Msaada jaman

Mpatuka

JF-Expert Member
Joined
Nov 15, 2015
Posts
2,333
Reaction score
3,714
Nimefanikiwa kuitwa kwenye usaili sekretarieti ya ajira tarehe 26 mwezi wa 3 mwaka 2022.

Lakini changamoto niliyonayo ni kwamba nimepoteza kitambulisho cha utaifa na hata vitambulisho vingine pia sina.

Hivyo wakuu wangu naombeni msaada wa mawazo ni hatua gani naweza kuchukua ili niweze kufanya usaili huu.

Natumaini wapo watu walishapitia changamoto kama yangu hivyo kupitia uzoefu wao wanaweza kunielekeza Jambo la kufanya na hatimae nikafanikiwa kufanya usaili.
 
Inabidi atleast uende serikali za mtaa uchukue barua ya utambulisho, pia ambatanisha na lost report labda watakufikiria maana swala la id wanatilia mkazo mno kwa macho nimeshuhudia watu wakishindwa kufanya usaili kwa kukosa kitambulisho so fanya kila unachoweza kupata evidence za kutosha
 
1.Kachukue loss report polisi (kama bado hujaichukua)
2.Je hauna soft copy au photocopy ya hiyo NIDA ID yako? Kama unayo unaweza kwenda nayo kisha ukawaonyesha wahusika kwenye interview photocopy ya NIDA ID pamoja na hiyo loss report na kuwaambia kuwa ulipoteza IDs zako mkuu.
3.Kama hauna soft copy wala photocopy ya NIDA ID yako, eKuna namba unaweza ukatuma meseji (nimeisahau), ukaandika jina lako kamili, then wanakutumia Namba yako ya NIDA, at least pia ukiwa nayo hiyo namba na loss report, unaweza kuwa convince wahusika kuwa kitambulisho chako kilipotea.
4.Lakini pia ukienda kwenye website ya NIDA i think unaweza kudownload a copy of NIDA ID yako (sina uhakika sana, ngoja niconfirm pia)... Unaandika tu majina yako kamili na namba ya simu uliyoitumia kuandikisha NIDA ID.
Pole sana mkuu, I hope mawazo yangu yatakusaidia.... Yote kwa yote, loss report niuhimu sana mkuu, get it kama bado hujaichukua.
 
Sawa mkuu nitafanya hivyo
 
Asante sana mkuu nitafanya hivyo
 
Print taarifa zako za namba ya nida uende nazo kwenye usaili ila ni bahati nasibu unaweza ukakutana na msimamizi muelewa au wakazingua
 
Natumaini umepata msaada maana nikiongezea nitaharibu
 
Wazo zuri sana mkuu

Tena ikiwezekana vile ambavyo anauwezo wakiviombea loss report aviombee
 
Print taarifa zako za namba ya nida uende nazo kwenye usaili ila ni bahati nasibu unaweza ukakutana na msimamizi muelewa au wakazingua
Kaka hakuna namna unaweza pata kitambulisho cha NIDA ofisini kwao kwa dharura kama za namna hii hata kama kuna fees uwa applicant unstakiwa kulipa.
 
Kaka hakuna namna unaweza pata kitambulisho cha NIDA ofisini kwao kwa dharura kama za namna hii hata kama kuna fees uwa applicant unstakiwa kulipa.
Mkuu chukua loss report then nenda ofisi za nida wilayani kwako watakupa kitambulisho kingine kwa malipo ya sh 20,000/

Next time Uwe unascan documents zako unahifadhi kwenye email ili kuepuka usumbufu,
 
Mkuu chukua loss report then nenda ofisi za nida wilayani kwako watakupa kitambulisho kingine kwa malipo ya sh 20,000/

Next time Uwe unascan documents zako unahifadhi kwenye email ili kuepuka usumbufu,
Asante sana kaka
 
Mkuu umeitwa kada gani kule... Mbona safari hii hawajaspecify reason kama mtu hajaitwa Usaili..?
 
Ww kwenye account yako ushawekewa namba ya mtihani..?
 
Bado mkuu sijawekewa mpaka sasa but nahisi kuanzia j3 wataweka tu
Duuuh,, utumishi wanachofanya sio fine kabisa kwanini tusiitane Interview tukafeli wenyewe.. Sio poa kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…