MREJESHO; Shida ya mkojo

MREJESHO; Shida ya mkojo

Kinjekitile Jr

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2021
Posts
592
Reaction score
1,698
Wakuu ni matumaini yangu mu bukheri wa afya kabsa;

Mwezi uliopita nilikuja hapa kwenye hili jamvi nikaeleza kuhusu shida ya mkojo iliokuwa inanikabili na wengi wenu mkanishauri niende hospital nikafanyiwe uchunguzi zaidi ili nifahamu nini kinanikabili.Wengi wenu mli-predict uenda ikawa ni Urethral stricture au Tezi dume.

Wiki hii(14 February)nimeenda Bugando referral hospital,wamenifanyia kitu kinaitwa Cystoscope na wakabaini kuwa mrija wa mkojo(urethra) upo vizuri kabsa ila ninasumbuliwa na kichocho yaani kuna mazalia makubwa sana ya mayai ya kichocho ambao wamepelekea kupata haja ndogo ya kusua sua.Hivyo wamenipatia vidonge niweze kutumia

Je,kichocho kinaweza kusababisha kupata haja ndogo mbovu kama mgonjwa wa Tezi dume au urethral stricture…?

Lakini pia niliwekewa catheter (mpira wa kutolea mkojo),je ni upi muda muda sahihi wa kukaa na hiyo catheter,maana nahitaji nirudi kwenye shughuli zangu za kulijenga taifa letu pendwa la tanzania🇹🇿

Tafadhali,Mjuzi wa haya mambo anisaidie.

SOMA: Je, kuna madhara ya kufanyiwa upasuaji njia ya mkojo?
 
Wakuu ni matumaini yangu mu bukheri wa afya kabsa;

Mwezi uliopita nilikuja hapa kwenye hili jamvi nikaeleza kuhusu shida ya mkojo iliokuwa inanikabili na wengi wenu mkanishauri niende hospital nikafanyiwe uchunguzi zaidi ili nifahamu nini kinanikabili.Wengi wenu mli-predict uenda ikawa ni Urethral stricture au Tezi dume...
Mkuu endelea na kutumia dawa za hospitali kwa muda wa mwezi mmoja usipo pona nitafute kwa wakati wako ili nipate kukutibia maradhi yako ya kichocho kwa dawa zangu za asili na utapona kabisa maradhi yako na kurudi hali yako kama ya zamani uguwa pole.

UGONJWA WA KICHOCHO (BILHARZIA)​

Tatizo hili huwapata watu wengi hasa watoto wanaocheza katika madimbwi ya maji wakati wa mvua au wanapotumia maji ambayo yana vijidudu vya maradhi hayo. Vijidudu vya kichocho humuingia binadamu na kwenda kuishi katika kibofu cha mkojo au utumbo wake.

Kwa kawaida kimelea cha kike hutaga mayai ambayo hutoka kwa mtu mwenye ugonjwa huo na kuingia katika maji ikiwa mtu huyo atakojolea maji hayo au wakati wa haja kubwa. Mayai hayo huanguliwa na kutoa viluilui ambavyo hupenya kwa konokono wa majini. Viluilui hawa baada kutoka kwenye mwili wa konokono huweza kumuingia binadamu na kupenya katika ngozi na kwenda kutulia ktka mishipa ya ini ambapo hukomaa na baada ya hapo hutoka na kuingia katika mishipa ya kibofu cha mkojo na njia ya haja kubwa katika utumbo mpana.

Mgonjwa asipotibiwa haraka hupata matatizo katika njia ya haja kubwa na kibofu cha mkojo na wakati mwingine mayai ya kichocho huingia katika uti wa mgongo au katika ubongo na kusababisha matatizo.

DALILI
Kupatwa na homa siku 30 baada ya kunywa maji yenye maambukizi
Kikohozi kikavu na kujihisi kuchoka.
Baadaye damu huanza kutoka kwenye mkojo na haja kubwa lakini hatua hii ni baada ya ugonjwa kukomaa.


