Mrejesho: Matokeo ya Usaili kwa kazi niliyotangaza humu

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,185
7,491
Wakuu nawasalimu.
Nilitangaza nafasi ya kazi humu ya usimamizi wa biashara ambapo kigezo cha kwanza nilichokuwa nimetoa ni uaminifu.
Nafasi ya kazi kwa mtu mwaminifu sana


Matokeo ni kama ifuatavyo:

(a) Watu 81 waliomba kazi hii.
(b) Watu 29 walijibu maswali niliyouliza ya kupima uaminifu na wakathibitisha kuwa uaminifu wao hauna shaka, hivyo kupita kwenye hatua ya kwanza ya usaili.
(c) Katika hatua ya pili ya usaili, nilichagua waombaji 15 kutoka kwenye 29, hapo juu, nikawatumia fedha kwa tigo/mpesa kwenye namba walizonipa (kutoka kwenye namba wasiyoijua bila maelekezo yoyote.

Kiwango nilichotuma kwa kila mmoja ni kati ya ya 2000 - 10,000/=. Kati ya hao 15, 13 walipokea hela wakazilamba bila hata kuuliza mtumaji kama alikosea namba au alituma kwa makusudi na kama alituma kwa makusudi alituma za nini.(hatua hii imewafanya kushindwa usaili).

Watu wawili waliuliza, nikawambia nimetuma kwa makosa, wakaonesha dhamira ya kunirudishia ndio nikawajulisha kuwa ilikuwa ni sehemu ya pili ya usaili wa kazi hii. (hao wawili wamefaulu usaili kwenye hatua hii) na kati yao mmoja atapewa kazi.

Nawatakia kila la heri.
 
Wakuu nawasalimu.
Nilitangaza nafasi ya kazi humu ya usimamizi wa biashara ambapo kigezo cha kwanza nilichokuwa nimetoa ni uaminifu.
Nafasi ya kazi kwa mtu mwaminifu sana



Matokeo ni kama ifuatavyo:

(a) Watu 81 waliomba kazi hii.
(b) Watu 29 walijibu maswali niliyouliza ya kupima uaminifu na wakathibitisha kuwa uaminifu wao hauna shaka, hivyo kupita kwenye hatua ya kwanza ya usaili.
(c) Katika hatua ya pili ya usaili, nilichagua waombaji 15 kutoka kwenye 29, hapo juu, nikawatumia fedha kwa tigo/mpesa kwenye namba walizonipa (kutoka kwenye namba wasiyoijua bila maelekezo yoyote. Kiwango nilichotuma kwa kila mmoja ni kati ya ya 2000 - 10,000/=. Kati ya hao 15, 13 walipokea hela wakazilamba bila hata kuuliza mtumaji kama alikosea namba au alituma kwa makusudi na kama alituma kwa makusudi alituma za nini.(hatua hii imewafanya kushindwa usaili).Watu wawili waliuliza, nikawambia nimetuma kwa makosa, wakaonesha dhamira ya kunirudishia ndio nikawajulisha kuwa ilikuwa ni sehemu ya pili ya usaili wa kazi hii. (hao wawili wamefaulu usaili kwenye hatua hii) na kati yao mmoja atapewa kazi.

Nawatakia kila la heri.
So interesting.
 
Wakuu nawasalimu.
Nilitangaza nafasi ya kazi humu ya usimamizi wa biashara ambapo kigezo cha kwanza nilichokuwa nimetoa ni uaminifu.
Nafasi ya kazi kwa mtu mwaminifu sana


Matokeo ni kama ifuatavyo:

(a) Watu 81 waliomba kazi hii.
(b) Watu 29 walijibu maswali niliyouliza ya kupima uaminifu na wakathibitisha kuwa uaminifu wao hauna shaka, hivyo kupita kwenye hatua ya kwanza ya usaili.
(c) Katika hatua ya pili ya usaili, nilichagua waombaji 15 kutoka kwenye 29, hapo juu, nikawatumia fedha kwa tigo/mpesa kwenye namba walizonipa (kutoka kwenye namba wasiyoijua bila maelekezo yoyote. Kiwango nilichotuma kwa kila mmoja ni kati ya ya 2000 - 10,000/=. Kati ya hao 15, 13 walipokea hela wakazilamba bila hata kuuliza mtumaji kama alikosea namba au alituma kwa makusudi na kama alituma kwa makusudi alituma za nini.(hatua hii imewafanya kushindwa usaili).Watu wawili waliuliza, nikawambia nimetuma kwa makosa, wakaonesha dhamira ya kunirudishia ndio nikawajulisha kuwa ilikuwa ni sehemu ya pili ya usaili wa kazi hii. (hao wawili wamefaulu usaili kwenye hatua hii) na kati yao mmoja atapewa kazi.

