Mrejesho biashara ya madini 'third season'

Usage mawe bure alafu unatoa 40% ya mawe kwa mwnye klemu ndo nn hii bure sasa??.mpaka sasa una tani.200 almost hizo ni zaidi ya tank.6 za tani.3 kama sample inasoma 8+ppm alafu unalia eti mtaji mdogo,hyo unachenjua na faida juu ya kutosha tena iliopitliza ila subilia ukakutane na changamoto wizi wa carbon ukienda plant na wizi wa dhahabu elusion uje usimulie vizuri hadithi yako umu
 
Eeh eeh
 
Nakushaur shirikisha wataalam upate ushaur ndugu yangu...usije ukaja shtuka kumbe ushapoteza pesa nying...tushapita huko kaka...

Dhahab ya inch hii inataka ufaham unafanya nin...unaweza spend all ua time kumbe mahala hapo ppm znasoma ndogo sana .dhahab ipo ila ni fractions...kama unapesa na mtaj nashaur nenda kawekeze na kuhangaika eneo la kanda ya ziwa kitaalam/ki geologia tunaita nyanza region..hilo ndo limefanyiwa utafit na makampun makubwa dunian na ndomana migod mikubwa yote Tz ya dhahab iko ukanda huo kuanzia tabora mwanza kwenda mbele huko shinyanga..huku kwingne dhahab ni ya kubahatisha mno..ushaur tuu ndugu
 
Ila Crusher ya 30mm plate bei yake ni 7.5-8.5mil kwa sasa
Hizi zinabeba hadi viroba 6 kama una gololi zakutosha.

Ambapo unapewa Engine ya 20HP

Gololi 600 60mm na 80mm

Hapo naongelea Shinyanga Best/B52
 
Hongera sana nimekufuatilia toka mwanzo sema ni vile dunia imekua sio rafiki tena niko Mbeya ningekuja nijifunze kitu hila nakutakia mafanikio na mapambano mema tutakutana uko
 
Sijui kama itawezekana tena manake keshawekeza huko vya kutosha
 
Mkuu mcrounmj hongera sana kwa mapambano. Nilikua Chunya mwezi wa 12 nimejionea uwekezaji unaonedelea huko. Kila la kheri kwenye harakati zako.

Aidha unapitisha rudio lako mwaloni? Kama unapitisha si unaokota vipoints vya dhahabu hapo ambayo ukiuza ingeweza kuendelea kuendesha kazi especially kama rudio lako linasoma vizuri hivyo 8ppm ni concentration kubwa. Ningeshauri nenda plant sasa tayari rundo lako ni kubwa enough na bado uzalishaji unaendelea.

Ukienda plant Hakikisha unapata mkemia msomi na mzoefu maana huyo tu anaweza kukuharibia shughuli yote na uchenjuaji hauna kurudi nyuma, ukifika elution kuwa makini sana yani zaidi ya sana kuna wizi wa carbon huko hatari although umepungua miaka ya sasa wanavyodai.

Afu unasagia watu wengine pia kwa malipo? Nadhani hiki nacho kingeweza kuwa chanzo kingine cha mapato.

Toka uanze kuchimba michirizi inapotea na kurudi au base yako ni kubwa ni kuvuna tu mawe?
 
Hivi karasha lipi ni zuri hili ball mill crusher au hammer mill crusher nakuna hii jaw crusher naomben msaada hapo
 

Pole na majukumu na hongera sana mkuu ningependa kujulishwa sehemu husikua au kijiji unapofanya kazi zako maana hiyo ppm ya 8 ni nzuri sana
 
Hivi karasha lipi ni zuri hili ball mill crusher au hammer mill crusher nakuna hii jaw crusher naomben msaada hapo

Hivi karasha lipi ni zuri hili ball mill crusher au hammer mill crusher nakuna hii jaw crusher naomben msaada hapo
Naamini mcrounmj na akina Mathare watakuelezea hili kwa undani na kwa ufasaha zaidi kwani wao wako field. Tusubiri tu!
 
I have to subscribe. Nina take note mkuu naanda dodoso langu nitaliweka hapa na PM. Ninafanya study baada ya mwaka ninunue mitambo na niweke 30m. Biashara ikianza kutembea naacha kazi
 
Mkuu nimekutumia PM
 

Chunya inazalisha zaidi ya kilo 300 ya gold kwa mwezi kwanini aende kanda ya ziwa?

Makampuni makubwa yanamitaji mikubwa na yanataka mzigo mkubwa, faida ya 100M kwake inaweza kuwa kubwa ila kwa GGM it's nothing so kila mtu anakula kwa urefu wa kamba yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…