Ngoja kijana amwage radhi kwanza. Utasikia moto wake baada ya hapo. Vijana wamechoka na ubabaishaji huu. Utamsikia tu Nape, na wengine wengi saaana sasa watajitokeza hadharani.
Thanx, tujuze mkuu... But al n al bora atangaze kuhama tu... Atue cdm tupge kazi
Kama kweli UVCCM wanakitakia mema Chama chao na nchi kwa ujumla, basi wajitokeze na kutamka hadharani kuwa hawakubaliani na Ufisadi. Baada ya hapo wawataje Mafisadi hao kwa majina na nafasi zao ktk Chama, na kuwataka waondoke ktk Chama ili watu wafanye kazi za kujenga nchi badala ya kutumia muda mwingi kuchekea "upumbavu" ndani ya Chama.
Tualitaka hili lifanyike pia kwa CCM wenyewe. Kwanini munaoneana haya wakati munaangamia? Munategemea nini? Yaani Chama na nchi viangamie kwa sababu ya watu wachache saaana? Nani kasema maneno hayo? Wakati wa mageuzi ndani ya CCM ni sasa.
Mara ya kwanza nilidhani viongozi wa vyama vya upinzani wangeishinikiza Serikali iwapeleke Mafisadi ktk mkono wa sheria, lakini kwa mshangao nikasikia kuwa nao wameishanunuliwa. Nilipofuatilia kwa ukaribu nyendo zao nikakubaliana na aliyeniambia kuwa wamenunuliwa, kwani kila ukisikia wanakemea Ufisadi basi wao humtaja Rais Kikwete huku wakijua wazi kuwa wanaolitafuna Taifa hili ni akina nani.
Kama kweli wanawatetea watanzania basi wajitokeze kwa staili yao ile ile wawabomoe Mafisadi kama alivyofanya Reginald Mengi. Bila ya kufanya hivyo, basi tutaendelea kuamini kuwa mumenunuliwa na Mafisadi kama inavyofahamika huku mitaani.
Hili la kununuliwa na ukimya wa wapinzani na mimi sasa linaanza kuniingia na staili hii ya kizamani ya kipolisi ya kulinda ubungo na huku wakijua ujambazi utafanyikia magomeni sasa inatuonyesha kwamba kuna jambo. Hawa hawana ujasiri wakusema wazi kwamba mafisadi ni kina nani kwa vile wanajua kwamba kuna mshiko ambao baadhi yao wanaupokea kutoka kwa mafisadi ili kukaa kimya na kuuyumbisha ufisadi. Matokea yake wako bize kumtukana Rais wetu ambaye hana hata doa la ufisadi. Hao hao mafisadi sasa ndiyo wanashirikiana nao kutoa majarida ya kuwasafisha na hata kutumia magazeti yao kuwasafishia njia ya kuelekea ikulu na wakati huo huo kuwachafua walio wasafi. Nashangaa walivyokaa kimya pale tuhuma za Dr. Mwakyembe kuuawa na wakijua kwamba hata Dr. Slaa naye yumo kwenye orodha. Hawa hawa ndiyo wanaruhusu magazeti yao yamdhihaki mzee Mengi katika kesi yake iliyofunguliwa na mafisadi pale alipoujulisha umma viwavi jeshi wa uchumi wao.
Mimi nasema Ulega, Makonda, Gambo na wengine ni watu ambao nchi hii inastahili kuwaenzi kwa kufanya lile ambalo hao wanaopata ruzuku wameshindwa kulifanya. Wameamua ku-bite the bullet kwa manufaa ya wote halafu watakaoamua kuzunguka kuleta porojo tena kwa hela za mafisadi waendelee kuulea ufisadi wa kweli.
Post yako nimeikubali mkuu.
Siku zote mie naamini hivo kuwa zengwe lianzishiwe mlemle ndani ya CCM na wanamageuzi wakamate madaraka ndani ya chama, lakini viongozi wa upinzani hawawezi kulikubali hilo kwani nao wamejimega kule kutaka kusaka madaraka, sasa ukileta point hii unawakera sana japo ni ukweli wa kuleta maendeleo ya kitaifa zaidi.
Chadema ya sasa iko imara na imejitosheleza. Hatutaki tena mazagazaga yaliyonyimwa fursa ya kufisadi ndani ya ccm.
