Mrejesho:mwalimu anataka kuitoa roho...

Mrejesho:mwalimu anataka kuitoa roho...

Powel Mizengo

Senior Member
Joined
Jan 20, 2014
Posts
126
Reaction score
24
Nadhani mtakumbuka wiki mbili zimepita tangu nilipowaeleza kisa cha yule rafiki yangu na mchumba wake ambaye ni mwalimu huko Moro!

Baada ya kupokea maoni na ushauri wenu wanajamvi;hasa ukizingatia wengi wenu mlishauri asirudiane naye,nami nilimshauri hivyohivyo.

Chakushangaza jamaa aliendelea kumfatilia huyu mwanamke na hivi sasa navyowaandikia thread hii,Jamaa yangu yupo Hosp amejeruhiwa vibaya na yule msela ambaye alikuwa akitoka na mchumba wake!

Kumbe siku ya Ijumaa ya wiki iliyopita, rafiki yangu aliamua kwenda tena Moro na alipofika home kwa demu wake hakumkuta,alipopeleleza akaambiwa kuwa mchumba wake yupo Bar iitwayo Makuti pale Msamvu na mwanaume mwingine wakinywa Mvinyo!

Ndipo jamaa alienda mpaka pale na kilichotokea ni varangati kubwa sana na sasa jamaa yangu yupo hospital kwa matibabu kwani amepigwa chupa ya kichwani na uso umevimba manundu kadhaa !

Juhudi za kumkamata mtuhumiwa zinaendelea; na yule mwanamke pia amekwishakamatwa ila yupo nje kwa mdhamana!!!

Nilijitahidi sana kumpa ushauri kadri wanajamvi mlivyonipa ushauri but jamaa ndo hayo yalomkuta!

Nawaombeni msaada wa sala na maombi ili jamaa yangu apate kupona kwa haraka!

Asanteni!
 
Papuchi itamtoa karoho.....shauri yake.
 
mpe pole.....hakuna kitu kizuri duniani kama kukubaliana na ukweli... utakuepusha na shida nyingi
 
Hayo ndo mahaba niue....labda akipona ndo atajua kuwa mwanamke hamfai
 
pole yake,
Akubali matokeo tu, kama aliweza kumpata huyo ataweza pia kumpata mwingine
 
Pussy and money...so many people get killed for those two things
 
Hayo ndo mahaba niue....labda akipona ndo atajua kuwa mwanamke hamfai
Daudi1 nani kasema?Nakwambia akitoka hosp kitu cha kwanza ataenda kufuta kesi na kumtafuta huyo mchumba wake malaya kumuomba msamaha kama vile yeye ndiye kakosa!Chezea papuchi wewe??

Alafu sijui wanaume wengine tukoje,mtu hata hujamuoa,umethibitisha ni malaya,unamg'ang'ania wa nini?Mbona papuchi ziko nyingi tu barabarani?Tena kuna uzi humu wa maeneo zinapopatikana?

Nasema,apigwe tu,apigwe na apigwe tu!
 
Last edited by a moderator:
Mapenzi jamani, huyo mwl ndio anayependwa jamaa. Hiyo ndio inaitwa 'no matter what'.
 
Hahahhahhaaa hataki serikali mbili? anataka tatu? ohoooooo pole yake, amuulize Samsoni na Dalila
 
Huyu wa Tanga nini? Maana inaonekana anayajua mapenzi labda tofauti na wanaume wengine. Pole zake.
 
Mapenzi nipoteze,mpe pole ,nalijua jamaa litarudia tena tu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom