Msaada: Biashara ya duka la madawa Muhimu

Msaada: Biashara ya duka la madawa Muhimu

Wangda

New Member
Joined
Sep 9, 2021
Posts
2
Reaction score
1
Kama kichwa hapo naomba kufahamu jinsi ya kuendesha biashara/huduma ya duka la dawa muhimu kubwa zaidi ni kuhusu mtaji wa sh ngapi naweza anza nao, na taratibu zake zikoje natanguliza shukrani.
 
Najaribu! unatakiwa uwe na chumba kikubwa chenye partion mbili,moja inakuwa kama store ya dawa...sakafu ya tiles na makabati ya aluminium,haya hayabebi uchafu sana na rahisi kusafisha..Kutoka kwenye duka lako hakikisha hakuna duka lingine umbali wa chini ya mita 300..ukishapata eneo lako la biashara nenda kamuone mfamasia wa wilaya atakuja na timu yake kukagua kisha utapewa go ahead..Utahitaji leseni ya biashara na kibali kutoka TFDA ambayo ni mamlaka ya chakula na dawa...Mtaji inategemea na ukubwa wa duka unalotaka,kuanzia milioni 2 unaweza pata dawa za kuanzia hiyo ni nje ya gharama jengo,makabati,na process ya vibali
 
Back
Top Bottom