Madhara ya Kichocho

  • Kansa ya kibofu cha mkojo (cancer of urinary bladder)
  • Figo kushindwa kufanya kazi
  • Cor pulmonale
  • Gastrointestinal bleeding - Kuvuja damu ndani ya mwili hasa katika mfumo mzima wa chakula
  • Portal hypertension
  • Seizures - Kifafa au degedege
  • Reflex nephropathy
Jinsi ya kuzuia kichocho

  • Kuondoa na kuangamiza konokono waliopo kwenye maji au ambao hupenda kuishi kwenye maji ambao ni muhimu katika mzunguko wa kuuwaji wa vimelea vinavyoleta kichocho kwa kutumia Acrolein, copper sulfate na niclosamide.
  • Kwa sasa kuna utafiti unaendelea kwa ajili ya kutafuta chanjo ya ugonjwa huu wa kichocho.
USHAURI
Kichocho ni ugonjwa unaotibika haraka kwa dawa iwapo itabainika mapema.
Watoto wazuiwe kuogelea katika madimbwi au maji yaliyosimama.
Kunywa maji masafi na salama.
Wanaoish kando ya mito, maziwa na bahari wasikanyage maji hayo bila kuwa na viatu maalumu vya kuzuia maji kupenya na mabwawa yote ya kuogelea yawekwe dawa ya kuua vijidudu.

KICHOCHO (Biliharzia) NI UGONJWA HATARI.jpg

Aina za Konokono wanaoambukiza Kichocho na wale wasio ambukiza. Sehemu wanaopenda kukaa Konokono

 
Mkuu endelea na kutumia dawa za hospitali kwamuda wa mwezi mmoja usipo pona nitafute kwa wakati wako ili nipate kukutibia maradhi yako ya kichocho kwa dawa zangu za asili na utapona kabisa maradhi yako na kurudi hali yako kama ya zamani uguwa pole...
Asante sana mkuu nitafanyia kazi ushauri wako
 
Mkuu endelea na kutumia dawa za hospitali kwamuda wa mwezi mmoja usipo pona nitafute kwa wakati wako ili nipate kukutibia maradhi yako ya kichocho kwa dawa zangu za asili na utapona kabisa maradhi yako na kurudi hali yako kama ya zamani uguwa pole.

UGONJWA WA KICHOCHO (BILHARZIA)​

Tatizo hili huwapata watu wengi hasa watoto wanaocheza katika madimbwi ya maji wakati wa mvua au wanapotumia maji ambayo yana vijidudu vya maradhi hayo. Vijidudu vya kichocho humuingia binadamu na kwenda kuishi katika kibofu cha mkojo au utumbo wake.

Kwa kawaida kimelea cha kike hutaga mayai ambayo hutoka kwa mtu mwenye ugonjwa huo na kuingia katika maji ikiwa mtu huyo atakojolea maji hayo au wakati wa haja kubwa. Mayai hayo huanguliwa na kutoa viluilui ambavyo hupenya kwa konokono wa majini. Viluilui hawa baada kutoka kwenye mwili wa konokono huweza kumuingia binadamu na kupenya katika ngozi na kwenda kutulia ktka mishipa ya ini ambapo hukomaa na baada ya hapo hutoka na kuingia katika mishipa ya kibofu cha mkojo na njia ya haja kubwa katika utumbo mpana.

Mgonjwa asipotibiwa haraka hupata matatizo katika njia ya haja kubwa na kibofu cha mkojo na wakati mwingine mayai ya kichocho huingia katika uti wa mgongo au katika ubongo na kusababisha matatizo.

DALILI
Kupatwa na homa siku 30 baada ya kunywa maji yenye maambukizi
Kikohozi kikavu na kujihisi kuchoka.
Baadaye damu huanza kutoka kwenye mkojo na haja kubwa lakini hatua hii ni baada ya ugonjwa kukomaa.


