Salaam Wadau,
Naomba msaada wenu juu ya taratibu na Gharama za Kupata Building Permit ya Ghorofa 1 kwa ajili ya makazi, eneo la Kibada, Kigamboni.
Kiwanja ni cha mradi (Kimepimwa),
Pia Ramani zote mbili (kawaida+Civil) ninazo.
Shukrani
Mkuu kwanza pata michoro (both Architectural and structural) na iwe imegongwa mihuri ya registered engineer (kwa structural drawings). Kisha nenda nayo pale Temeke manispaa. Gharama yake haizidi shilingi za kitanzania elfu arobaini na tano tu. Ila kama kuna vikorombwezo vingine mfano, ukuta (fence), servant quarter n.k gharama zinaongezeka kidogo. Hawa jamaa hufanya vikao vyao mara moja kwa kila miezi miatatu kutoa vibali isipokuwa kama kuna dharura ambapo mwombaji inabidi alipe kama milioni 2. Kwahiyo fanya mapema waweza kubahatisha ukakuta kikao kiko karibu kufanyika.
mmhh kaazi kweli kweli...but mbona huwa tunapita pita mitaanai tunaona watu wanatupia magorofa yao na hata hamna vibao nje kuonyesha kama wana building permit au nn??
Kuna jamaa yangu juzi walimpiga laki nane, but alitumia lawyer wake binafsi kushughulikia