Habari wana Jf, mimi naishi Morogoro wilaya ya Kilosa nimepata wazo la kufanya ufugaji wa Ng'ombe wa maziwa na kisasa
Lengo langu niwe na Ng'ombe wawili majike wa maziwa then niwe na ng'ombe wanne wa kienyeji ambao hawa watakuwa kwa ajili ya nyama na kuuza japo na maziwa kidogo.
Nahitaji kujuwa Ng'ombe gani wazuri wa Maziwa ambao wanatija?,wanapatikana wapi?, na jee bei zao zipoje?
Kuhusu ng'ombe wa kienyeji hawa hawana shaka wapo wengi kwa wamasai wanapatikana kirahisi minadani
Naombeni mnisaidie nitashukuru sana