Wakuu heshima kwenu. Nina jambo ambalo halinizuii mi kufanya shughuli zangu kwenye simu yangu lakini huwa silipendi. Kama kawaida kukiwa na version mpya kwenye application unakuwa notified ili wewe unaziupdate.
Sasa kuna application moja nilidownload nikaanayo kwenye simu yangu kwa muda na siku moja nikapata notification kuwa niweze kuiupdate. Nikafanya hivyo. Hiyo application inatumia sauti ukitaka kusoma baadhi ya vitu na ndio iliyokuwa niiupdate. Ikaanza process ya kuupdate lakini ikawa haisogei hata kidogo kudownload ile update. Nimekaa nayo kwa muda ikiwa inaonesha kama inataka kuanza kudownload lakini haianzi. Nikaamua ku- uninstall ile application ile kitu haikutoka. Nika install tena bado iko pale pale haianzi lakini inaonekana kila wakati kwenye notification bar. Hata baada ya ku -unainstall ile application bado iko pale pale.
Msaada wa wataalamu nifanyeje ili itoke maana kila siku inaonekana inadownload lakini haianzi hata kesho.
Siku nyingine usipokee kitu ambacho huna uhakika nachi unless umesearch mwenyewe.
Kuna applicaation nyingi za spy ambazo anaweza kuituma mtu then inakuwa inapop up ili uipokee. Ukishaipokea na kuinstall either hautaiona tena au hauwezi kuifanya chochote.
Na pia app nyingi za hivo huwa zinapewa majina fake ili uingie mkenge vizuri.