Tumeona kupitia Shibuda kwamba it if difficult to unlearn the ccm culture and behavior. Tumeona pia kupitia makamanda wapya wa Chadema bungeni kwamba upya hauna ufisadi na tamaa kama wazoefu
Hayo yote amekuwa akiyajua siku zote kabla na baada ya kujiunga na CCM. Mrisho, usiwe mnafiki na kutaka huruma ya wananchi. Kama hujatendewa haki kwa nini usitumie ngazi za chama? Unalalamika wenzako wamekimbilia kwenye vyombo vya habari, ni vyombo hivyo hivyo unatumia. Umekata rufaa? Umelalamikia hatua hiyo? Kwa nini kama umeshachukua hatua unakimbilia vyombo vya habari? Je uongozi wa juu ukibariki maamuzi ya mkoa? Subira yako iko wapi?
Acheni kutumika, nyinyi ndio mnaiua hii nchi kwa njaa na sifa zenu. Kama mtu ana mtoto wa chuo kikuu halafu bado ni kijana unatuambia sisi tufanye nini? Leo ndio mmejua?
Hivi kwani mtu hawezi kuwa mpambanaji mpaka atoke ndani ya ccm? Mi sikubaliani na wote wanaotaka wanaopambana na ufisadi watoke ccm kwanza.
Wako wapi kina Mpendazoe, Mrema nk? Wote wamechemsha baada ya kuhama CCM.
Mpambano ni lazima uwe ndani ya chama ili kuwang'oa wezi wa nchi hii. Nashauri wapiganaji wote wasihame CCM ila wawe makini na michezo michafu inayofanyika ndani ya CCM.
"msiwaachie nguruwe wale shambani peke yao"
sikubaliani na mawazo yako ndugu yangu! Chama huwa kinajivunia idadi ya wanachama. Na kuwa mwanachama lazima uwe unafanana nao kiitikadi, mtazamo na kimsimamo. Ndio maana mi naona kama Mrisho ametofauthana na wenzake na amefanana na cdm arudi arusha tumpe kadi tufanye kazi. Huku hatufanyi kazi kwa nguvu ya chama. Its people's power!
Hapo kwenye RED ndio pananipa mwashawashaYule Kada wa CCM kupitia UVCCM aliyeanzisha sakata la akina EL na RA ataongea na wandishi wa habari leo saa nne asubuhi, hapa Dar es Salaam.
CHINI NI TAMKO LAKE FULL TEXT
=======================
Ndugu zangu wahariri na waandishi wa vyombo vya habari, nimeona leo nikutane nanyi ili niweze kufafanua mambo machache maana mmekuwa mkinipigia simu sana pamoja na kuniandikia ujumbe wa maandishi kwa lengo la kutaka kupata maoni yangu kuhusu maazimio ya baraza la vijana la mkoa wa Arusha na yalio andikwa kwenye magazeti kabla ya baraza hilo na baada ya baraza hilo. Kwa kuwa yaliondikwa yamegusa utu wangu na kwa kweli nisingeweza kukutana na mtu mmommoja ili kuelezea hali halisi hivyo nikaona tukutane sote hapa ili tujuzane sote pamoja na kuweka historia sawa.TAARIFA YA NDUGU MRISHO GAMBO KWA VYOMBO VYA HABARI
JUMAPILI TAREHE 3 APRILI 2011
Kwenye baraza la vijana la UVCCM mkoa wa Arusha kama sote tulivyo ona kwenye vyombo vya habari maana walitangaza kwenye vyombo vya habari kuwa wamenivua uongozi wa vijana ndani ya UVCCM, japokuwa hadi leo hawajaniandikia barua kuhusu jambo hili, na wakaamua kupeleka kwenye vyombo vya habari taarifa hii kabla hata ya kuniita na kunihoji kama taratibu zilivyo kwenye chama chetu. Jambo hili lingeishia kwenye baraza na uongozi wa Mkoa ukaniandikia barua kimya kimya wala nisingekuwa na haja ya kuja kuzungumza na waandishi wa habari huku ukizingatia kuwa hawana mamlaka hayo ya kunivua uongozi .