Madhara ya Kichocho

  • Kansa ya kibofu cha mkojo (cancer of urinary bladder)
  • Figo kushindwa kufanya kazi
  • Cor pulmonale
  • Gastrointestinal bleeding - Kuvuja damu ndani ya mwili hasa katika mfumo mzima wa chakula
  • Portal hypertension
  • Seizures - Kifafa au degedege
  • Reflex nephropathy
Jinsi ya kuzuia kichocho

  • Kuondoa na kuangamiza konokono waliopo kwenye maji au ambao hupenda kuishi kwenye maji ambao ni muhimu katika mzunguko wa kuuwaji wa vimelea vinavyoleta kichocho kwa kutumia Acrolein, copper sulfate na niclosamide.
  • Kwa sasa kuna utafiti unaendelea kwa ajili ya kutafuta chanjo ya ugonjwa huu wa kichocho.
USHAURI
Kichocho ni ugonjwa unaotibika haraka kwa dawa iwapo itabainika mapema.
Watoto wazuiwe kuogelea katika madimbwi au maji yaliyosimama.
Kunywa maji masafi na salama.
Wanaoish kando ya mito, maziwa na bahari wasikanyage maji hayo bila kuwa na viatu maalumu vya kuzuia maji kupenya na mabwawa yote ya kuogelea yawekwe dawa ya kuua vijidudu.

View attachment 2122088

Aina za Konokono wanaoambukiza Kichocho na wale wasio ambukiza. Sehemu wanaopenda kukaa Konokono

Mimi kuna tatizo linanisumbua kuna muda inatokea kama siku mbili na kukata mpk miezi miwili , yaani nikikojoa baada ya mkojo wote kumalizika unastop km sekunde kadhaa una kuja mkojo wa mwisho mchache mchafu una rangi kuelekea km damu ya mzee lkn sipati maumivu yoyote imepita miaka sasa nahofia isije kuwa tatizo kubwa naomba muongozo.
 
Mimi kuna tatizo linanisumbua kuna muda inatokea kama siku mbili na kukata mpk miezi miwili , yaani nikikojoa baada ya mkojo wote kumalizika unastop km sekunde kadhaa una kuja mkojo wa mwisho mchache mchafu una rangi kuelekea km damu ya mzee lkn sipati maumivu yoyote imepita miaka sasa nahofia isije kuwa tatizo kubwa naomba muongozo.
Nenda haraka hospitali huenda una matatizo kwenye figo au njia ya mkojo au kibofu cha mkojo wako kina matatizo nenda ukapime hospitali haraka iweze kanavyo kabla halijawa tatizo kubwa na sugu .
 
Nenda haraka hospitali huenda una matatizo kwenye figo au njia ya mkojo au kibofu cha mkojo wako kina matatizo nenda ukapime hospitali haraka iweze kanavyo kabla halijawa tatizo kubwa na sugu .
Shukrani ,kwa dar hospitali gani nzuri kwa mambo ya mkojo na kibofu ?
 
Shukrani ,kwa dar hospitali gani nzuri kwa mambo ya mkojo na kibofu ?
Nenda Hospitali ya muhimbili Sehemu ya kulipia bei yake itakuwa ni poa kuliko hospitali za Watu binafsi. Au kama una pesa nenda hospitali ya Wahindi Hindul Mandal ipo maeneo ya upanga aka uhindini jiji Dar.au nenda hospitali ya Ağ khan pia nzuri kwa kupima mkojo.
 
Nenda Hospitali ya muhimbili Sehemu ya kulipia bei yake itakuwa ni poa kuliko hospitali za Watu binafsi. Au kama una pesa nenda hospitali ya Wahindi Hindul Mandal ipo maeneo ya upanga aka uhindini jiji Dar.au nenda hospitali ya Ağ khan pia nzuri kwa kupima mkojo.
Daktari upo? Siku nyingi sana nimekumbuka topics zako. Tiba asili za pressure na sukari zipo? Vipi kuhusu kitengo cha tiba asili pale muhimbili kina tofautiana vipi na tiba za wamasai?
 
me saingine mkojo ukinibana nkitaka kukujoa sekunde hata 15 una delay ila sina maumivu
 
Back
Top Bottom