Nawatakia kila la heri.
Aaaaahhh watu mna makusudi kweli hapo n sawa na kumshika simba sharubu wakt ananjaa
 
Kwenye masuala ya hela bhana ni changamoto uaminifu ila mtu tsh 5000 au 9000 itakusaidia nini?

Mimi kuna siku nilitoa hela M-pesa 40,000, nilipokea meseji ya ila sikuifungua kuona imeandikwa nini na wakala nae akawa yuko bize na smatfon kuona tu meseji imekuja kwangu akanipa hela.

Kufika mbele naifungua ile meseji nikaona mmh mbona inanitaarifu kuwa transaction imekuwa cancelled kutokana na tatizo la mtandao?

Sikujali nikasema labda wakala ye alipata meseji ....sasa siku nyingine nanunua muda wa maongezi naambiwa salio ni 55000 wakati najua nilitoa 40 imebaki kumi na kitu ndo nikakumbuka ile meseji iliyoingia kwangu nilipotoa hela.

Nikamrudia yule wakala nikamuuliza ananionyesha na hesabu ya siku hiyo kwamba ni kweli alipata shoti...nikampa hela yake ila ndo hakusema hata asante! Hata kama tenda wema nenda zako ila mmh nilimshangaa sana sijui kabila gani yule neno asante kutamka gumu!
 
Vizuri sana. Ila hao 81 wote uliwatumia hayo maswali? Kama ndio, deadline mpaka ukapata hao 81 ilikuwa lini? Maana nami nilikupm ila UKWELI ni kwamba sikupata hayo maswali.

Waajili wote wawili mkuu kama usaili umeisha au pendekeza huyo jamaa kwa watu wako.
 
Kwenye masuala ya hela bhana ni changamoto uaminifu ila mtu tsh 5000 au 9000 itakusaidia nini? nikampa hela yake ila ndo hakusema hata asante! Hata kama tenda wema nenda zako
Hongera sana dada. watu wana maudhi mengi ila kabla ya kumlaumu mwenzako wewe tekeleza wajibu wako.mfanyie mwanzako ambayo nawe ungetamani ufanyiwe.
keep it up na nakuambia siku moja matendo yako yatakurudia kwa namna ambayo hukuwahi kuifikiria. Kuna kitu kinaitwa "Karma". Karma ni mujarab!
 
Vizuri sana. Ila hao 81 wote uliwatumia hayo maswali? Kama ndio, deadline mpaka ukapata hao 81 ilikuwa lini? Maana nami nilikupm ila UKWELI ni kwamba sikupata hayo maswali.
mkuu, wewe sijakufanyia usaili awamu ya pili. nilichagua sample kama nilivyoeleza hapo juu. Ila kama upo serius, nitakufanyia usaili.
 
Kwenye masuala ya hela bhana ni changamoto uaminifu ila mtu tsh 5000 au 9000 itakusaidia nini? Mimi kuna siku nilitoa hela M-pesa 40,000, nilipokea meseji ya ila sikuifungua kuona imeandikwa nini na wakala nae akawa yuko bize na smatfon kuona tu meseji imekuja kwangu akanipa hela. Kufika mbele naifungua ile meseji nikaona mmh mbona inanitaarifu kuwa transaction imekuwa cancelled kutokana na tatizo la mtandao? Sikujali nikasema labda wakala ye alipata meseji ....sasa siku nyingine nanunua muda wa maongezi naambiwa salio ni 55000 wakati najua nilitoa 40 imebaki kumi na kitu ndo nikakumbuka ile meseji iliyoingia kwangu nilipotoa hela. Nikamrudia yule wakala nikamuuliza ananionyesha na hesabu ya siku hiyo kwamba ni kweli alipata shoti...nikampa hela yake ila ndo hakusema hata asante! Hata kama tenda wema nenda zako ila mmh nilimshangaa sana sijui kabila gani yule neno asante kutamka gumu!
Haha atakua mnyaturu uyo awajuag kusema asante
 
Back
Top Bottom