Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,436
- 5,234
Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha ACT Wazalendo, Mhe. Luhaga Mpina, amesema Taifa linahitaji kukombolewa upya ili kudhibiti uonevu, rushwa, ufisadi na mateso kwa wananchi.
Akizungumza leo Agosti 18, 2025 mjini Shinyanga wakati wa zoezi la kuomba udhamini, Mpina amesema hatua hiyo ni muhimu ili kurejesha matumaini ya Watanzania na kujenga nchi yenye misingi ya haki na usawa.
“Nchi yetu inahitaji kukombolewa upya, nchi yetu inahitaji ukombozi mpya. Hatuwezi kunyamaza, tutaenda kuwafuta machozi Watanzania. Na chama ambacho kimeletwa kwa ajili ya kulikomboa Taifa hili ni ACT Wazalendo,” amesisitiza Mpina.
Akizungumza leo Agosti 18, 2025 mjini Shinyanga wakati wa zoezi la kuomba udhamini, Mpina amesema hatua hiyo ni muhimu ili kurejesha matumaini ya Watanzania na kujenga nchi yenye misingi ya haki na usawa.
“Nchi yetu inahitaji kukombolewa upya, nchi yetu inahitaji ukombozi mpya. Hatuwezi kunyamaza, tutaenda kuwafuta machozi Watanzania. Na chama ambacho kimeletwa kwa ajili ya kulikomboa Taifa hili ni ACT Wazalendo,” amesisitiza Mpina.