Naomba mwenye uzoefu anifahamishe maana sijawahi kutumia dawa zao:

1. Je dawa wanazotumia ni za asili au za kitalaam (kuna mdau aliniambia wanatumia miti ya asili ya kwao).

2. Vipimo vyao vinaaminika?

Vipi kuhusu NIMR, maana walisema wanayo dawa kwa miezi 3 kwa sh 360,000

Naomba uzoefu wenu wakuu

Siku njema
 
Ulienda kutibiwa nini mpaka usiwaamini walipokuambia una tezi dume?

Je, hicho ulichotibiwa ulipimwa?
 
Wahi kalitoe hospital kabla tatizo halijawa kubwa ,huko kwa wakorea utaliwa pesa halafu utajikuta umechelewa
 
Kapime kwenye hospitali kubwa ili uweze kujua stage ya hilo Tezi dume kwanza then utaanza kutafuta matibabu yenye unafuu.
 
Ulienda kutibiwa nini mpaka usiwaamini walipokuambia una tezi dume?

Je, hicho ulichotibiwa ulipimwa?
Nilienda kutibiwa miguu kuuma, magoti, mkojo kuuma wakati wa kukojoa, na mkojo kutokuisha wote. Yaani nikikojoa kabla sijarudi kukaa, nasikia tena hasa nikiwa nimetoka kuoga
 
Nilienda kutibiwa miguu kuuma, magoti, mkojo kuuma wakati wa kukojoa, na mkojo kutokuisha wote. Yaani nikikojoa kabla sijarudi kukaa, nasikia tena hasa nikiwa nimetoka kuoga
umepona?
 
Bado kiongozi. Waliniambia wanichome sindano za magoti kila wiki 2 kwa wiki 5. Walisema ni baridi yabisi. Ndo wakaniambia pia nina tezi dume nilipie 150,000
Ndo nauliza kama dawa zao zinatambulika
 
Kapime kwenye hospitali kubwa ili uweze kujua stage ya hilo Tezi dume kwanza then utaanza kutafuta matibabu yenye unafuu.
Leo nimekwenda hospitali ya mkoa, wamesema prostate ni kubwa kama 50. Kuna dawa wamenipa, tamsulosin ambayo ni ya kutuliza tu ila wameniambia niende Muhimbili kitengo cha mkojo kwa uchunguzi zaidi
 
Bado kiongozi. Waliniambia wanichome sindano za magoti kila wiki 2 kwa wiki 5. Walisema ni baridi yabisi. Ndo wakaniambia pia nina tezi dume nilipie 150,000
Ndo nauliza kama dawa zao zinatambulika
Pole sana mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom