Maramla
JF-Expert Member
- Jan 8, 2014
- 581
- 642
Kumekuwa na kelele nyingi zinazohusu utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa Nchini, awali vigezo vya kupingwa maendeleo ilikuwa "SERIKALI INAFANYA MIRADI ISIYOSAIDIA WATU WOTE".
Ununuzi wa ndege ulipingwa, ujenzi wa reli ulipingwa, mradi wa bwawa la kufua umeme ulipingwa hata elimu bila malipo ilipingwa.
Baada ya Mhe. Rais Magufuli na Serikali kukaza msuli na kuonesha matokeo chanya, wale wote waliopinga miradi hii kutekelezwa wamehamishia hasira zao Chato.
Kwanza nawapa pole sana kwakuwa maendeleo hayataweza kusimama kwakuwa mpinga maendeleo anapiga yowe.
Kwa wanaosoma maandiko matakatifu watakubaliana nami kuwa Yesu alipingwa alipoponya, alipofufua, alipofundisha pia. Mwisho walihamishia hasira zao kwenye uhai wake, lakini neno halikukoma.
Hivyo nchi itaendelea kusonga mbele na hata Msipoisema Chato basi mtaisema Tandahimba.
Ununuzi wa ndege ulipingwa, ujenzi wa reli ulipingwa, mradi wa bwawa la kufua umeme ulipingwa hata elimu bila malipo ilipingwa.
Baada ya Mhe. Rais Magufuli na Serikali kukaza msuli na kuonesha matokeo chanya, wale wote waliopinga miradi hii kutekelezwa wamehamishia hasira zao Chato.
Kwanza nawapa pole sana kwakuwa maendeleo hayataweza kusimama kwakuwa mpinga maendeleo anapiga yowe.
Kwa wanaosoma maandiko matakatifu watakubaliana nami kuwa Yesu alipingwa alipoponya, alipofufua, alipofundisha pia. Mwisho walihamishia hasira zao kwenye uhai wake, lakini neno halikukoma.
Hivyo nchi itaendelea kusonga mbele na hata Msipoisema Chato basi mtaisema Tandahimba.