Lucchese DeCavalcante
JF-Expert Member
- Jan 10, 2009
- 5,471
- 734
Kila mwaka aliyekuwa mnajimu na mtabiri maarufu Afrika Mashariki na Kati, Sheikh Yahya Hussein alikuwa akifanya utabiri. Mwaka huu Januari 13, mrithi wa kazi zake Maalim Hassan Yahya Hussein amechukua nafasi yake.
Mwaka huu wa 2012 umeanzia siku ya Jumapili, siku hii inatawaliwa na Sayari ya Jua ambayo nyota yake ni moja tu nayo ni nyota ya Simba.
Sayari hii inahusika na, kufanyiana kiburi, kutumia nguvu, ufahari, mambo yote yanayohusiana na Siasa, udereva, ufundi wa mambo ya moto na magari
Tarehe 20/5/2012 ambayo pia itakuwa siku ya Jumapili Jua litapatwa kiasi (Partial Eclipse) kwa mara ya kwanza na kupatwa huku kwa jua kutaonekana kwa upana wa kati ya kilometa 240 na 300 na sehemu zitakazohusika ni Asia Mashariki, Kaskazini mwa bahari ya Pacific na Magharibi ya Marekani.
Tokyo (Japani) ambayo iko kilometa 10 mwa mstari wa kati itashuhudia kupatwa huku kwa dakika 5 na sekunde 26.
Mwisho wa Mwaka huu tarehe 13/11/2012 ambayo itakuwa siku ya Jumatano ambayo inatawaliwa na sayari Mercury jua litapatwa kamili (Total Eclipse) watu wanaoishi Australia na Bahari ya Pacific ndio watakaokumbwa na kiza cha kupatwa na jua.
Kwa sababu huu mwaka umeanzia na siku ya Jumapili na siku hiyo inatawaliwa na sayari ya Jua, hatari za kupatwa huku zitaikumba Dunia moja kwa moja.
Mwaka huu una namba 12 (2012) ambayo kinyota inaashiria, uadui wa kisiasa na kijamii, watu kulipizana visasi na upinzani kupata nguvu, wanyonge kudai haki zao kwa nguvu na mafanikio ya wataliwa dhidi ya watawala.
Vile vile inaashiria kutokea kwa vimbunga, kusikika sana kwa habari za Waandishi au Waandishi kupata madaraka makubwa katika siasa.
Pia ni mwaka ambao kutazuka Moto sehemu mbalimbali duniani na kuleta madhara makubwa na hiyo inaashiria kuzuka kwa magomvi baina ya viongozi wa kisiasa na wananchi.
Pamoja na hayo tutasikia habari za kutokea matetemeko ya ardhi yatakayoleta madhara makubwa, Wasanii kupata kwa kuchaguliwa au kuteuliwa kushika nafasi za kisiasa na kutokea kashfa kubwa kwa viongozi zitakazohusiana na masuala ya fedha au mambo ya ufisadi au wizi mkubwa utakaoshitua watu.
Kutokana na hayo:-
Natabiri kutokea shida kubwa za Majanga ya Asili na kuongezeka kwa maradhi au kufumuka maradhi yasiyojulikana na kuiletea Dunia wasiwasi mkubwa.
Natabiri, Uadui mkubwa kutokea kati ya viongozi wa nchi na wananchi kwa ujumla na kusababisha vita vya wenyewe kwa wenyewe na viongozi kuvuliwa madaraka.
Natabiri kutokea vifo vya Mahakimu na Majaji na Wanasheria maarufu katika nchi za Mashariki, Tanzania ikiwemo
Natabiri kutokea vifo vya Mawaziri na Wizara zao kupatwa na matatizo.
Natabiri Kutokea kwa Njaa kali kutokana na Jua kuwa kali na ukame kukumba nchi.
Natabiri tutasikika habari za wanawake kuuwa waume zao na watumishi kuwauwa mabwana wanaowafanyia kazi.
Natabiri Mwaka huu ni mwaka ambao utatawaliwa na vifo vitakavyoshtua watu wengi.
Natabiri: Huu ni mwaka wa vijana kushika nafasi za uongozi na kuchukua madaraka na wazee wengi watapoteza nafasi zako hasa katika chaguzi mbali mbali zitazofanyika.
Natabiri malumbano makubwa, vurugu na magomvi kwenye mabunge, wabunge watagombana bila kujali itikadi za vyama vyao.
Natabiri mivutano iliyopo hivi sasa katika vyama haitaharibu vyama husika hasa katika vyama vya CUF,NCCR na CCM.
Natabiri: Kutokea vifo vya ghafla kwa viongozi wa kisiasa waliopo madarakani au Serikalini.
Nashauri:- Serikali iwe makini katika utekelezaji wa shughuli zake kwa sababu kunaweza kuzuka mgogoro mkubwa utakaotikisa nchi.
