Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Aliyekuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera, Venance Stanslaus Martin, ambaye pia ni mpwa wa Hayati Rais Dkt. John Pombe Magufuli, amechukua fomu ya kugombea ubunge wa Jimbo la Chato Kaskazini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Venance amefika katika Ofisi za CCM Wilaya ya Chato na kupokelewa na Katibu wa CCM wa wilaya hiyo, Charles Mazuri, na kukabidhiwa rasmi fomu ya kugombea nafasi hiyo ya uwakilishi.
Venance amefika katika Ofisi za CCM Wilaya ya Chato na kupokelewa na Katibu wa CCM wa wilaya hiyo, Charles Mazuri, na kukabidhiwa rasmi fomu ya kugombea nafasi hiyo ya uwakilishi.