Kabla ya kikao hicho cha baraza la Arusha nilipata taarifa mbalimbali kuwa kuna kikundi cha watu kinafanya vikao ili kuhakikisha kuwa ninavuliwa uongozi kutokana na yaliyo andikwa kwenye magazeti kuwa Kashfa za Richmond na Dowans zimechangia sana kukipotezea mvuto chama chetu cha Mapinduzi na inaonekana tija kwa wahusika kuwajibishwa kama sehemu ya kujivua gamba kwa chama chetu. Mimi niliwajibu kuwa kama wanachosema ni kweli chochote watakachopewa wachukue kwa kuwa Mungu ameamua kunifanya daraja la wao kurudishiwa kodi zao.
Pia nataka kuwakumbusha kitu kimoja kuwa agenda za hali ya kisiasa na tathmini ya uchaguzi zilisha fanyika kwa ngazi ya Jumuiya na chama mikoani na wala hapakuwa na malalamiko yoyote kuhusu mimi. Agenda hizi pia zilijadiliwa kwenye baraza la vijana la CCM Taifa hivi karibuni ambapo pamoja na mambo mengine lilipitia taarifa zote za tathmini kutoka mikoani huku Mkoa wa Arusha ukiwa ni miongono mwao. Chakushangaza kwenye tamko lao baraza la uvccm mkoa wa Arusha wakairudia agenda ya hali ya kisiasa na tathmini ya uchaguzi ili hali tayari taarifa yao ilishapelekwa kwenye vikao vya juu bila mimi kulalamikiwa chochote. Hii ni ishara tosha kuwa ilikuwa ni njama maalum.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari na nakala ya tamko la uvccm mkoa wa Arusha kumesemwa kuwa wametangaza kunisimamisha uongozi kwa kuwa sikumpigia kura na nimemsema vibaya Dada yangu mpendwa Batrida Burhani. Kwa mtu yeyote mwenye akili timamu anajua kuwa kura ni siri na ni haki ya mtu ya kikatiba, hakuna mtu yeyote mwenye mamlaka ya kuhoji namna mtu anavyo tumia haki yake ya kupiga kura. Hili ni wazo dhaifu na halina tija kwa wao walio litoa na hasa kwa vijana wa Tanzania ambao wana changamoto nyingi kama vile ajira na matatizo ya bodi ya mikopo. Kwa mtazamo wangu binafsi kama wanafanya kazi hii kwa kutumwa na mtu yeyote basi wajue kuwa kazi wanayo mfanyia mtu huyo ni sawa na kupiga rangi upepo.
Watanzania wa leo ni watanzania wa Dot com na si wa BBC (Born before computer), kwa kuwa wana uwezo wa kupata taarifa mapema. Tamko la baraza la vijana mkoa wa Arusha lilitumwa kwa waandishi wa habari kabla hata ya kikao cha baraza kuisha. Ushahidi ninao wa kutosha, ikiwa ni pamoja na maoni ya baadhi ya wajumbe wa baraza wakiwataja watu walio husika na mpango huo. Miongoni mwao ni mjumbe mmoja wa baraza la mkoa kuwakilisha vijana kwenye mkutano mkuu wa CCM Taifa ambaye ana mtoto anae soma chuo kikuu huku bado akijiita kuwa na umri wa ujana kwa maana ya chini ya miaka 30 kwa taratibu za jumuia yetu.
Nimesikitishwa sana na tamko la baraza la vijana mkoa wa Arusha kulifanya tamko la vijana wa mkoa wa pwani kama sehemu ya azimio lao. Hawana uwezo wowote wa kikanuni wa kuujadili mkoa wa pwani na ukizingatia kuwa baraza kuu la vijana la UVCCM Taifa lilokutana karibuni halikutoa tamko lolote kuhusiana na tamko la vijana wa mkoa wa pwani.
Hofu yangu kubwa ni kuwa nini kinawafanya vijana wenzangu hawa watumie muda wao kujadili matamko ya mikoa mingine badala ya kushughulika na changamoto za vijana wenzetu kuanzia kwenye ngazi ya mashina hadi kwenye ngazi ya mkoa wetu.
Tunahitaji tafakuri ya kina sana kama vijana ili tuweze kufanya mambo kwa maslahi ya chama chetu cha mapinduzi na nchi yetu kwa ujumla.
Ahsanteni sana kwa kunisikiliza.
MWISHO