Natabiri, Rais Jakaya Kikwete kupata umaarufu mkubwa wa kisiasa mwaka huu na atashirikisha wapinzani katika shughuli kadhaa za kiserikali hivyo nyota yake kuzidi kung'aa kitaifa.
Natabiribaadhi ya viongozi wa dini kukumbwa na kashfa mbaya na za kutisha zitakazovunja hadhi zao.
Maalim Hassan Yahya Hussein
Sayari hii inahusika na, kufanyiana kiburi, kutumia nguvu, ufahari, mambo yote yanayohusiana na Siasa, udereva, ufundi wa mambo ya moto na magari
Tarehe 20/5/2012 ambayo pia itakuwa siku ya Jumapili Jua litapatwa kiasi (Partial Eclipse) kwa mara ya kwanza na kupatwa huku kwa jua kutaonekana kwa upana wa kati ya kilometa 240 na 300 na sehemu zitakazohusika ni Asia Mashariki, Kaskazini mwa bahari ya Pacific na Magharibi ya Marekani.
Tokyo (Japani) ambayo iko kilometa 10 mwa mstari wa kati itashuhudia kupatwa huku kwa dakika 5 na sekunde 26.
Mwisho wa Mwaka huu tarehe 13/11/2012 ambayo itakuwa siku ya Jumatano ambayo inatawaliwa na sayari Mercury jua litapatwa kamili (Total Eclipse) watu wanaoishi Australia na Bahari ya Pacific ndio watakaokumbwa na kiza cha kupatwa na jua.
Kwa sababu huu mwaka umeanzia na siku ya Jumapili na siku hiyo inatawaliwa na sayari ya Jua, hatari za kupatwa huku zitaikumba Dunia moja kwa moja.
Mwaka huu una namba 12 (2012) ambayo kinyota inaashiria, uadui wa kisiasa na kijamii, watu kulipizana visasi na upinzani kupata nguvu, wanyonge kudai haki zao kwa nguvu na mafanikio ya wataliwa dhidi ya watawala.
Vile vile inaashiria kutokea kwa vimbunga, kusikika sana kwa habari za Waandishi au Waandishi kupata madaraka makubwa katika siasa.
Pia ni mwaka ambao kutazuka Moto sehemu mbalimbali duniani na kuleta madhara makubwa na hiyo inaashiria kuzuka kwa magomvi baina ya viongozi wa kisiasa na wananchi.
Pamoja na hayo tutasikia habari za kutokea matetemeko ya ardhi yatakayoleta madhara makubwa, Wasanii kupata kwa kuchaguliwa au kuteuliwa kushika nafasi za kisiasa na kutokea kashfa kubwa kwa viongozi zitakazohusiana na masuala ya fedha au mambo ya ufisadi au wizi mkubwa utakaoshitua watu.
Kutokana na hayo:-
Natabiri kutokea shida kubwa za Majanga ya Asili na kuongezeka kwa maradhi au kufumuka maradhi yasiyojulikana na kuiletea Dunia wasiwasi mkubwa.
Natabiri, Uadui mkubwa kutokea kati ya viongozi wa nchi na wananchi kwa ujumla na kusababisha vita vya wenyewe kwa wenyewe na viongozi kuvuliwa madaraka.
Natabiri kutokea vifo vya Mahakimu na Majaji na Wanasheria maarufu katika nchi za Mashariki, Tanzania ikiwemo
Natabiri kutokea vifo vya Mawaziri na Wizara zao kupatwa na matatizo.
Natabiri Kutokea kwa Njaa kali kutokana na Jua kuwa kali na ukame kukumba nchi.
Natabiri tutasikika habari za wanawake kuuwa waume zao na watumishi kuwauwa mabwana wanaowafanyia kazi.
Natabiri Mwaka huu ni mwaka ambao utatawaliwa na vifo vitakavyoshtua watu wengi.
Natabiri: Huu ni mwaka wa vijana kushika nafasi za uongozi na kuchukua madaraka na wazee wengi watapoteza nafasi zako hasa katika chaguzi mbali mbali zitazofanyika.
Natabiri malumbano makubwa, vurugu na magomvi kwenye mabunge, wabunge watagombana bila kujali itikadi za vyama vyao.
Natabiri mivutano iliyopo hivi sasa katika vyama haitaharibu vyama husika hasa katika vyama vya CUF,NCCR na CCM.
Natabiri: Kutokea vifo vya ghafla kwa viongozi wa kisiasa waliopo madarakani au Serikalini.
Nashauri:- Serikali iwe makini katika utekelezaji wa shughuli zake kwa sababu kunaweza kuzuka mgogoro mkubwa utakaotikisa nchi.
Natabiri, Rais Jakaya Kikwete kupata umaarufu mkubwa wa kisiasa mwaka huu na atashirikisha wapinzani katika shughuli kadhaa za kiserikali hivyo nyota yake kuzidi kung'aa kitaifa.
Natabiribaadhi ya viongozi wa dini kukumbwa na kashfa mbaya na za kutisha zitakazovunja hadhi zao.
Maalim Hassan Yahya Hussein