Mgombea Urais kupitia Chama cha ACT Wazalendo, Luhaga Joelson Mpina, amewasili katika ofisi za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Tofauti na wagombea wengine wa vyama vingine, wengi wao wakifika na matarumbeta au vikundi vya ngoma, Mpina ameambatana na idadi ndogo ya wanachama wa chama hicho.