Msaada juu ya soko la mahindi na soya

Senir

New Member
Joined
Dec 11, 2015
Posts
3
Reaction score
1
Habari wakuu,

Mimi ni kijana mpenda mabadiliko ambaye nimeamua kugeukia sekta ya kilimo na kujaribu kuwekeza humo.

Nimeanza mwaka huu kwa kupanda Mahindi na Soya kwa kilimo cha kisasa lakini bado nakuwa na maswali ya kujiuliza ninayokosa majibu maana kwa ushauri niliopewa ni kwamba nafaka inalipa zaidi kama nitapeleka Dar Es Salaam.

Maswali hayo ni :

1) Nani atakuwa mteja wangu kwa bei inayofaa?
2) Bei ya jumla kwa mazao hayo ntauzaje ili inilipe vizuri (MAHINDI na SOYA)?

Naombeni msaada wenu wakuu kwa wenye uzoefu na mambo haya mana ndo nimeanza.
 
Wenye kujua haya mambo tujuzeni
 
Wateja wapo hasa kwenye soya ingawa sijajua umelima kiasi gani. Kama uko Nyanda za juu kusini kuna Kampuni inaitwa Silverlands iko Ihemi-Iringa inanunua Soya hata kama uko na tani 500 wao wanatengenezea chakula cha kuku na bei wanayoofer ni Nzuri.

Swala la kuuza bei gani nadhani soko ndilo litakusukuma japokuwa katika kupanga bei tunaangalia gharama za kuzalisha na kisha tunaongeza asilimia ya faida
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…