officialBossmtoto
JF-Expert Member
- Jul 1, 2019
- 369
- 1,178
Kama mnakumbuka kisa kilichonikumba mpaka kupelekea kujifukuzisha kazi huku nikiacha msako wa kunitafuta ukiendelea basi leo nina furaha kuwaletea mrejesho. Tamaa imeniponza, nimeamua kujiachisha kazi
Sitaki kuzungumza sana maisha pale Morogoro, ila kiukweli changamoto zilikuwa nyingi. Nilianza kulala kituoni siku mbili nikiuza simu nikapata pesa kidogo nikapanga kwenye magetto ya uchochoroni. Mengi nilipitia ila nilikuwa nafatilia kwa karibu hali ya usalama wangu huku Dar.
Nilipata msaada kutoka kwa Jamaa mmoja huku JF (jina kapuni) ambae aliniunganisha na Mabinti wawili ambao wao walinihakikishia kwamba yule dada atarejesha ile pesa.
Nilipata hata jeuri ya kumsaka boss kwa namba mpya na nikamuahidi kabla ya mwezi wa pili kuisha hela yake yote itarejea nitaweka na faida.
Kweli tarehe 20/02/2023 nilipigiwa sim nikadaka abood nikaja Dar. Wale mabinti wakaniambia niwape account wakaniwekea 7,000,000 alafu wakaniambia tumekuwekea yote wewe angalia utatuonaje kwa kazi yetu.
Nilipata wasiwasi kidogo kutaka kujua wamemfanyaje yule dada, wakasema ni mzima na hawajamgusa popote ila hatakaa arudie. Niliomba niwape milioni moja sababu ndo kwanza naanza mapambano upya, wakakubali ila nikawaahidi baada ya miezi miwili nitawapa tena milioni nyingine.
Jamaa wa humu Jukwaani naye nikampa shukrani ya laki tano. Boss nilimpelekea hela Cash akanirejesha kazini. Kesho jumatatu naanza rasmi mapambano.
Nafuraha isio kifani. Japo sina hata shilingi ila nitayaweza yote. Hapa nimeongea na mwanangu amenijenga 20.000 ya kuanzia week.
NIMEIJUA NGUVU YA MMU, WALE WAOMBA USHAURI MSIKATE TAMAA
Sitaki kuzungumza sana maisha pale Morogoro, ila kiukweli changamoto zilikuwa nyingi. Nilianza kulala kituoni siku mbili nikiuza simu nikapata pesa kidogo nikapanga kwenye magetto ya uchochoroni. Mengi nilipitia ila nilikuwa nafatilia kwa karibu hali ya usalama wangu huku Dar.
Nilipata msaada kutoka kwa Jamaa mmoja huku JF (jina kapuni) ambae aliniunganisha na Mabinti wawili ambao wao walinihakikishia kwamba yule dada atarejesha ile pesa.
Nilipata hata jeuri ya kumsaka boss kwa namba mpya na nikamuahidi kabla ya mwezi wa pili kuisha hela yake yote itarejea nitaweka na faida.
Kweli tarehe 20/02/2023 nilipigiwa sim nikadaka abood nikaja Dar. Wale mabinti wakaniambia niwape account wakaniwekea 7,000,000 alafu wakaniambia tumekuwekea yote wewe angalia utatuonaje kwa kazi yetu.
Nilipata wasiwasi kidogo kutaka kujua wamemfanyaje yule dada, wakasema ni mzima na hawajamgusa popote ila hatakaa arudie. Niliomba niwape milioni moja sababu ndo kwanza naanza mapambano upya, wakakubali ila nikawaahidi baada ya miezi miwili nitawapa tena milioni nyingine.
Jamaa wa humu Jukwaani naye nikampa shukrani ya laki tano. Boss nilimpelekea hela Cash akanirejesha kazini. Kesho jumatatu naanza rasmi mapambano.
Nafuraha isio kifani. Japo sina hata shilingi ila nitayaweza yote. Hapa nimeongea na mwanangu amenijenga 20.000 ya kuanzia week.
NIMEIJUA NGUVU YA MMU, WALE WAOMBA USHAURI MSIKATE TAMAA